Sasa watuu wataweka details zote hapa? Terms ni kati yake yeye na mwekezaji ambaye atakuwa yuko tayari, watakaa chini watajadili namna nzuri ya kufanya.
Mimi nadhani haya ni matokeo ya kisiasa yasiyo na tija kwa mkulima . Kuendekeza sera za ujamaa kwa mkulima na katika dunia ya kibepari ni kuwatia umaskini wakulima. Sasa hivi kilimo ni biashara, hata mazao ya chakula ni biashara pia. Kufunga masoko ya nje ili kulinda "mlaji" wa ndani ni...
Mkuu, bora hata huyo ambaye hakurudi kabisa. Shida ni kwa yule ambaye alijichanga akaamua kurudi kwa matumaini kwamba pesa itamkuta kwenye hatua labda ya palizi au ya mbolea. Mtu anajikusanya kwa nguvu zote ananunua mbegu, analima, anapanda, anapalialia....hapo kwenye mbolea ndiyo keshaanza...
Sasa utamuuliza nani ndugu? Maafisa wa NFRA watakwambia hawajaletewa pesa, wanasiasa watakujibu kiasiasa, kikubwa ni kwamba toka mwezi wa tisa mwaka jana kuna wakulima hawajalipwa pesa zao. Wengi wamepata hasara mashambani sababu pesa ya pembejeo iko NFRA.
Hawana hata mpango, hata kuzungumtia tu, hata kutoa ufafanuzi kuwapa matumaini wakulima. Hapo ndiyo mtamkumbuka Bashe na janjajanja zake lakini alitufaa,
Nyie watu huu ushauri sjuwi huwa mnautoa wapi. Mahitaji ya mkonge ni makubwa kuliko uwezo wa nchi kuzalisha. Yaani mtu mpaka amenunua shamba amepanda zaidi ya eka 60 unafikiri hajafanya utafiti?
Mwanzo nilidhani anamaanisha Nusu Hekta, ambayo ni sawa na ekari moja na kidogo, hiyo inawezekana bila shaka. Lakini kwenye comment amekuja kufafanua kwamba alimaanisha nusu ekari, hapo ndiyo amejidhihirisha kwamba hajawahi kufanya kazi ya kilimo hapa Tanzania.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.