Unamwonea Bashuru tafadhali. Katibu Mkuu Kiongozi ni ngazi ya juu sana ya utawala. Haiendi kwa shule peke yake. Nawashangaa wanaochezea nafasi hiyo kwa kuchaguana kirafiki!!
Suala hili si rahisi kulielezea ila linafikirisha. Katika historia kuna maswali kama kwa nini Wajerumani na akili zao waliruhusu Hitler akaua binadamu wengi kiasi hicho? Jibu ni kwamba katika kila jamii huwa kunatokea wakati ambao sehemu kubwa ya jamii inarubuniwa na viongozi wachache waovu na...
Maelezo mazuri ya historia na umenikumbusha watu ambao nilikwisha anza kuwasahau! Nakushukuru sana. Ila katika orodha hiyo wengi wamesha kwenda mbele ya haki na siyo wale uliowataja peke yao. Pili, hoja ya G 55 ilianza baada ya jaribio la Zanzibar kutaka kujiunga na OIC bila kuihusisha Serikali...
Ni kweli unaweza kuuliza wazee wastaafu walikuwa wapi. Lakini somo la saikolojia na hulka ya binadamu ndiyo inatoa jibu. Ukiacha kiongozi mmoja na mwingine nusu, wengi wao wanajali namna watakavyotaka kuzikwa kuliko kugombana na viongozi wa sasa. Hili jibu nalitoa kama unataka maelezo yasiyo ya...
Hapo sasa ndipo uone Serikali zinavyokuwa wasemaji wa makampuni yao makubwa ambayo kwa hakika ndiyo yenye usemi. Timing ya pressure yao kwa serikali yetu nayo ni jambo muhimu la kuzingatia. Ndiyo maana kuna pressure pia ya kuondoa zile sheria zilizopitishwa na Bunge kulinda maliasili za...
Hata mimi nina mambo mengi ambayo nimeshuhudia Mzee huyu akionesha utu na uungwana wake. Uliloandika latosha na nashukuru umefanya kwa niaba yetu sote. Mwenyezi Mungu Amrehemu Mzee Mwinyi! RIP Mzee Ruksa!
Matamshi hayo yanawezekana katika nchi zinajulikana kama " Banana states." Ni kiasi cha kujiorodhesha na kujipa u Sultani wa bandia tu, basi unakuwa Kiongozi wa Banana state. Mhe. SSH hataki hiyo sifa!
Utawala wa Serikali hauendeshwi kwa mujibu wa imani. Kama maafa yangetokea na wahusika wakapelekwa mahakamani hapo ndipo tungesikia kama imani ya mpanga njia ya kiongozi wa kitaifa ni utetezi unaokubalika kisheria. Tukemee kufanya maamuzi yenye uwezekano wa madhara ambayo tunaweza kuyaepusha...
Ni wajibu wa Serikali kuhakikisha bidhaa muhimu zinapatikana wakati wote bila kutoa umuhimu wa mhula wo wote ule. Sera ya kuwaachia walimaji sukari kuwa na usemi kwenye uagizaji wa sukari pungufu ulitoa ushindani ukawahakishia walima sukari kupata faida kupitia bei wakati wote bila kujali tija...
Mimi ni Ofisa wa Serikali mstaafu na si shabiki wa chama cho chote wala Simba au Yanga. Nashangaa ofisa gani Mwandamizi wa Serikali anaweza kumpitisha Kiongozi ye yote wa kitaifa katikati ya halaiki ya maandamano ambayo ni rasmi, achilia mbali ya kiongozi mwenyewe kuafiki huo utaratibu. Ni aibu...
Ni kweli. Nakumbuka zile kampeni za Kikwete awamu ya kwanza ya Urais zilipendeza na dunia nzima ilijua kuwa Tanzania kuna demokrasia na kwa mara ya kwanza nilisikia usemi wa "Chaguo la Mungu". Watanzania kumbukumbu zetu ni fupi sana!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.