Faida za kiuchumi za Uwanja wa Ndege Chato

Ngamanya Kitangalala

JF-Expert Member
Sep 24, 2012
501
1,214
Tangu kuanza kwa mchakato wa kampeni za uchaguzi mkuu wa October mwaka huu, nimepata bahati ya kufuatilia kampeni za baadhi ya wagombea wetu wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Kwa bahati mbaya kwenye baadhi ya mikutano ya kampeni ya baadhi ya wagombea, Kumekuwepo upotoshwaji mkubwa kuhusu ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa katika mkoa wa Geita, unaoendelea kujengwa katika wilaya ya Chato.

Binafsi naamini sisi kama watanzania tunawajibu mkubwa wa kupima na kutafakari kwa umakini mkubwa tuhuma mbalimbali zitolewazo na baadhi ya wagombea dhidi ya wagombea wengine katika mikutano mbalimbali ya kampeni inayoendelea kwenye maeneo kadhaa hapa nchini.

Nadhani ipo haja ya sisi Watanzania, kuelewa umuhimu na faida za kiuchumi ( Economics Benefits) kwa uwanja wa ndege wa kimataifa Chato.

Kwanini uwanja wa ndege Chato?
Ukisoma ilani ya uchaguzi ya CCM mwaka 2015- 2020 , ilieleza umuhimu wa serikali kuchukua hatua za makusudi katika kukuza na kuendeleza sekta ya utalii nchini,ili ifikapo mwaka 2020, Tanzania iwe na uwezo wa kupokea watalii wasiopungua 2,000,000 kwa mwaka toka watalii 1,200,000 ilivyokuwa mwaka 2014,hasa ukizingatia kuwa kwa mujibu wa ripoti ya World Economic Forum ( WEF) iliyotolewa mwala 2014,ilionyesha Tanzania ni nchi ya pili duniani kwa kuwa na vivutio vingi vya asili vya utalii baada ya Brazil.

Japokuwa kwenye ripoti nyingine ya 2019 kutoka World Economic forum ambayo utolewa kila baada ya miaka 5, imeonyesha Tanzania inashika nafasi ya 12 duniani na ya 1 kwa Afrika kwa kuwa na vivutio vingi vya asili vya utalii(Tumeshuka kwa nafasi 10)

Lakini pia ukisoma ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi ya 2020-2025, latika ukurasa wa 111, imeeleza lengo la serikali la kutaka kukuza sekta ya utalii, na kufikia kupokea watalii 5,000,000 kwa mwaka, ifikapo mwaka 2025, na kuongeza mapato ya utalii kutoka dola za kimarelani 2.6 billion mwaka 2020 hadi kufikia dola za kimarekani 6.0 bilionimwaka 2025

Na ni kwa nini utalii?
Sekta ya utalii Tanzania,ni moja ya sekta muhimu kabisa katika uchumi wa nchi yetu, kwani sekta hiyo ndio inayoongoza katika kuingiza fedha nyingi za kigeni kuliko sekta nyingine yeyote ile hapa Tanzania,Asilimia 25 ya fedha zote za kigeni( foreign currency) zinatokana na sekta ya utalii, Kwa mfano katika mwaka wa fedha wa 2018/ 2019 sekta ya utalii, iliingizia taifa takribani dola za kimarekani 2.4 bilioni( Tsh trilioni 5.2) pia katika mwaka wa fedha wa 2019/2020 sekta ya utalii pekee, iliingiza takribani dola za kimarekani 2.6 billion ( Tsh trilioni 5.4 )

Lakini ukiangalia jumla ya thamani ya shughuli zote za kiuchumi hapa nchini, kwa maana ya pato ghafi la taifa( Gross Domestic product ), sekta ya utalii inachangia 17.6%, ya GDP

Lakini pia sekta ya utalii imetoa ajira za moja kwa moja takribani watu 6000 na ajira zisizo za moja kwa moja takribani watu 2,000,000

Sasa kwa Tanzania, ukanda pekee unaofanya vizuri katika utalii ni ukanda wa Kaskazini, ambapo unaopokea watalii wengi kuliko kanda zingine za utalii,kama, kanda za Kusini na Kanda ya Kaskazini magharibi, takribani 90% ya watalii wote wanaoingia hapa nchini wanaelekea ukanda wa Kaskazin

