Recent content by VUTA-NKUVUTE

  1. VUTA-NKUVUTE

    Kwa Sinema tulizozionesha CCM, No Reforms No Election haipingiki

    Mabadiliko kwenye mfumo wa chaguzi zetu hayapuuziki wala hayazuiliki. Pamoja na jeuri ya kichama na kidola, mabadiliko ni muhimu kama chumvi na ndimu kwenye supu adimu. Muhimu kama elimu ya kumkomboa mwanadamu kutoka zamadamu. No Reforms, No Election imepata uungwaji mkono na sinema za CCM. Ni...
  2. VUTA-NKUVUTE

    Tundu Lissu: Turufu pekee iliyobaki kwa Rais Samia

    Najua hamtaniamini. Najua mpo mtakaobisha vya kutosha na kutisha. Mtapaniki kuliko pikipiki ya kutumia kiki. Lakini, nawaambia jambo hili. Ni jambo geni na kubwa lakini muhimu na linalowezekana kwenye siasa za sasa. Siasa za sasa zinahitaji amshaamsha. Haifichiki tena kuwa mambo ndani ya CCM...
  3. VUTA-NKUVUTE

    Tundu Lissu si wa kupuuzwa, ni wa kusikilizwa kwa makini

    Nimeshindwa kuvumilia kutofuatilia na kushiriki siasa. Tangu miaka ya 80 nilipojiunga CCM baada ya kuhitimu masomo yangu pale Mlimani, nimejionea mengi. Nimewaona na kufanya kazi na wanasiasa waongo, wakweli, halisi na bandia. Wengi bado wapo, achilia mbali wale waliotangulia mbele ya haki...
  4. VUTA-NKUVUTE

    Why always Tundu Antiphas Mughwai Lissu?

    Mwaka 2010, Tundu Lissu aligombea kwa mara ya kwanza nafasi ya ubunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya CHADEMA akiwa na umri wa miaka 42. Mgombea wa Urais wa CHADEMA alikuwa Dr. Wilbrod Slaa na huku wa CCM akiwa ni Dr. Jakaya Mrisho Kikwete. Kwa kauli yake mwenyewe, tena akiwa anatetea urais...
  5. VUTA-NKUVUTE

    Jaribio la kumteka Deogratius Tarimo (Deo Bonge) huko Kiluvya, na Maswali tata

    https://www.youtube.com/watch?v=lnzeRYLOwJI
  6. VUTA-NKUVUTE

    PreGE2025 Kumekucha CCM: Nape na Makamba 'waula', walitumbuliwa ili kutambuliwa

    Haya ndiyo mambo ya kutumbuliwa ili kutambuliwa. Mawaziri wa zamani Nape Nnauye na January Makamba wamejumuishwa kwenye Kikosi Maalum cha CCM kinachoandaa Ilani ya CCM ya mwaka 2025 hadi 2030. Kikosi hicho kinaongozwa na komredi Stephen Wassira. Nyaraka za kichama zinaonesha kuwa Nape na...
  7. VUTA-NKUVUTE

    Rais Samia, kwanini unazipuuza Ripoti za Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora? Mnyeti na Makonda wanabaki vipi Serikalini?

    Tume hii ni Idara huru ya kiserikali iliyoanzishwa kwa mujibu wa Katiba (rejea Ibara ya 129 (1)). Ina wajibu wa kuhakikisha, pamoja na mambo mengine, haki za binaadamu na utawala bora vinatamalaki. Tume hii hupokea malalamiko; huyachunguza na kutoa ripoti zake. Katika siku za hivi karibuni...
  8. VUTA-NKUVUTE

    Nape hajatania wala kukosea, huo ndiyo ukweli wenyewe

    Ingekuwa kwenye nchi ya kidemokrasia na inayoiishi demokrasia, Waziri Nape Nnauye angeshapoteza uwaziri na ubunge wake muda huu. Angepoteza kwa shinikizo la wananchi au kuondolewa na Rais aliyemteuwa. Lakini hapa kwetu, Nape bado anadunda na anakejeli kwa kusema eti amechakachuliwa video yake ya...
  9. VUTA-NKUVUTE

    Spika Tulia tuambie, ushahidi wa Mbunge Mpina umeuonaje?

