Kinachowavutia waumini kwenye hayo makanisa ni miujiza na si mahubiri na ndio maana siku hizi hadi waislamu wanaenda huko makanisani, yote ni kwa sababu ya kufuata hiyo miujiza na si mahubiri.
Inategemea na eneo unaloishi ndio maana nasema kwa hapa Tanzania wakristo wengi huonekana kupenda miujiza ila ukienda nchi zengine utakuta wakristo wa huko hawana time na mambo ya miujiza.
Unazungumzia nchi gani au jamii gani? Kwa sababu anaweza akaja mwengine akasema kuna dini fulani wanapenda sana miujiza, lakini kumbe huyo mtu akienda nchi zengine huko anakuta waumini wa huko hawana time na mambo ya miujiza wao wako busy na kazi na wanaamini sana sayansi kuliko mambo ya miujiza.
Hiyo hard work unayoizungumzia tunaionaje kwenye bara letu hili la afrika ambalo ni masikini na lipo nyuma kimaendeleo na hizi dini zikihusishwa kuwa ni moja ya chanzo chenye kuchangia watu kutotumia sana akili na kufanya kazi kwa bidii badala yake wanategemea sana maombi na miujiza?mifano...
Pamoja na kueleza hayo yote ila bado inaonekana kijumla dini zinawafanya waafrika kutegemea maombi na miujiza zaidi kuliko kazi, je hili unalizungumziaje?
Hapana mkuu wala sio suala la kuzini wala dhambi na kama hiyo ingekuwa ndio sababu basi hata hizo ndoto usingepata kabisa, ndoto kuwa katika mafumbo ni kawaida. Sema changamoto ndio hiyo kwa ndoto zenye kuonyesha matukio yajayo inakuwa ngumu kidogo kuweza kujua maana ya ujumbe wa hiyo ndoto hadi...
Kwa sasa ndoto unaletewa kwa mafumbo ni tofauti na ulivyokuwa mdogo, hapo ukiweza kufuatilia hizo symbols katika ndoto zako na ukazielewa tafsiri zake kwako basi itakuwa rahisi kwako kuweza kufahamu maana ya ujumbe uliyo katika hizo ndoto zako.
Tunapokuwa tunaanza kufikiri kwa kutumia mantiki zaidi na ndivyo jamii inavyotaka ndio maana hata hapa utaona watu jinsi wanavyopokea hayo mnayoeleza humu kwa kuona kama ni kuchanganiyikiwa tu, hivyo unapokuwa unakutana na ukosoaji na unajikuta pia unajenga hali ya kujitilia mashaka mwenyewe...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.