Jamani wadau hivi hii serikali ina mpango gani na ndoa zetu maana sielewi. Huu ni unyanyasaji wa kiwango cha juu maana kama ni uhakiki umeshaisha lakini mpaka sasa hawataki kutoa uhamisho. Kama ni uvumilivu kwakweli tumevumilia mno. Tukisema serikali haipendi watumishi wake tutakuwa tunakosea...
Yani hata aijulikani maana ukiwapigia simu tamisemi wanasema wanasubiri tamko la magu aruhusu Ila wanasema haitafika mwezi wa Saba hivyo ngoja tuone mwezi huu au aprili
Mimi niliwapigia simu ijumaa iliyopita wanasema barua za uhamisho zipo tayari wanachosubiri ni agizo la rais kuruhusu uhamisho na ajira ndipo watatoa. Hivi mambo kama haya si yanahamuliwa na waziri husika? Kwa kweli hii ni shida.
Yani maisha ndo yanazidi kuwa magumu na hivi mwezi huu ndio wamekata 15% ya mkopo wa bodi yaani ndio Hali inazidi kuwa mbaya. Watuonee huruma tu watoe sasa huo uhamisho
Mimi leo nimewapigia simu tamisemi wao wanasema wanasubiri rais aruhusu ndio wao watatoa uhamisho. Hili na hili nalo wanasubiri maamuzi toka kwa rais ina maana gani ya kuwepo waziri katika wizara. Ama kweli hii kali
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.