Ninaihitaji haraka nyumba ya kupanga ya vyumba 3 vya kulala, kimoja kati yao kiwe master, iwe katika manispaa ya Singida. Mwenye nyumba tafadhali wasiliana nami kwa 0752456024.
Ujuaji wa kila mtu ni muhimu sana ktk kuleta maendeleo. Ujuaji unasaidia kuidhibiti serikali na kuifanya iwajibike. Mataifa yaliyoendelea yameendelea kutokana na ujuaji wa watu wao. Watawala ovyo hukerwa na ujuaji wa wananchi, hufurahia umbumbu wa watawaliwa. Hekima ya watawala wetu huonekana tu...
Kilimo? Tatizo huku Songea ardhi imechoka sana, yatahitajika matumizi makubwa ya mbolea ambayo yataongeza gharama za uzalishaji na hivyo kunipunguzia faida, mkuu. Heshima bar? Tusile mtaji, mh.
Nina tsh 80m, niko Songea. Nianzishe mradi(miradi) gani ili niuage umasikini? Nisameheni kwa kukopa kabla ya kuwa na wazo kwanza. Ninatakiwa niwe nimezirudisha benki baada ya miaka 15 kuanzia sasa na 21%. wazo, tafadhali.
Kama inaliwa hadharani, wewe mwenyewe umechukua hatua gani? Maafisa wa pccb hawawezi kuwa kila mahali kwa wakati moja. Watajuaje bila kuambiwa? Watashindaje kesi bila ushahidi kutoka kwako? Angalau ungewakemea wala rushwa, wangeinama, wangeona aibu na kuacha kula rushwa. Wananchi wa kawaida tuwe...
Wabunge wa viti maalum wa nini? Wabunge wa majimbo wanawawakilisha wananchi wote walioko jimboni wakiwemo wanawake, walemavu, n.k. Viti maalum ni anasa, gharama isiyokuwa ya lazima. Wengi wa wabunge hawa huhudhuria tu, hawashiriki ktk vikao vya bunge. Mbele ya safari tupiganie kuipunguza idadi...
Maneno gani sasa hayo? Niache kupanga mambo yajayo kwa kuwa kuna kufa? Je nisipokufa? Ndio maana nchi hii haiendelei watu hawafikirii miaka 20 ijayo, wanawaza leo tu!
Mimi ni kijana wa kidato cha pili. Ninayamudu karibu masomo yote. Mwaka kesho nitalazimika kuyaacha masomo ya biashara au ya sayansi. Ninategemea kuhitimu chuo kikuu mwaka 2021, ninaomba ushauri kutoka kwa waona mbali, nifani gani itakuwa na soko mwaka 2021?
Ni kweli, kikwete ana mamlaka kikatiba kuteua wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya atakavyo, na inategemewa kuteua watu anaowafahamu.
Lakini hivi kweli Kikwete amekosa watu anaowafahamu na wenye uwezo zaidi ya hawa ambao ni wabunge tayari, au wana kitu gani cha pekee ambacho wengine hawana?
Kwa...
Mi naona tatizo liko kwenye jamii yetu. Jamii yetu ni ya waongo. Utamtoa wapi waziri mkweli? Ni mara ngapi watoto hudanganywa, "usilie, ninarudi sasa hivi", wakati mzazi akijua atarudi baada ya masaa mengi! Kwenye simu ni kawaida mtu akiwa bafuni akioga kumsikia akisema, "niko njiani nakaribia...
Niko Songea, nina 2.5m mkononi. Nifanye biashara gani ili nami baadaye niwe kama akina fulani? Wazo lako litanifanya nipate kisima cha pesa, nibaki nikichota tu. Tafadhali nishaurini wakuu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.