Una uhakika gani ana warithi na kama anao umejuaje anataka kuwaachia urithi wa fedha. Hicho kikokotoo kwanini hakiwahusu wabunge na mawaziri au wenyewe wanaishi milele
Kuweka karibu milioni 100 kwenye fxed account na kuishia kupata milion 7 kwa mwaka ni uvivu ama uoga wa kuwekeza hiyo pesa. Kuna mizunguko ukiiweka hiyo milioni 100 kwa mwaka unakua umefunga milioni 300+.
Kujenga nyumba ya kupangisha ni biashara za wastaafu na waoga wa kuchukua risk.
Kazi za kuchosha mwili na akili kwa maslahi ya dàgaa watu wameshaachana nazo, hakuna mtu anayekataa kazi ikiwa na maslahi. Tatizo mnaotoa kazi mnapenda kunyonya watu kwa kisingizio unafundisha kazi na blahblah zingine za kinyonyaji.
Ifikie mahali watanzani tuache kulialia na kauli za tunaiomba serikali ili hali Serikali iliyopo imeshindwa kuongoza nchi alafu tena unaendelea kuiomba. Muhimu tuje na mbadala mwingine wa kuweza kutatua matatizo yetu ya ujinga na umaskini.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.