Mheshimiwa Zitto nafasi pekee ya jina lako kuandikwa vyema katika historia ya nchi hii ni kuwa mnyenyekevu, kili makosa. Ahidi na uwe mwaminifu kwa chama chako, bila shaka utavuna heshima na si aibu. Kutenda kosa si kosa.
Mleta mada ni mmojawapo wa watanzania ambao bado hawajajitambua. Wasiojitambua huwapa hadhi na heshima wezi wa mabilioni ya walipa kodi, lakini wako tayari kumtoa roho mwizi wa kuku. Ndiyo maana leo kijana ameajiliwa mwaka huu na anaonekana makini anapomiliki mali mwaka unaofuata na kuwa tajiri...
CCM inakufa ikiwa haina viongozi, inawaganga njaa tu. Nasema hivi kwa sababu hata tukimuangalia usoni, Mchemba anaonekana anasema au ameandika asichokiamini. Nani mjinga wa kuamini hayo ambayo hata mwenyewe unajua kwamba huyaamini?
Ivi Mheshimiwa mbunge mstaafu Warid Kabouru alikuwa mwenyeji wa mkoa gani. Mbona historia yake ni kusaliti mageuzi akarudi CCM. Isije ikawa hata watu wengine wa huko kwao walio upinzani wakawa wanatumika kama alivyotumika huyu mbunge wa zamani. Tanzanians take care.
Waliotuhumiwa kwenye mtandao (Zitto na wenzake) ni sawa na kisa cha kuoga mtoni, mwendawazimu kachukua nguo zenu anatimua mbio. Nanyi bila kutumia akili mnatimua mbio kumfuata mkiwa uchi wa mnyama. Kwa kashfa hii, tutamuona anayestahili kuwa kiongozi CDM.
Mvivu wa kufikiri pekee ndiye atachelewa kugundua kwamba Mchange kwa kuamua kutumika kuivuruga CDM umechagua jina lako lisomeke kama majina yenye laana katika historia ya matengenezo ya taifa letu. Kama unahekima rudi chamani uombe radhi utasamehewa. Mtu kujiunga na Chama mapema si kigezo cha...
Wooote mnao mtetea Zitto ni wapenzi wa CCM, mimi nawapeni pole kwa sababu chini ya uongozi mahili wa Mbowe mmeshindwa na sasa mmelegea. Mbowe mtamhonga nini, amezaliwa kwenye familia ya fedha. Sasa mnataka mapandikizi wenu mlio wanunua waongoze CDM mbinu hiyo mliitumia kuiua UDP, NCCR Mageuzi...
Wana CDM & Wana CCM jiulizeni: Kwa nini wenye mwelekeo wa CCM hapa jamvini wanamfagilia sana Zitto Kabwe na wanadhihirisha chuki zao dhidi ya Mbowe? Ebu tusiwe wavivu wa kufikiria.
:sad:
Sijaona sababu yoyote ya kusababisha kutilia shaka utendaji wa Mh. Mbowe katika uongozi wa Chama. Kama ni kufukuza wasaliti ndani ya Chama, hakuna adhabu mbadala kwa wasaliti wa CDM wanaofanya kazi kwa siri na Mzee Wasira, Mwigulu nk. CCM hawajapata kupumua vizuri katika kipindi chote cha...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.