    Suala la Mpina halipuuziki. Sema nasi tusikie. Mbunge Luhaga J. Mpina alidai bungeni kuwa Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amelidanganya Bunge kuhusu sakata la uingizwaji wa sukari nchini. Alidai, pamoja na mambo mangine kuwa Bashe alisema uongo zaidi ya mara kumi. Kwa mujibu wa Mpina, Waziri...
  10. VUTA-NKUVUTE

    PreGE2025 LGE2024 Swali kwa Kinana, Je haki na uhuru wa uchaguzi huamriwa na Rais?

    Kichama na kiserikali namfahamu Komredi Kinana tangu miaka ya 80. Naujua uhodari wake kijeshi (kwakuwa nami nilitumikia mojawapo ya vyombo vya ulinzi na usalama), kiserikali na kichama. Komredi Kinana si mtu wa maneno mengi. Ni mtu wa mipango ya viwango na vitendo na mwendo. Sikushangaa pale...
  11. VUTA-NKUVUTE

    'Magari ya Makonda' yakwama kukarabatiwa, mwenyewe agoma kutoa ushirikiano

    Unakaribia mwezi mmoja sasa tangu msafara Ndugu Paul Makonda, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, upate ajali kule Sululu, Masasi mkoani Mtwara. Ajali hiyo iliyohusisha magari yapatayo 10, ilitokea tarehe 11 mwezi uliopita na kusababisha uharibifu wa magari kadhaa yakiwamo ya...
  12. VUTA-NKUVUTE

    Nani anatoa 'kitita' cha kuwahamisha Wamasai kutoka Ngorongoro? Tunapata faida gani kama Taifa?

    Nipo hapa Arusha. Jana nami niliyashuhudia (lakini sikushiriki) maandamano ya amani ya CHADEMA katika viunga vya jiji la Arusha. Sikwami wala kuogopa kusema kuwa yalikuwa ni maandamano makubwa; washiriki walikuwa wamejipanga kila anga na yalipeperusha hoja za haja. Kabla ya jana, nilioneshwa...
  13. VUTA-NKUVUTE

    Ushauri kwa viongozi wangu wa chama na Serikali kuhusu ahadi za umeme

    Sasa ni dhahiri kuwa suala la umeme linakitweza na kukiaibisha chama tawala-CCM. Pia, umeme unaitweza na kuiaibisha Serikali iliyopo madarakani. Umeme unakatikakatika. Umeme haueleweki. Umeme hauaminiki. Umeme hauzoeleki. Umeme unagawiwa. Unaleta athari kubwa kwa wananchi na kwa nchi. Mimi...
  14. VUTA-NKUVUTE

    Mwanangu Makonda, umeichoka na kuikinai nafasi yako chamani?

    Jana nilikusikia na kukusikitikia sana. Jinsi unavyojikaanga kwa mafuta yako mwenyewe. Jinsi unavyoonesha kuchoka na kukinai nafasi uliyonayo kwasasa chamani. Pale ulipozungumzia kuhusu mdahalo na viongozi wa CHADEMA. Ngoja nikusaidie kwakuwa nilikuwa kiongozi mwandamizi chamani kabla yako...
  15. VUTA-NKUVUTE

    Chongolo uwe na amani, uchunguzi utafanyika na utatendewa haki. Chama kitaonesha ukubwa wake

    Kwanza, tunamshukuru Mungu kwa kuzuia hujuma zisizo na huruma kwa CCM yetu baada ya kuepusha kupokwa kwa nafasi ya Katibu Mkuu jana. Shukrani zetu, kama makada waandamizi na wazee wa chama, ni kwa Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa Mama Samia S. Hassan kwa kutusikiliza tulipomshauri cha kufanya...
Back
Top Bottom