maandamano oktoba 2025

No Wikipedia entry exists for this tag
  1. Cute Wife

    GE2025 Ukivaa nguo za CHADEMA, au kuongelea maandamano unawekwa gerezani hadi uchaguzi upite, jishikilie huo mdomo mpaka MO29!

    Wakuu, Hiki ndicho kinaendelea wakati huu, ukionekana umevaa gwanda za CHADEMA au unajisogoze sogeza na kuwa na viashiria vya kuwa mwana CHADEMA unadakwa chap, wanakutia selo, ndugu zako wanaambiwa hutoki mpaka uchaguzi uishe, hivyo wajipange tu kukuletea chakula na mahitaji muhimu...
  2. Cute Wife

    GE2025 Shabiki wa Simba aliyevaa jezi iliyoandikwa "I Love Lissu" hajulikani alipo

    Wakuu, Shabiki hiyo anayefahamika kwa jina la Abaissa Georgina (KE) alikuwa amevaa jezi yenye maneno "I LOVE LISSU" mgongoni, alipokuwa anaingia uwanjani akiwa ameongozana na ndugu zake kuangalia mechi ya Simba dhidi ya Nsingizini leo Oktoba 26, 2025. Wakati anaingia uwanjani alikamatwa na...
  3. M

    GE2025 Jeshi la Polisi: Atakayethubutu kuvunja sheria Oktoba 29 asitulaumu kwa hatua itakayochukuliwa dhidi yake

    Tarehe 29.10.2025 siku ya Jumatano ni siku muhimu sana katika Taifa letu, ambapo Watanzania watatekeleza haki yao ya kikatiba ya kupiga kura kwa ajili ya kuchagua Viongozi watakao waongoza katika nafasi ya Urais, Wabunge na Madiwani. Jeshi la Polisi kupitia taarifa hii, lingependa...
  4. PAYE

    GE2025 Mgombea Urais NLD, Doyo: Watanzania msithubutu kuandamana mtachafua nchi

    Mgombea Urais wa Tanzania kupitia chama cha NLD, Doyo Hassan Doyo amewasihi Watanzania kufanya uchaguzi kwa amani na kutoshiriki maandamano. "Nchi inapokuwa na watu welevu, inakuwa na kelele. Rai yangu kwa Watanzania wasithubutu kutoka kuandamana; watachafua nchi."
  5. Mafyangula

    GE2025 Kamanda Marwa Kisyeri: Msidanganyike kuvuruga amani ya nchi na kutojihusisha na maandamano yasiyo na tija

    Amani inazidi kupigiwa debe kila kukicha. Na jeshi la polisi wakiwa msatari wa mbele sana kipindi hichi. Uchaguzi ukiisha hapa hizi bwebwe zote kwisha ================== Mkaguzi Msaidizi wa Kata Bulongwa wilayani Makete Mkoa wa Njombe Marwa Kisyeri Oktoba 24,2025 ametoa elimu kwa vijana...
  6. DuaZaMama

    GE2025 Ngombale Mwiru awavaa wakuu wa mikoa wanaoonya kuhusu maandamano, asema wanatafuta teuzi

    Mgombea Urais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Kunje Ngombale Mwiru AAFP ameendelea na kampeni katika Mkoa wa Tabora ndani ya Wilaya ya Nzega. Mgombea Urais huyo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kunje Ngombale Mwiru amewavaa wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya ambao wanatishia wananchi...
  7. Waufukweni

    GE2025 Zitto: Oktoba 29 mkapige Kura hakutakuwa na vurugu yoyote

    Mgombea Ubunge Jimbo la Kigoma Mjini kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amewataka wasimamizi wa uchaguzi kuhakikisha zoezi la upigaji kura linakuwa la wazi kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi mkuu. "Ninajua watu wanahofu na uchaguzi, wengine wanauliza tukikupa kura hawa watu...
  8. PAYE

    GE2025 ACP John Imori: Maandamano bila kibali ni haramu na hili ndilo Tishio kubwa kabla ya Uchaguzi

    "Wale wanaotamani kuingia barabarani nawakataza, wasithubutu, ni marufuku, wasitoke mtu hata mmoja sababu maandamo bila kibali ni haramu" ACP John Imori.
  9. Matovu Godfrey

    GE2025 Wanajeshi kutoka Uganda wadaiwa kuingia Tanzania kuzuia maandamano ya Gen Z Oktoba 29

    Jana usiku, wanajeshi wa UPDF walivuka hadi Tanzania kupitia ziwa Victoria kwa boti kadhaa. Walikuwa chini ya uongozi wa Luteni Kanali Nsaju. Wapo kusaidia Samia kuanzisha vurugu dhidi ya vijana wa Kitanzania wanaotishia kufanya fujo. Haamini jeshi lake kwamba watafuata maagizo yake kwa hivyo...
  10. Keynez

    GE2025 Mange Kimambi anaweza kuwa ni "Double agent" anayewasaidia anaowasema 'vibaya' kila siku

    Wiki kadhaa zilizopita niliwataja Mange Kimambi, Humphrey Polepole na Luhaga Mpina kama watu ambao sijaamini dhamira ya maneno na matendo yao ya kisiasa. Haya maneno niliyasema siku kadhaa kabla taarifa za kupotea kwa Polepole hazijatoka. Niliwahi kusema master plan ya siasa za CCM ni kuwa...
  11. Waufukweni

