Kwa nini Lissu alidanganya bunge?

Kwa nini Lissu alidanganya bunge?

Kwani kanuni za Bunge si ziko wazi kwa MP anayesema uongo bungeni?? Sasa kwanini hizo kanuni. hazikutumika kwa Mh Lissu hadi wewe mtoa thread utake kutuaminisha kua Tundu Lissu alisema uongo???Bunge limuadhibu kama alisema uongo.....na sio kuja hapa tu na verbal diarrhoea.
 
Dr Kigwangwala anakazi ya ziada na mgonjwa wake bado hajapata nafuu

Nilisikitika sana kuona kigwangala anatumia muda wake wote aliopewa kuchangia kuhusu marekebisho ya sheria ya katiba yeye akautumia muda wote kumjadili na kumdhihaki mbowe huku akiingilia hadi mambo yake binafsi (mambo ya kifamilia) na naibu spika wala hakuona haja ya kumrudisha kwenye mada (bora angekuwepo mama makinda), hadi wabunge wenzake wenye busara zao wakaanza kusema 'basi inatosha'. kwa kweli alijidhalilisha sana na kujitoa dhamani, Mi nadhani yeye ndio bado hajapona
 
EZEKIEL MAIGE; Mbunge wa Msalala CCM, NAIBU Spika,Hakuwa sahihi kutomsikiliza Mbowe!
Baada ya Jauzi jana na leo kuendelea kwa malumbano bungeni kati ya Naibu Spika,wabunge wa CCM kwa upande mmoja na Wabunge wa upinzani kwa upande wa pili wakiongozwa na CDM,wadau mbalimbali wamekuwa wakitoa maoni yao juu ya kile kilichojiri jana wakati wa kikao cha bunge la Mchana baada ya Naibu Spika kutumia Askari wa bunge kumtoa nje KUB,hali iliyopelekea tafrani kubwa sana.

Akitoa maoni yake ktk ukurasa wa Facebook,Mh Ezekiel Maige mbunge wa Msalala alisema kuwa hakuona sababu kabisa ya kufikia hapo kwani hali hiyo ingewezwa kuepushwa.

Ingewezekana kabisa kuahirishwa kwa muswada huo na kutoa nafasi kwa kamati ya katiba na sheria kwenda Zanzibar kupata maoni ya wenzetu huko.

Najuwa kuna maelezo mazuri ya kushirikishwa kwa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,lakini Kikanuni baada ya muswada huo kusomwa kwa mara ya kwanza unakuwa mikononi mwa Bunge.Kamati ndio inayokusanya maoni na sio serikali.

Kwa kuwa hakuna ushahidi wa Public hearing iliyofanyika Zanzibar na kuwasikia Wazanzibari wa kawaida(nje ya serikali) basi kulikuwa na haja kabisa ya kurekebisha kasoro hiyo kwa kutoa nafasi kwa kamati kwenda Zanzibar!!

Swala la katiba ni swala kubwa hivyo ni vema zikafanyika jitihada za kutosha kuhakikisha tunakwenda pamoja(na wenzetu haswa wenye mtazamo tofauti na sisi CCM) badala ya kutumia "Wingi wetu" kwani mwisho wa safari tukienda hivi watakuwepo watakaodai kuwa katiba mpya sio yao na hivyo kuikosesha "Social legitimacy"!!

Kwa kiti (Naibu Spika) kutomsikiliza Mh Mbowe (KUB) nako kulitibua mambo bila sababu ya msingi.
Angepewa nafasi ya kusikilizwa hata kama hoja yake isingekubaliwa bado ingekuwa nafuu sana kuliko shari na aibu ya jana iliyotokea.

Tumesameheana lakini tujifunze na tujitahidi sana kwenda kwa maelewano.

Mungu ibariki Tanzania. By Ezekiel Maige mbunge wa Msalala kupitia CCM.

Ndivyo alivyoandika mh Ezekiel. Binafsi nimependa sana mada yake hii japo siamini kuwa km angekuwepo juzi na jana bungeni nae angeto maoni haya kwa chama chake.!! Nawasilisha.


Angepewa nafasi ya kusikilizwa hata kama
hoja yake isingekubaliwa bado ingekuwa
nafuu sana kuliko shari na aibu ya jana
iliyotokea.

Kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni si sababu ya kujiamulia kila ambacho unadhani ni sawa kwako,mbowe alikuwa na haki ya kusikilizwa tatizo hakufata utaratibu wa bunge,ni dharau aliyoonyesha kwa mheshimiwa mrema ambaye alipewa fursa ya kuchangia hoja halafu mbowe kwa kujiona yeye ndie bora na bunge tukufu lipo chini yake akajiamulia kumuinterupt mrema,siungi mkono maamuzi ya naibu spika ila mbowe nae ajue alichofanya kilikuwa ni nje ya utaratibu wa bunge,WHAT He GOT IS WHAT He DESERVED
 
pamoja na yote uliyoandika, lakini kwa hili CHADEMA na LISSU wameaibika. maelezo yametolewa vizuri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na yamejitosheleza. pia serikali ya mapinduzi Zanzibar ambayo ni ya ubia baina ya CUF na CCM imekiri kuwa imeshirikishwa na walitoa mchango wao. Ni aibu kwa chama cha upinzani kuumbuliwa hadharani

Kwa wanaomwamini Mwanasheria Mkuu, Lukuvi na maCCM wengine. Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Katiba, Sheria na utawala, na nilihudhuria vikao vyote vya Kamati wakati wadau wanatoa maoni yao mbele ya Kamati. In fact, niliondoka kwenda kwenye mikutano ya rasimu ya Katiba baada ya Kamati kukamilisha kazi ya kupokea maoni ya wadau na pia kuridhika kwamba Safari ya Zanzibar ilikuwa haiwezekani tena.

