Omba Mungu umsahau kabisa maana kinachoendelea sasa pamoja na huyo jamaa kufutwa ila bado hamjamsahau na hiyo inakuwa kama mtu aliyefiwa na mpenzi wake aliyekuwa akimpenda sana.
Na mimi najua iko hivyo kama hapo wewe una experience yako kuhusu waganga ila wao kwao ni tofauti, mtu hana experience yeyote na kitu anachokipinga ndio maana ni tabu kubishana na watu kama hao.
Nimesema kwamba kuna magonjwa yanajulikana hayana dawa ila kwenye mitishamba hayo magonjwa hutibika, kinachofanya iendelee kusemwa hakuna dawa za hayo magonjwa ni kutokuwepo uthibitisho wa kisayansi kwa hiyo mitishamba kutibu hayo magonjwa ndio maana inabaki kutambulika hakuna dawa za hayo...
Hili suala la uthibitisho ni tata maana mfano unakuta inajulikana hakuna dawa ya ugonjwa fulani lakini kuna watu huko wanatumia mitishamba yao kutibu ugonjwa huo huo ila kwa kuwa hakuna uthibitisho wa kisayansi kwa dawa hiyo basi inaendelea kubaki kuwa huo ugonjwa hauna dawa.
Kwa maana kwamba mtu unaweza kwenda kwa mganga kwa kutaka kumroga mtu afe na akafa kweli au awe chizi awe chizi na kweli akawa chizi huwa ni mind game tu hatujajua?
Lakini navyojua wakati mwengine mganga anaweza kukutajia dawa ya tatizo ukaitafuta mwenyewe na ukajitibu tatizo lako pasina kutibiwa na mganga, je hapo source ya nguvu ya hiyo dawa inatoka wapi?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.