    GE2025 Samia: Mimi ndio Amiri Jeshi Mkuu wa Nchi, Oktoba 29 maandamano pekee yatakayotokea ni ya kwenda kupiga kura

    Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wafuasi wa chama hiko kujitokeza kupiga kura siku ya Oktoba 29, 2025, na kuwahakikishia kuwa hakutakuwa na maandamano zaidi ya maandamano ya kwenda vituoni kupiga kura. "Niwahakikishie tarehe 29...
  12. Waufukweni

    GE2025 Mzee Mpili: Wanaotaka kufanya maandamano wanatafuta matatizo

    Shabiki wa Klabu ya Yanga, Mzee Mpili amesema kuwa wanaotaka kuandamana Oct 29,2025 wanatafuta Matatizo Mzee Mpili ameyasema hayo Leo Oktoba 20,2025 katika uwanja wa Ujamaa Ikwiriri Wilayani Rufiji Mkoani Pwani Kwenye Mwendelezo wa Mikutano ya Kampeni za uchaguzi Mkuu 2025 ya Mgombea wa kiti...
  13. W

    GE2025 Mama Ramso: Yapata wiki mbili sasa wananizungusha tu lakini mwanangu sijamuona. Naomba mnisaidie apatikane

    Ramso ni msanii wa vichekesho na mtoto wa pekee kwa mama yake, ambaye inasemekana ametekwa na watu wasiojulikana baada ya kuposti video akimtaka Rais Samia ajiuzulu kwani hakuna anayemtaka. Mama yake ametoka hadharani kuomba msaada wa mwanaye kupatikana ikiwa ni wiki mbili toka mwanaye...
  14. Cute Wife

    GE2025 Kwanini tunasema kuna mtu mwingine anaendesha nchi? Hatuamini Samia anaweza kuwa ndio msimamia shoo mwanzo mwisho?

    Wakuu, Kumekuwa na hizi assumption kutoka pande mbalimbali kwamba Samia yupo tu kama geresha na nyuma yake ndio kuna mtu ambaye hasaaa ameshika usukani na kuamrisha kete zipelekwe kule ambako anataka yeye zifike! Hivi ni kwanini tunafikiria haya, kwanini tunaona kama Samia hawezi kuwa...
  15. Criss

    29 Oktoba, 2025 Ni siku ya kuionyesha Dunia kuwa unalipenda Taifa lako kwa vitendo

    Usijitazane ulivyo na usijione dhaifu , kwa namna ulivyo ni mtaji tosha wa kuyaleta mageuzi unayoyatamani kuyaona kwenye Taifa lako . Kitendo cha kutoka na kuungana na wenzako ,utakuwa umetimiza moja ya jambo kubwa sana kwenye sababu ya uwepo wako Duniani . Kwa maana utakuwa unefanikiwa...
  16. Cute Wife

    GE2025 Jinsi comedy inavyotumika kufikisha ujumbe wakati huu wa Uchaguzi. Ukishindwa kote hapa huwezi kukwama kuelewa

    Wakuu, Hapa hata kama unakuwa huelewi matamko makubwa makubwa, sijui maandiko marefu, hapa unaelewa! Ujumbe unafikishwa kama utani lakini ndio umefika hivyo, na unakaa akilini vizuri. Kama wanavyotumia sanaa kuhamasisha watu kuachana na maandamano, amani bila haki, na propaganda za kipuuzi...
  17. Cute Wife

    GE2025 Simba SC wamesaidia kusambaza taarifa ya Maandamano na MO 29 ikimaanisha Maandamano Oktoba 29. Hutaki kula jiwe!

    Wakuu, Kwani jamaa kasema uongo hapa Wakuu? Jezi za Simba zilizoandikwa MO 29 maana yake ni M - Maandamano O - October 29 - Hii haitaji hata tafsiri inajieleza, siku ya tar 29 ndio yenyewe! Simba wameupiga mwingi kuhakikisha Watanzania hata wa Nanjilinji wanapata taarifa kuhusu maandano...
  18. PAYE

    GE2025 Nassibu Kitabu: Samia ni lulu, msitishike na kitu chochote dola ipo, mkapige Kura

    Mgombea Udiwani wa Kata ya Jangwani, Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Nassibu Hassan Kitabu, ametoa wito kwa wananchi wa kata hiyo kutoogopa vitisho vinavyoenezwa na baadhi ya watu wanaopanga kuzuia Uchaguzi Mkuu kupitia maandamano. Akizungumza...
  19. PAYE

    GE2025 Ezra Chiwelesa: Kuandamana ni kuwanyima wengine Haki ya Kikatiba

    Mgombea Ubunge wa Biharamulo Mhandisi Ezra Chiwelesa amesema kuandamana siku ya kupiga kura ni kosa kisheria maana huko ni kuzuia uchaguzi na pia jambo hilo litafanya kuwanyima wengine haki ya Msingi ya Kupiga Kura.
  20. Waufukweni

    GE2025 Albert Chalamila: Nimesoma mitandaoni kuhusu fujo Oktoba 29, ndugu zangu mji wenu uko salama

    Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amesema kumekuwepo na baadhi ya maandiko mbalimbali mtandaoni kuwa Vijana na Makada wa Vyama vya siasa wanahamasisha maandamano siku ya Uchaguzi Mkuu Octoba 29, 2025 ambapo amewaonya wanaotaka kujaribu kufanya vitendo hivyo kwani hawatofanikiwa. Chalamila ameyasema...
Back
Top Bottom