Kwa kifupi, Kamati ilitengeneza orodha ya wadau wa Zanzibar ambao tulitaka kuonana nao. Wadau hao ni hawa wafuatao:
1) Zanzibar Law Society
2) Zanzibar Female Lawyers Association
3) State University of Zanzibar
4) University of Zanzibar Tunguu
5) Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA)
6) Umoja wa Walemavu Zanzibar
7) Profesa Abdul Sheriff
8) Association of NGOs in Zanzibar (ANGOZA)

Ratiba ya Kamati ilikuwa inaonyesha kwamba Kamati ingeonana na wadau hawa Zanzibar Kati ya tarehe 14-16 Agosti. Kamati ilizuiliwa kwenda Zanzibar na kwa hiyo hakuna mdau hata mmoja wa Zanzibar aliyeonana na Kamati.

Mwanasheria Mkuu Werema amedai kwamba chama cha Jahazi Asilia walikuja kutoa maoni yao kwenye Kamati. Swali ni je, chama cha jahazi asilia ni chama cha Wazanzibari peke yao? Kwa kadri ninavyojua, Jahazi Asilia ni chama kilichosajiliwa Dar es Salaam sawa na CUF, CCM, CHADEMA, n.k. Hakuna chama cha siasa cha upande mmoja wa Muungano kwa maana ya kisheria. Vyama vyote vinatakiwa na Sheria ya Vyama Siasa kuwa vya Muungano. Notebook yangu ya kikao cha Kamati cha tarehe 30 Julai inaonyesha kwamba vyama vyote vya siasa, Jahazi Asilia included, vilitoa maoni siku hiyo. Hakuna hata kimoja kilichokuja kwa niaba ya Wazanzibari.

Kuhusu Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kushirikishwa kwenye maandalizi ya Muswada, hiyo vile vile ni ngonjera ya maCCM. Sisi kama Kamati hatukukutana na mwakilishi yeyote wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kipindi chote cha Muswada kuwa kwenye Kamati. Ukweli ni kwamba hata SMZ hawakushirikishwa mpaka Jumatatu ya wiki walipom-summon AG na Lukuvi Zanzibar baada ya Kamati kuhojinushirikishwaji wa Zanzibar katika Miswada yote miwili. Ndio maana ilibidi Muswada wa Sheria ya kura ya maoni uondolewe kwenye orodha ya shughuli za Bunge za wiki hii kwa sababu SMZ iliwaambia haiko tayari kutoa ridhaa yake. Huyo Mzee Iddi Sefu ametumiwa kuokoa jahazi la CCM Bungeni. Tutafahamu vizuri juu ya ukweli wa jambo hili very soon.

In fine, mimi sikudanganya chochote Bungeni. Ndio maana hao wanaodai nimedanganya hakuna hata mmoja aliyethubutu kuniambia nithibitishe kauli yangu vinginevyo niifute Kama inavyotakiwa na kanuni za Bunge. Na Kama nilikuwa nimekosa kweli, mimi ni Mtu wa kusamehewa na watu hawa kirahisi hivyo? Si ningefukuzwa Bungeni Kama Zitto mwaka fulani kwa jinsi walivyo na hasira na mimi?

All the best,

Tundu
 
pamoja na yote uliyoandika, lakini kwa hili CHADEMA na LISSU wameaibika. maelezo yametolewa vizuri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na yamejitosheleza. pia serikali ya mapinduzi Zanzibar ambayo ni ya ubia baina ya CUF na CCM imekiri kuwa imeshirikishwa na walitoa mchango wao. Ni aibu kwa chama cha upinzani kuumbuliwa hadharani
barua iliyoletwa bungeni ya makamu wa pili wa raisi ambaye ni ccm wabunge wake hawakutoka nje......lakini makamu wa kwanza hakuleta barua pale wabunge wake walitoka nje...vile vile barua haithibishi kushirikishwa kwa wadau alitakiwa ataje tu siku fulani ....tarehe fulani.....tulikutana na huhuyu na yule full stop....
 
Nadhali VILAZA WA CCM mmejibiwa vyema na Kamanda anayeogopeka kama Njaa Tundu Lisu. Asante sana Kamanda wangu. Natambua jinsi CCM walivyojitahidi kuwa rubuni wajumbe wa mabaraza kuimba Kiitikio "Kwasababu 2napendekeza serikali mbili" na kuumbuliwa na Mzee Butiku na Mama Kibibi.
 
