Waheshimiwa Wabunge wetu. Nimemsikiliza Spika Ndugai akiweka msimamo wake kuhusu hatua yenu ya kuondoka Bungeni kwa muda.
Spika Ndugai anastahili kujibiwa rasmi na hadharani, na napendekeza yafuatayo kuwa sehemu ya majibu yenu.
1. Je, Wabunge wa CHADEMA ni watoro?
Kwa kadri ninavyofuatilia...
For the Record: What Goes Around Comes Around!!!
Leo wapinzani wa Serikali ya Magufuli tumesemwa sana na kutishiwa kushughulikiwa bungeni na nje ya Bunge.
Kwa sababu hiyo, naomba niweke rekodi ya masuala haya sawa sawa.
Mwezi Machi '97 Bunge lilipitisha Sheria 2 kwa siku moja kwa kutumia Hati...
Hiyo habari ya kujiunga na chama akiwa na miaka 16 ina maana alijiunga mwaka '92, mwaka wa kuanzishwa kwa CHADEMA. Hata hivyo, madai hayo hayajawahi kuthibitishwa zaidi ya kurudiwa rudiwa Mara nyingi. Kwa taarifa nilizozisikia kwenye Kongamano la BAVICHA siku ya Jumapili, MM ni miongoni...
Kwa wanaomwamini Mwanasheria Mkuu, Lukuvi na maCCM wengine. Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Katiba, Sheria na utawala, na nilihudhuria vikao vyote vya Kamati wakati wadau wanatoa maoni yao mbele ya Kamati. In fact, niliondoka kwenda kwenye mikutano ya rasimu ya Katiba baada ya Kamati kukamilisha...
Kwa Wanaotaka kujua ukweli wa utetezi wangu wa Wazanzibari, nilianza kuwatetea tangu siku ya kwanza ya kikao cha Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala cha tarehe 29 Julai ilipokutana kwa ajili ya kujadili Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na Muswada wa Sheria ya Kura ya Maoni. Siku hiyo...
Wanajamii,
Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Singida imewaachilia huru Dr. Kitilla Mkumbo na Mwita Mwikwabe Waitara baada ya kuona kwamba upande wa mashtaka haukuthibitisha makosa yoyote dhidi yao kwa kiwango kinachotakiwa na sheria. Itakumbukwa kwamba Dr. Mkumbo na Waitara walishtakiwa kwa madai...
Naomba kuingilia kati mjadala huu kwa sababu naona, kwa kiasi fulani, unanihusu. Na nataka niweke maelezo ya upande wangu ili angalau kumbu kumbu ziwe sawa. Mwanzoni mwa mwaka jana nikiwa Mwanza kwa ajili ya kesi ya uchaguzi yabMbunge wa Ilemela, Mh. Highness Kiwia, Nilialikwa na jumuiya ya...
Hivi tunavyoandika humu ndani Wilfred Lwakatare yuko mahabusu ya Segerea kwa sababu amenyimwa dhamana kwa makosa ya kutunga ya ugaidi aliyoshtakiwa nayo. Na kwa wasiomfahamu, basi niseme kwamba hali yake ya kiafya sio nzuri kwa sababu anasumbuliwa sana na ugonjwa wa kisukari. Kwa mazingira aliyo...
Kwa kawaida huwa sijaribu kuchangia hoja anazoanzisha Mwigulu Nchemba kwa sababu namchukulia kama kipimo cha muflis wa kisiasa wa maCCM. Hata hivyo naomba nivunje jadi yangu hiyo kwenye jambo hili, sio kwa lengo la kujitetea au kuitetea CHADEMA bali kwa lengo la kusaidia watu wengine kumwelewa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.