Recent content by Stanley Mengsen

  1. S

    Mkurugenzi PSSSF afikishwa mbele ya Baraza la Maadili

    Mheshimiwa Waziri wa Afya, Ummi Mwalimu, Napenda kukusalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Naamini kwamba bado uamuzi haujafikiwa kuhusu "Universal Health Insurance Fund" ambayo itajumuisha watanzania wote. Nafahamu pia kuwa yapo mapendekezo ya kuanzisha "regulator" wa huduma za...
  2. S

    Dkt. Tulia Ackson, Mawaziri wa CCM hawana majibu usiwabane sana

    Mheshimiwa Spika, Naomba niseme kweli bila kupapasa macho kuhusu yanayokupata Bungeni sasa hasa kuhusu Waziri wa Fedha na Uchumi. Kwanza, ni wazi kabisa kwa ujumla wabunge ulionao Bungeni baadhi yao ni weledi sana (akiwemo Mpina). Na kwa bahati mbaya sana unao pia wabunge na mawaziri...
  3. S

    Kamati Kuu ya CHADEMA yawavua nyadhifa na uanachama Halima Mdee na wenzake 18 walioapishwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum

    Kwanza, napenda kumpongeza Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Freeman Aikael Mbowe kwa uamuzi madhubuti na sahihi kwa kuwafukuza uanachama kundi lote la Covid 19. Adhabu uliowapa inaonyesha wazi kuwa usaliti wao ni hatari kwa CHADEMA. Pili, niseme kuwa nadhani adhabu hiyo haitoshi kwa sababu upo uwezekano...
  4. S

    Barua ya wazi kwa dada Halima Mdee

    Nadhani Wakuu hapa jambo la kuangalia sio kupeleka majina tu huko Bungeni, bali kuangalia CHEDEMA wakipeleka majina Bungeni maana yake ni nini? CHADEMA wakipeleka majina kwa ajili ya viti maalum ni sawa na kahalalisha udhalimu wote uliofanywa wakati wa uchaguzi mkuu uliopita. Halima Mdee ni...
  5. S

    GE2020 Kuna mgombea amekuwa akipotosha kuwa tukichagua upinzani kutatokea vita. Anatakiwa kuitwa kwenye Kamati ya Maadili

    Kuna mgombea amekuwa akipotosha kuwa tukichagua mpinzani kutatokea vurugu na vita, tena amekuwa akiienda mbali kwa kusema "uongozi haujaribiwi". Naomba tume NEC imuite akajieleze kuhusu upotoshaji wake. Pamoja na hilo pia ametoa hongo ya barabara kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za uchaguzi...
  6. S

    GE2020 Lissu anaongelea tu Serikali za Majimbo kujiamulia mambo ila haelezi gharama za uendeshaji zitatoka wapi

    Gharama za uendeshaji wa serikali za majimbo utakuwa ni sawa kabisa na kama inavyoendeshwa hivi sasa na serikali kuu. Na vyema ikaeleweka ya kuwa, kwa uwepo wa serikali za majimbo, itakuwa si kwamba fedha zote zipatikanazo kutoka katika jimbo husika zitatumika zote hapi hapo tu. La hasha! Kwa...
  7. S

    Faida za kiuchumi za Uwanja wa Ndege Chato

    Watanzania wote wanajua kwamba ujenzi wa Uwanja wa ndege wa Chato ni ubinafsi uliokithiri wa kiongozi Magufuli. Hakuna sababu kwa nini kiwanja cha Mwanza hakikujengwa kwanza. Kwa kigezo cha uchumi Mwanza inaongoza, Kwa kigezo cha Madini Mwanza inaongoza, Kwa kigezo cha utalii Mwanza inaongoza...
  8. S

    Prof Kabudi: Tanzania tuliipigia kura Kenya Baraza la Usalama UN. Wametushukuru, nasi tumewaambia hapana ule ni wajibu wetu kama ndugu!

