Hii inaonekana kama ni Nongwa au Husda au kutaka kuchafuana hivi.
Hao wakopaji walikopa kwa utaratibu naamini katika utaratibu huo kuna dhamana waliweka ili ikitokea wameshindwa kulipa "Defaulting" dhamana zao zikamate ziuzwe kufidia deni.
Au hizo benki ziliwakopesha bila dhamana, si washike...
Kunde
Division Zero na Ubalozi!
Waendelee kumpa ukuu wa mkoa tuu aendelee kubwabwaja kwa kiswahili!
Umewahi kuona wapi Bashite ameongea sentensi mbili zilizonyooka za kiingereza!
Huwa napenda sana hizi stori za utafutaji kimafia za madingi.
Nikimtazama Huyu mshua kwa hii picha mmeweka hapo, naona wazi mshua amekwenda ameshiba miaka na ana mvi zake. Kwa sura yake hii atakuwa kwenye late 60's or early 70's. . 😁
Pumzika Mzee ukute hata iyo pepo haipo ni kiini macho tuu. 😁
Dogo huwa anajivurugiaga mwenyewe japo ana ngekewa.
Waswahili wanasema hutakiwi kuongea sana wakati wa kula.
Waswahili wakaongeza kwamba unapomenya karanga za kipofu, usiongee piga mruzi huku unatafuna ili kipofu asijue unakula karanga zake, maana ukiacha kupiga mruzi atajua unakula karanga.
Acha huyo mzee, kuna mshikaji wangu amesomea "MIPANGO" ana degree ya Mipango na hela hana!
Sasa sijui kasoma mipango gani?
Huwa namuuliza hata yeye hana majibu.
Niliwahi pata Manzi mmoja! Dah yani yule Manzi kila muda anataka mnachati, stori, stori, WhatApp, Sms za kawaida muda wote.
Vikanishinda sijazoea hayo maisha. Na yeye akawa ananishangaa etii. 😁
Wife alitakaga kuanza kuimba kwaya!
Nikaweka karamu na karatasi tatu mezani nikamwambia nikikuona tena kwenye kwaya namwaga wino chap. Sijawahi msikia tena na habari za kuimba, naona alichagua ndoa akaacha kwaya. 😁
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.