Sasa ili kufikia malengo ya kuongeza idadi ya watalii, serikali waliamua kufungua baadhi ya kanda zingine za utalii, kanda hizo ni Kanda ya Kusini( mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe,Songwe) ambapo Kitulo ilipandishwa hadhi na kuwa hifadhi ya Kitulo, na kanda ya Kaskazini magharibi yenye mikoa ya ( Geita, Mwanza, Kagera, Kigoma)

Serikali walifanya nini kwa kanda ya Kaskazini magharibi?
Hatua ya kwanza waliofanya, ilikuwa ni kuyapandisha hadhi mapori tengefu ya Burigi, Biharamulo, Kimisi ,Ibanda, Rumanyika & Kyerwa na kuwa hifadhi za taifa( National parks)

1. Burigi- Chato National Park

2. Ibanda-Kyerwa National Park

3. Rumanyika-Karagwe National Park

Sasa ili kuweza kuvutia watalii waweze kufika Kwa urahisi zaidi katika hifadhi hizo, serikali waliona ipo haja ya kujenga uwanja mkubwa wa kinataifa wa ndege ulio karibu na maeneo hayo, ambapo watalii wataweza kufika kwa urahisi zaidi kuliko ilivyo sasa, ambapo kimsingi kunapatikana hifadhi ya tatu kwa ukubwa hapa Tanzania, hifadhi ya Burigi- Chato yenye ukubwa wa kilometa za mraba 4,702, ikitanguliwa na hifadhi za Serengeti na Sellou

Kwa hiyo kwa kuzingatia umuhimu wa kukuza sekta ya utalii nchini, ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Chato una manufaa makubwa sana katika kukuza uchumi wetu

Ngamanya Kitangalala Mwaswala
kngamanya@yahoo.com
 
Amejenga uwanja wa ndege wa kimataifa kijijini kwake hilo ndilo kosa kubwa zaidi ya yote, halafu;

Hata mbuga ya Ruaha ambayo ndiyo kubwa kuliko zote Tanzania haina kiwanja cha ndege cha kimataifa, Selou pia haina, hata the Great Serengeti haina kiwanja cha kimataifa

Kwanini ujenge kiwanja cha ndege cha kimataifa katika mbuga changa ambayo hata wanyama haina na ndio wanafanya kuleta wanyama sasa?

Kwanini ujenge kiwanja cha kimataifa cha gharama za ajabu kwenye mbuga ambapo hata hoteli zenye hadhi ya nyota 2 au 3 hazipo?

Hakuna hata historia ya mapato ya mbuga hizo ndio kwanza zimetengwa na kiwanja kimejengwa wakati kuna Mbugu zinajulikana tangu kabla ya uhuru na zinaingiza mapato makubwa sana lakini hakuna uwanja wa kimataifa

Je, unapojenga uwanja wa kimataifa Chato unataka ule wa Mwanza uliopo kilometer chache tu ufanye kazi gani?

Je, mbona suala la ujenzi wa uwanja wa chato halikujadiliwa bungeni?

Kwanini ndugu yake Magufuli ndio amepewa tenda ya kujenga uwanjwa wa Chato kwa mchakato wenye walakini mkubwa?

Kwanini magu amemweka mpwa wake (Doto Bulembo) kuwa mlipaji mkuu wa serikali? Nepotism.

Ni vigumu sana kumtetea Magu na mambo yako yote.
 
Katika watu wenye mawazo ya ovyo wew wa kwanza. Umejitaidi kutoooa takwimu ili kujenga hoja ila nikiwa Mtalaam wa hayo mambo nakuona kinachokusumbua ni muhemuko tu. Hoja ni kwanin uwanja wa Kimataifa ujenge chato7 ulitakiwa ujikite hapo tu.

NYERERE alisema " CHEO NI DHAMANA, SITATUMIA CHEO CHANGU KWA MANUFAA BINAFSI" haya turudi kwenye hoja yetu. chato ni kijiji anapotokea nani? Na je ametumia cheo chake kwa ajili na MANUFAA BINAFSI kwake? Ukimaliza hilo, ndo utaelewa kwanin Mzee baba hajajibu chochote kuhusu hilo.

Pili, lini bunge liliidhinisha mabilioni hayo kujenga huo uwanja?