    P Prof Kabudi, hili sio suala la kuzungumza bila ushahidi. Ushahidi wa kwamba tuliwapigia Djibuti upo hapa chini. Ni vyema kusema ukweli kwani hat a majirani zetu watakuheshimu zaidi.
  9. S

    Serikali imenyoosha mikono dhidi ya watoa huduma za TV!

    Ukweli ni kwamba TCRA ni wala rushwa wa hali ya juu, kwa sababu kama sheria wanayoitumia haifai basi wangefuata utaratibu wa kupendekeza mabadiliko ili itungwe sheria mpya inafaa. Ukiangalia sababu TCRA wanazotoa kwa kutoweza kuitekeleza sheria iliyopo hazina msingi wowote. Hii ni changamoto kwa...
  10. S

    Medard Kalemani alikuwa Mkurugenzi wa sheria Wizara ya Madini, Mikataba ilipita kwake, anaponaje?

    Wakuu, Niliwahi kujiuliza maswali mengi kuhusu Medard Kalemani-Mbunge wa jimbo la Chato na Naibu, Waziri nishati na Madini. Dr. Medard Kalemani kabla ya nafasi aliyonayo hivi sasa, alikuwa mwanasheria mkuu katika hiyo hiyo ya Nishati na Madini. Hii ina maana kwamba wakati wizara hiyo ikiongozwa...
  11. S

    Hakika Tundu Lissu amewachoma sindano ikagusa mshipa

    Wakuu, Tundu Lissu ni mpinzani, na wajibu wa wapinzani katika siasa ni kuikosoa serikali iliyoko madarakani. Alichofanya ni kufichua kilichokuwa kimefichwa na serikali kuhusu kuchelewa kwa ndege iliyonunuliwa kwa pesa za walipa kodi. Sasa msemaji wa serikali anamshutumu Tindu Lissu kwa kutokuwa...
  12. S

    TRA kuwataka wafanyabiashara kurudisha mashine za EFD na kununua mpya ni kuwaua kibiashara

    Wakuu, Watanzania wengi hawakuzoea kulipa kodi. Hii inatokana na sababu nyingi. Mojawapo ya sababu hizo ni kwamba kwa muda mwingi imekuwa vigumu wananchi kuridhika na matumizi ya fedha zinazotokana na hizo kodi. Sababu nyingine ni kutokuwa na uelewa mzuri wa jinsi kila mmoja anavyowajibika...
  13. S

    Maoni: Rais Magufuli ahutubie kama Rais

    Wakuu, Inawezekana kabisa Raisi wetu bado hajiamini kuwa yeye ni Raisi na ni mkuu wa majeshi yote ya ulinzi na usalama. Hii inajidhihirisha jinsi anavyotoa hotuba zake kila sehemu anazokwenda. Ukisikiliza hotuba zote alizotoa huko mikoani ni vigumu kupata ujumbe wowote aliotaka wananchi...
  14. S

    Kampuni ya Reli Tanzania(TRL) yavikana vichwa vya Treni, yataka virudishwe vilipotoka

    Wakuu, salam kwenu. Hili suala la vichwa vya treni vilivyoshushwa bandarini na kuambiwa hatujui mwenyewe ni jambo la aibu na fedhea sana kwa nchi inayojitawala kama Tanzania. Haingii akilini kwamba vichwa vya treni 11 vinashushwa na hatujui ni vya nani. Pamoja na vyombo vyote vya dola...
  15. S

    Mauaji yanayoendelea Kibiti, Pwani: Maoni, Ushauri na Mapendekezo ya nini kifanyike ili kuyatokomeza

    Ukiangalia yote yaliyotokea na yanayoendelea kutokea huko mkoa wa pwani kuhusu mauaji ya askari, viongozi wa CCM na wananchi wengine, ni dhahiri kuwa wanaofanya mauaji hayo ni watu wenye mafunzo ya kijeshi. Hii inajionesha jinsi wanavyowaua wenzetu hawa. Mimi kwa haraka haraka naamini wanaofanya...
Back
Top Bottom