Mengi ni mtanzania safi mwenye nia thabiti ya kuinua maisha ya raia wenzake. Juhudi za kumchafua kwa maneno ya kubuni hazitafanikiwa. Kumbuka mti hujulikana kutokana na matunda yake.
Akipata nafasi ya kuhutubia watanzania itakuwa jambo zuri sana. Tuweze kupata mawazo mapya na kujua pia uwezo alio nao kwani nimgombea urais mtarajiwa. Lakini nimjuavyo dr Slaa sijui kama atakubali!
Mnamwogopa sana Dr Slaa. Inavyoelekea mngekuwa na ushahidi japo mdogo tu wa hizo tuhuma zenu mngeziweka kila siku hapa! Lakini maneno matupu kama haya ayaonyeshi chochote zaidi ya woga.
Hayo yameshafanyiwa kazi. Jinsi watu walivyo na kiu ya mabadiliko hawatajali nani anashinda alimradi asiwe ccm tu basi. Nimeliona live leo huku Nzasa leo nikashangaa sana.
Nchi yetu inahitaji maombi. Tumuombe Mungu wa rehema atuwezeshe kupata viongozi ambao watajali maisha ya raia wao maskini. Hospitali hazina dawa, lakini kiongozi anaishi kama vile ana pesa ya mafuta!
Mnajipongeza nini? Hamjajitambua kuwa hamuwezi tena kuongoza hii nchi? Kila mahali mmefilisi nbc, nssf, eskro, iptl na kwingineko. Hakuna ata jambo moja la kujivunia kama watanzania. Pumzikeni tupate mawazo mapya.
Hapana. Wametufanyia mengi kwa kadri ya uwezo wao. Wamefika mahali wamechoka wanatakiwa kupumzishwa. Kwa heshima watakubaliana na maamuzi ya wengi na taifa litasonga mbele, maisha yataendelea. Mungu wetu, kwako tunaomba baraka tuweze kubadilisha uongozi wa taifa letu kwa amani na utulivu.
Labda kama umeumbwa hivyo! Wengine hawawezi kujifanya tofauti na utashi wa nafsi zao. Mimi ni mmoja wa wasioweza kufanya tofauti na utashi wa nafsi niko huru sana.
Tumia akili yako vizuri, makosa yao hayafanani.
Hawa polisi wanaomwagia mama zetu maji ya kuwasha kwa kutumia haki yao iliyo kwenye katiba wanatumwa na nani? Nchi inaendeshwa na polisi, ajabu!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.