Tatu, kandarasi ya ilitangazwa - rejea sheria za manunuzi. MAYANGA construction ana uhusiano gan na Mzee Baba, hajatumia cheo chake kwa manufaa binafsi kwa Mayanga

Nne, ikitokea akapata miaka mingine 5 akimaliza uraisi jiulize huo uwanja ni ndege ipi itaenda tena uko. Mpaka muda huu no ndege ipi inayoenda uko kila cku au wk zaidi ya kumpeleka yeye na ndugu zake.

Hii sio hoja ya kuchokoza ina makondokando meng sana ndugu

NNE
 
Hata mim nimekaa kuzubgumza na malecture hapa wa department of tourism.wanasema ile ni target kubwa ya kuutangaza utalii hasa wa Rubondo ambako kule kuna utalii anuwai,wa maji,wa wanyama kuogelea kuvua sato.yan kama hujafika Rubondo huwez kujua uzuri wake.

sasa ile ni mikakkat endelevu kuja kuitangaza.kwa Nchi zingine Rubondo peke yake ingekua a great tourist attraction haijwah kutokea.
serikal haipang mambo kuangalia leo serikal inapnga mambo miaka 50 inayokuja.

uwanja uke ni sahih kabisa. Wito wa kuiomba serikal yetu sikivu kuikarabat viwanja vyote vya mikoa ziweze kutua ndege zetu
 
Nijibu maswali yafuatayo

1. Ni kampuni gani iliyojenga huo uwanja wa ndege?
2. Je imewahi kujenga viwanja vya ndege kabla ya huu?
3. Mchakato wa tender uliendaje? Kampuni ngapi zili bid?
4. Gharama ya project nzima ni kiasi gani?
 
Uvccm hata kujenga hoja mnashindwa ndio maana wenzenu wakitoka upinzani wanakamata vitengo haraka.
Umeweka porojo nyingi ambazo kimsingi kila mtu anafahamu umuhimu wa utalii nchi hii.

Swala ni je kuna economic viability ya kujenga uwanja chato?.
Na mchakato mzima wa ujenzi ulikuwaje kuondoa harufu ya upendeleo.?
 
Hata kushawishi hujui. Utalii upo Arusha na Zanzibar huko Chato imekuwaje na si gharama kubwa zitatumika kuutangaza huo utalii mpya. Usitufanye wajinga, hapa mmetupiga na tarehe 28 tunaenda kumwaga zege kwenye kaburi lenu ili hata mkifufuka msiweze kutoka.
 
Wewe mleta Post unapajua CHATO au umetumwa kuleta post hapa,

CHATO ni kijijini kabisa, mbuga ya wanyama haina hata wanyama, hadi wasombwe kwa magali ya Jeshi, na wakigikishwa polini hawakai, kwa akili ya kawaida hata ya chekechea, toka uwanja huo wa CHATO ufunguliwe, Kuna ndege ngapi zimepeleka watalii, zaidi ya ndege ya mseveni na ndege ya Ikulu yetu?

Acha kujipotosha hakuna fursa ya utalii CHATO.

Waliokutuma waambie wakupe nauli uende CHATO ukashuhudie kwa macho.
 
Watanzania wote wanajua kwamba ujenzi wa Uwanja wa ndege wa Chato ni ubinafsi uliokithiri wa kiongozi Magufuli. Hakuna sababu kwa nini kiwanja cha Mwanza hakikujengwa kwanza. Kwa kigezo cha uchumi Mwanza inaongoza, Kwa kigezo cha Madini Mwanza inaongoza, Kwa kigezo cha utalii Mwanza inaongoza. Hakuna mtu mwenye akili timamu atayekuambia Chato inastahili uwanja mkubwa namna hiyo. Magufuli akumbuke Mobutu alijenga uwanja wa ndege za concorde kijijini kwake na leo hii kiwanja hicho ni malisho ya n'gombe na mbuzi. Hakuna wa kumdanganya hapa wote tunaelewa vizuri jambo hili.
 
Kiwanja cha Biharamulo kingefaa zaidi kuongezewa na kupandishwa hadhi kuwa cha KIMATAIFA.

SIYO KWENDA KUJENGA UWANJA MPYA CHATO.
 
Uwanja ulijengwa baada ya mama yake Magufuli kupata stroke, ni rahisi kumpeleka na kumrudisha Dar kwenye check ups.
 
Back
Top Bottom