ili kuing'oa ccm tengeneza vijana ingiza kwenye mfumo wa ccm wakishapata nafasi wanafanya mambo kwa maslahi ya nchii. Hii inatakiwa kuwa long term project ni kama USA walivyoisambaratisha Urusi.
Martin Maranya ni rika moja na Mnyika labda ungesema uongozi utengeneze mkakati wa kuandaa vijana na sio kuwakabidhi madaraka.
Vijana wengi waliotengenezwa na Chadema wamerubuniwa na ccm na kupewa uongozi. Ni bora kubaki na kina Mnyika ukijua unabaki na watu wanaokipambania chama.
Mbowe amekuwepo kwenye uongozi mpaka wamemchoka, Mnyika na Heche ndio wamepokea vijiti kwanini unakimbilia kusema wamezeeka wakati umri walio nao ni sahihi.
Kwanini usiwape ushauri ccm ya kna Wassira na Dr Migiro.
Hiyo ni hatua ya kwanza, hatua ya pili ni kudai fidia. Kuna kipindi mkutano ulifanyika Afrika Kusini kuhusu kudai fidia baadhi ya nchi zikavuruga kwa makusudi kuingiza swala la Palestina na Israel kwa sababu ya mitazamo yao ya kidini.
Argentina wanajua walichofanya dhidi ya waafrika wana hofu...
Biashara inahitaji uvumilivu, kaa angalau miezi sita ndio ufikirie kufunga biashara.
Kuhusu wafanyakazi wengi wanaokotaokota tafuta angalau mfanyakazi mmoja aliyesomea mambo ya hotel atakusaidia kuanzia ubora wa chakula, lugha ya kuzungumza na wateja na mengineyo.
Mwalimu Nyerere alishagundua alifanya kosa kuungana na watu ambao wana ubinafsi lakini hakutaka kurudi nyuma ila kuungana na watu kama hao ni tatizo kubwa.
kwanini hizo nchi zisisusie kushiriki kombe la Dunia, USA haina athari yoyote katika soka la Dunia wao michezo yao ni BasketBall, Baseball na American Football.
Maandamano makubwa nitakayoshiriki ni kuikomboa Tanganyika na kudai katiba mpya, Lissu najua ataachiwa ila bila kupigania mambo ya msingi hizi kesi hazitaisha watakamatwa watu wengine lakini kwa sababu hawana influence kama Lissu wataozea gerezani.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.