Nadhani tumetafsiri vibaya kauli ya Makonda. Kwa nilivyoitazama Mimi alidhamiria kuonesha kazi anayoifanya ya kutetea wanyonge hata Mungu anaifurahia hivyo anaposimama Makonda Mungu anakua upande wake. Sasa mlitaka aseme akisimama na shetani amesimama?.......Nani amemfuata Makonda ili atoe...
Jana katusaidia mengi sana wananchi wa Mabwe pande. Sikubaliani na hoja kwamba ziara zake hazitatui matatizo. Jana tu tatizo la Maji, Ardhi na afya viliwekwa sawa.
Uvivu ni tabia ya mtu haihusiani na kuswali swala 5 wala kuhudhuria vikao vya dini. utafiti wako wa watu wawili hautoshi kuhitimisha hoja yako. pia naona hiyo ya mlokole umeiweka tu kubalance. yaleyale Radio iman Vs Radio Maria.
umenena vyema Mkuu. mkoani fursa bado ziko wazi na ukizitumia vizuri unapasua fasta. hatuwezi kujazana Dar ili tufanikiwe. hatuishi kwa mazoea Bali tunaishi kwa kujifunza.
kama mmetimiza vigezo vya utanzania, std 7, doc za serikali ya mtaa n.k basi endeleeni kufanya subra. haya maneno ya mtaani ni ya kukatisha tamaa. hebu endeleeni na mapambano kuliko kuzua uongo usiokuwepo.
wagala ni wehu sana. sasa hapo muujiza gani ikiwa mtu amefariki kifo cha kawaida akitokea kwenye matibabu India. hakuna muujiza hapo kwani kitu mtu anaonja kifo.
hapana si kweli wengine tumepita madrasa, tumehifadhi Quran na bado tuna GPA kubwa kutoka vyuo vinavyoheshimika duniani hivyo ni suala la mtu sio mfumo wa kiislamu.
Mimi ni muislamu ila kiukweli hatuko serious kwenye elimu. Mimi nimepeleka mwanangu wa miaka minne shule ya awali ya kiislamu hakuna utaratibu wa kueleweka wanavyo mchukulia mtoto wa nursery ni sawa na darasa la NNE. tusipobadilika tutabaki kulalamika daima.
Naomba ushauri kwa wataalamu mana jambo linanitia hofu sana. ni kwamba mke wangu amejifungua kwa operation miezi sita iliyopita sasa tumegundua amepata mimba nyingine wakati afya yake haijatengamaa. Kuna athari gani kwa mama na mtoto?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.