Safari hii hujajipanga, huwenda ulikuwa unaandika hii thread ukiwa msalani. Hakuna aliyepinga kuwa Aatish hakodishi Ambulances. Hoja hapa ni wewe kututhibitishia kuwa hizo Ambulances kauziwa na Lema. Vinginevyo, unacheza mchezo ule ule wa ccm kupakazia vyama mbadala!
Hebu nielezeni nielewe; kwanini mnaitetea Rwanda, hivi inahitaji digrii kuelewa M23 ni wa-Nyarwanda? Hili ni kundi linaloungwa mkono na Rwanda kwa ajili ya maslahi ya Rwanda. Chuki yote ya Kagame dhidi ya Tanzania ni kutokana na Tanzania kupeleka majeshi Congo na kutoa kichapo kwa M23.
Hata mimi niliyepitia jeshi nimechanganyikiwa, possibly tunatakiwa kwenda Refresher Course. Cheo chake ni Luteni Kanali (Lieutenant Colonel) lakini kofia aliyovaa si ya cheo hicho (ua la mbele), kofia hiyo huvaliwa na na Colonels & Brigadiers.
Tatizo lako sijui ni ufahamu mdogo wa lugha ya kiingereza au basi tu nawe uonekane umepost kwenye thread husika..!? Kusema "I love you" haimaanishi kumpenda mtu kimapenzi pekee bali pia upendo uliopitiliza kutokana na mambo anayofanya au aliyofanya. Vile vile hutumika kuelezea upendo kwa watu...
Mkuu inaonekana hujaelewa, waliolalamika ni Ubalozi wa Tanzania uliopo Rwanda. Na kwa kuwa wapo Kigali, wamelilalamikia gazeti moja kwa moja. Sio sahihi kwa wao kupitisha malalamiko Ubalozi wa Rwanda hapa kwetu. Serikali hapa ndio inaweza kuwasilisha malalamiko kupitia wawakilishi wa serikali ya...
Hebu tujuze, anatoa wapi hela? Nijuacho mimi miradi yote inatekelezwa kwa fedha za Halmashauri inazopata kupitia kodi na ruzuku (kama ipo) toka Serikali Kuu. Halmashauri ya TMK ina mpango kazi wake na vipaumbele vyake. Hivyo miradi ya barabara inatekelezwa baada ya kupitishwa na baraza la...
Unadhani wote waliokuwepo kwenye huo mkutano ni wanaccm? Je kwenye zile kata 4, mikutano yenu haikupata watu ndio maana mkashindwa vibaya? Wingi wa watu kwenye mikutano ya kampeni si kigezo cha kukubalika au kushinda uchaguzi. Chaguzi za kuangalia chama zimepitwa na wakati sasa hivi, watu...
Labda nisaidie kuelewa; CDM ilianzishwa Kaskazini? Makao yake Makuu yapo Kaskazini? Wajumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ni kutoka Kaskazini? Hebu nijuze ili nione kama nikuunge mkono kwa hili la ukaskazini wa cdm!
Naona unashindwa kutofautisha kati ya jina Stephen na Wassira. Wassira ni ukoo ambao una watu wengi nyuma yake. Kwa hiyo kama huyo ndugu analitumia basi huenda ana uhusiano nalo. Iwapo analitumia kwa kumaanisha Stephen Wassira basi amepotea maana huyo anayeitwa Stephen Wassira hana umaarufu...
Kweli script ni nyingi. Huyu ndugu mbona anajichanganya? Maelezo yake ya awali yanatofautiana kabisa na haya. Mwanzo alisema alikuwa kwenye baa na sasa alikuwa njiani akielekea nyumbani. Tushike lipi na tuache lipi?
Nakubaliana na wewe. Ni kutokana na udhaifu huo wa uongozi ndio maana kina Shoza na wenzake walipokea pesa kuihujumu CDM. Vile vile na kubaliana na wewe, ni kutokana na udhaifu huo, ZZK alikisaliti chama kwa kusaidia wagombea kadhaa wa ubunge kupitia CCM wapite bila kupingwa. Kama hiyo haitoshi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.