Mpaka sasa upande wenye kupinga uwepo wa laana wameweza kujibu kwanini wakati mwengine watu hutokewa na madhara baada ya kutolewa laana, wamesema huwa ni hofu yake tu(nocebol effect) ndio yenye kusababisha kujiletea hayo madhara lakini si laana ndio maana wengine hawapatwi na madhara yeyote hata...
Nadhani hiyo ni nocebo effect badala ya placebo.
Kwahiyo hapo kwa nilivyokuelewa ni kwamba kinachomfanya mtu apate madhara kama matokeo ya laana ni hofu yake inakuwa nocebo effect ila kwa asiyekuwa na hofu hawezi kuathiriwa na chochote?
Ulichoeleza ni sahihi kwa maana ndio inapaswa iwe hivyo na ndio maana mimi nauliza ni chanzo kipi cha nguvu ambacho ndio kinaleta athari kwa aliyelaaniwa? Lakini kwenye uhalisia wa maisha yetu ya kiafrika kuna baadhi ya matukio ambayo ni kama yanaeleza kitu tofauti na ulichoeleza.
Na ndio maana nasema hata kwenye jambo lenye sura ya uongo kunawezekana kuwa kuna chembe ya ukweli na hata kwenye jambo lenye sura ya ukweli kunaweza kuwa na chembe za uongo, shida kila mmoja anapotaka kushika upande wake uwe ndio sahihi kwa 100%, hali inayotufanya tushindwe kuchunguza uhalisia...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.