Hivi lile fail la lissu pale mirembe lipo wodi gani vile?
 
barua iliyoletwa bungeni ya makamu wa pili wa raisi ambaye ni ccm wabunge wake hawakutoka nje......lakini makamu wa kwanza hakuleta barua pale wabunge wake walitoka nje...vile vile barua haithibishi kushirikishwa kwa wadau alitakiwa ataje tu siku fulani ....tarehe fulani.....tulikutana na huhuyu na yule full stop....

porojo tupu. Na alivyosema mtei kuwa wajumbe wa tume kutoka znz ni wengi huku akionyesha ubaguzi wa kidini ulikuwa wapi ww? Waliberali new union mna tabu sana
 
maelezo ya kihuni kabisa haya. Kumbe uliondoka wakati wana kamati wanaenda znz, sasa imekula kwako, mchakato utaendelea kama kawaida. Ndoa yenu mpya ya kiliberali mliyofunga juzi dodoma haina baraka hata kdg. Mwanasheria ametoa maelezo ya kutosha na zaidi pindi chana amekuchana chana vyema kwa hiyo povu unalotoa hapa machadema wenzio ndio watakaodanganyika


ifweero

Tuwekee hapa ushahidi kama mrejesho kwamba kamati ilikutana na walengwa hawa hapa chini na walipendekeza nini?

1) Zanzibar Law Society
2) Zanzibar Female Lawyers Association
3) State University of Zanzibar
4) University of Zanzibar Tunguu
5) Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA)
6) Umoja wa Walemavu Zanzibar
7) Profesa Abdul Sheriff
8) Association of NGOs in Zanzibar (ANGOZA)

Ratiba ya Kamati ilikuwa inaonyesha kwamba Kamati ingeonana na wadau hawa Zanzibar Kati ya tarehe 14-16 Agosti. Kamati ilizuiliwa kwenda Zanzibar na kwa hiyo hakuna mdau hata mmoja wa Zanzibar aliyeonana na Kamati.
 
porojo tupu. Na alivyosema mtei kuwa wajumbe wa tume kutoka znz ni wengi huku akionyesha ubaguzi wa kidini ulikuwa wapi ww? Waliberali new union mna tabu sana


Ok ifweero, wewe usifanye porojo waache hao wenye porojo lete majibu basi mkuu.

kutukana peke yake hakuleti maana sahihi ya mjadala, jenga hoja tutakuelewa.

Hebu tusaidie kwamtazamo wako walau majibu kwa kinachonitatiza.


a) Unauhakikagani kwamba data na maelezo ya ccm na pindi chana siyo ya
kupindapinda na kuwahadaa watanzania?

b) Nani amethibitisha kwamba kati ya CCM, Pindi Chana na Lukuvi sio
waongo? Ifweero umefanya utafiti wowote? thibitisha....

Marangapi CCM na
dola yake imewahaada watanzania kupitia viongozi wake
wa juu? mfano:-

1. Pinda Kulidanya bunge na watanzania kuhusu mgogoro wa vurugu za
Arusha Polisi na chadema.....

2. Kikwete maisha bora kwa kila mtanzania ....... yamekuwa maisha duni
kwelikweli kwa kila mtanzania...

3. Chagonja mwangosi ameuwawa na wafuasi wa chadema, picha zikamuumbuwa,
hakujuwa kama kuna picha za wauwaji....

4. Kikwete, Lowasa na basili mramba ni majembe......Kama ni majembe
mbona kavuliwa uwaziri mkuu na maramba anakesi ya uhujumu uchumi????
 
hakika kamanda Tundu Lissu umemaliza kila kitu na ni wazi jahazi hasilia wameokoa jahazi la maccm.

Ni wazi lazima mtu yeyote ashangae kukusamehe kama kweli ilikuwa ni uongo.
 
kama kweli Lissu amelidanganya bunge mbona hatuona akidhibiwa au kuambiwa afute kauli yake? kuna kitu kimejificha hapa. na kama wazanzibari wanasema wameshirikishwa sawa ila wasije kukimbiana huko mbeleni. ninaamini lissu hajakurupuka ila waliosiliza wanonekana kukurupuka.
 
Baada ya kusoma ufafanuzi wa Lissu wala sikusoma michango mingine, malezo ya Lissu yapo straight na yamejikidhi, hongera kamanda Lissu!
 
Hivi lile fail la lissu pale mirembe lipo wodi gani vile?

Wewe kweli jembe na "great thinker" yaani "unamchana" TL mchana kweupe. Endelea hivi utafika mbali. Lakini utafanya vizuri zaidi kama utacrush hoja za TL kwa point. Jaribu tena.
 
porojo tupu. Na alivyosema mtei kuwa wajumbe wa tume kutoka znz ni wengi huku akionyesha ubaguzi wa kidini ulikuwa wapi ww? Waliberali new union mna tabu sana
sasa wajumbe wa baraza la katiba na mswaada wa katiba wap na wapi
 
Back
Top Bottom