Mkuu jibu bi simple, sio lazima uwe na degree kujibu. Mfano ukitoka mzigo sehemu A kwenda sehemu B kisha mtu wa B akasema nimerudisha mzigo. Wewe unadhani amerudisha wapi?
Je unahakika Benki za ndani hawatoi hiyo huduma. Unaweza toa mfano wa benki uliyoenda ukaambiwa hakuna hiyo huduma? Tatizo wabongo tunataka kufanyabiashara ofisi kwenye begi ambayo haitambuliki kisheria.
Unadhani msaada anaupata huku zaidi ya kutokwa na maneno na kulala tuh! Nenda kwenye page yao ya facebook, twitter lakini pia unaweza kuongeano kwenye website yao (www.crdbbank.com) utapata msaada.
Tatizo watu wanajifanya wanajua sana. Overdraft ni huduma ambayo mtu anaomba haimaanishi kama wewe una akaunti ya hundi unakuwa na uwezo wa overdraft. Saving account inaweza kuwa na deni kwasababu fulani, na kujua nisababu gani? mimi kama mteja natakiwa kuonge na benki husika kujua nini shida?
Ukipita kwa umakini maneno yako utabaini kuwa hakuna hoja ya msingi. Kuhusu kusambaa naamini CRDB wamesambaa sana. Na ni ipi hasa maana ya tenda? ule sio uteuzi. Out of banks wao wameshinda tenda. Isiwe nongwa. Au ndo ukoloni wa kuona benki yenye wazungu ndo ipewe tenda??
CRDB ni benki yetu watanzania lakini pia inachangia sana kwenye ujenzi wa uchumi wa nchi yetu na ndio inaongoza kutoa mikopo kwa miradi ya serikali na kwa watanzania. Kwa nini yenyewe isipate tenda hiyo? Au kwa kuwa ni benki ya watanzania na sisi siku zote tunataka wapate wazungu wa NMB. Kweli...
Acha kupotosha watu kwa kutoa taarifa za uzushi. Gazeti la Mtanzania tunzeni heshima yenu kwa watanzania ili mzidi kupendwa na kuaminika. Toeni taarifa za kweli sio kuuza gazeti tu, tafuteni habari kwa kina zenye ukweli ndani yake. Tunzeni "brand" yenu.
Unapoenda benki unatarajia kutopoteza muda, Kama ukienda na kupoteza Muda sio sahihi. ATM Zenu zinasumbua sana ndani ni msongamano wa watu, mtandao unasumbua.
NMB mobile sio kabisa mbovuuuu unatuma pesa leo zinafika baada ya siku tatu wakati shida imeisha na nimetafuta alternative ya kufanya.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.