UTI mara kwa mara, maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kiuno kuuma hiyo ina uwezekano mkubwa wa kuwa ni UTI ambayo haikutibiwa vizuri na dawa zenye viwango nadhani na ndiyo maana nashauri kupima mkojo pamoja na culture na sensitivity itakayoonyesha aina ya maambukizi pamoja na dawa inayowaweza...
Niwie radhi sana ndugu yangu naishi ughaibuni hivyo nikiri kwa nyumbani sijui gharama zikoje. Kupima mkojo kuangalia kama kuna maambukizi na kupima damu kuangalia kama figo ni nzima kungesaidia zaidi kuliko ultrasound
Pole sana . Muone daktari akusaidie kukufanyia vipimo. Pima mkojo pamoja na culture na sensitivity, pima damu kuangalia utendaji kazi wa mafigo yako, ultrasound inaweza kuboresha wigo wa kuangalia mafigo na vitu vingine tumboni. Pima na choo. Kukata tamaa kama unavyosema kunaweza kuchangia sana...
Ah si soma heading halafu uendelee tu. Siyo lazima kusoma kila kitu. Kwa namna hii utakuja kutuhimiza tuache kufuatilia kampeni za Mheshimiwa Rais. Wengine tunapenda kujua yajayo.
Pole sana ushauri wangu ni kwamba siku nyingine ukinunua dawa dukani usisahau kusoma maelekezo nje ya boksi. Jivu la Kongo ni la kuchelewesha kufika kileleni. Na limefanya kazi kwako vizuri kupindukia. Mimi nilidhani unalalamika kwamba ulitapika mara baada ya kunusa tuu kumbe ilikuchukua masaa...
Hapo umenena vyema. Ujira unaendana na uefanya au unafanya nini . Sasa mtu akiwa na PhD lakini kazi yake ni kukata tiketi za ushuru wa mabasi yaingiayo stendi ungependa alipwe milioni tano? Wakati mwingine hebu tuacheni ushabiki.
Ninatumaini Mheshimiwa waziri atakuwa amefanya homework ya kutosha maana maziwa ya maji yana changamoto zake hasa kuyafanya yabaki fresh kwa ajili ya chai vinginevyo watu watakunywa chai ya mtindi. Na nahisi hii sheria inawahusu Dodoma, Shinyanga na Mwanza maana nilipoishi Mtwara na Masasi...
Wengine tuliosoma kipindi kile tulipewa maboom nakadhalika BURE na wakati huo gesi, mafuta na uranium vilikuwa bado havijagunduliwa, na hazina mpya za madini ukanda wa Mbeya, Sumbawanga mpaka Kigoma ilikuwa haijagunduliwa, na Kenya bado walikuwa wanauza Tanzanite duniani kama wenye migodi wakati...
Jamani, huu ni ushauri tu. Haya mambo ya kuandika andika vitu, hasa kashfa bila kufikiria madhara yake ni hatari sana. Je unajua Mzee Slaa akipeleka madai yako mahakamani unaweza kufungwa au kulipa faini? Kuweni waangalifu jamani, msichukulie mambo kienyeji kienyeji yanaweza yakawaliza machozi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.