Kwangu mimi huyu ndo alikuwa mtume wa kweli kwa Tanzania (Tofauti na mitume wa sasa wanang'ang'ania kuhubiri utajiri badala ya kuwakumbusha watu duniani tunapita), kwani alihubiri katika tabu na mateso makubwa, matunda yake tunayaona sasa. Mwisho wa Safari yako duniani imefika, kapumzike kwa...
Kuna ajali nyingine tena lori limeparamia coaster eneo hilo hilo tena usiku huu wa saa moja na nusu Hivi hayo mataa wameweka urembo, ni muda mwingi utakuta haziwaki wakati eneo lenyewe ni la hatari
Dah, nimejikuta nimetoa chozi baada ya kusoma ujumbe huu. Pole sana Mkuu najua kidonda cha mapenzi kinavyouma, Mungu na akutane na huzuni yako, akupe mke aliye mwema atakayekusahaulisha yote haya. Cha muhimu tuliza aikili yako usifanye papara kutafuta mwingine, mshirikishe Mungu katika kila...
Hapa inabidi tuwaangalie wote wawili Amu na Ticha, wengi wetu tume base upande mmoja wa kumuonea huruma ticha. Lakini tukirejea post karibu zote za Amu inaonyesha Ticha kwa sasa hana nafasi tena. Hivyo hata akiambiwa arudi kwa ticha itakuwa sawa na kutwanga maji kwenye kinu. Nafikiri kuna kitu...
Unachokisema mimi nakuelewa sana na nakuunga mkono... maana hata huyo ndugu yangu kwa sasa anajuta kwa alichokifanya lakini hawezi rudi nyuma tena. Ila kwa hali aliyofikia Amu ni ngumu kukubaliana nawe, akili yake imefikia kikomo. Nafikiri ili asizidi kumuumiza huyo kaka ni vyema aachane nae tu...
Mkuu sidhani kwa hatua aliyofikia Amu kama atakuelewa. Nafikiri achague anachokitaka yeye maana keshafika kwenye point ya kutokurudi nyuma tena ambapo hata kama akiamua kuolewa atamuumiza tu huyo ticha. Bora amwambie mapema tu huyo kaka ataumia lakini maisha yataendelea. Kuna ndugu yangu alikuwa...
Hii ni tabia ya mtu tu si kwamba ni kwasababu msichana au mvulana, hata nyie wanaume kuna baadhi yenu hawafikirii mara mbili (Ninakwambia hivyo kwa sababu yamenitokea mimi).
Amu pole kwa mawazo, nafikiri ni vyema umwambie ukweli tu huyo kaka kabla mambo hayajaenda mbali zaidi. Maji ushayavulia nguo sharti uyaoge. Kiukweli namuhurumia huyo kaka kwa jinsi atakavyopokea maamuzi yako (najua inavyouma kwani nami ilinitokea). Lakini huwezi kupretend kama wampenda kisha...
Kaka yangu kwa jinsi mapenzi siku hizi yalivyo ni kama sinema usithubutu kutanguliza pesa mwanzoni. Inavyoonekana alishakusoma akajua unazo. Mwanamke gani siku ya tatu tu ushaanza kuomba hata haya hana kha!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.