Mjinga mwenyewe ,jenga yako ufanye hivyo. Suala la nyumba za kupangisha ni kama shule tu. Shule zingine unalipa ada mara moja kwa mwaka, nyingine unaambiwa mara 2, nyingine mara 4. Hivyo unapeleka mtoto kwenye shule unayoimudu. Ni hivyo hivyo kwenye nyumba wengine wanachukua miez 2, wengine 3...
Usikurupuke mimi sio mleta mada na pia na wewe maelezo yako hayajitoshelezi. Jifunzeni na kama ni ngumu kuelewa basi kubali kuwa hujui maana shida yenu mafundi mnaamini kila kitu ni cha kujua tu mtaani wakati ukweli vitu vingine ni vya kielimu zaidi.
Fundi ni hivi unapoambiwa ratio ya...
Yuko sahihi .Ni mambo ya shule kidogo .Anaposema ratio ya cement na mchanga ya 1:3 maana yake ujazo wa cement/ujazo wa mchanga=1/3=0.33. Lakini pia Resho inaweza kuwa kwa upande wa uzito. Sasa anaposema mfuko mmoja wa cement changanya na ndoo 6 kubwa, sababu ni kwamba mfuko mmoja wa cement...
Picha haina madhara kwa jamii ya umri gani? Kijana mdogo wa kiume labda umri miaka 13 na dada yake ukiwakuta wamekaa hivyo nyumbani ni sawa?
Ndio maana watoto wadogo wanakuwa na muongozo kwenye kutumia mitandao ili kuepukana kuona na picha kama hizi maana kwao ni rahisi kuiga kwa namna tofauti.
Jibu ni kwamba hakuna mtu anaenda kanisani akiwa amelewa ,hata kama kunywa pombe hakuna shida lakini je kila mlevi akijirekodi amelewa huko baa na kusambaza kwa public je ni sawa hiyo?
Sio kila jambo unalofanya hata kama ni halali linapaswa kuonwa na public. Ni kama tu mamiziki ya mabongo fleva mengine unavyoyaona hayafai kutazamwa na watoto.
Kila vazi na maeneo yake ila maadili ndio yamefanya iwe hivyo. Sio kila ulivyovaa maeneo fulani yapaswa kuonwa na kila mtu. Umeenda beach au klabu ya usiku unaweza kuvaa kwa mazingira hayo ila sio kila vazi ulilovaa huko upige picha usambaze kwa public.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.