kila jambo na muda wake, muda wa kazi ni kazi, nyumbani ni family business,
sio tu mkiwa career moja, hata kama mpo tofauti cheo kinatakiwa kuishia ofisini.
nyumbani ni mama au baba
hakuna namna ambavyo utachagua pesa over mwenzi wa maisha, never...pesa zinatafutwa na mkizisaka kwa pamoja mtapata tu.
mi ningechagua tu kubaki na mume wangu izo pesa ntaziacha tu zipite.
unaweza chagua pesa na kamwe usizifurahie pale unapokumbuka umemwacha mwenzio kwa ajili hiyo.
pesa...
mwee kikwetu sie kumlea mama mkwe sio ombi ni lazima, na kwanini usimlee labda, huyo ndo mama mzaa chema kama unampenda mumeo lazima upende na familia yake, wala hutakiw kuuliza. yani wew ukae na mama yako kwa mumeo halaf mama yake asiwepo, hiyo haipo
ila inategemea na mila zenu na tamaduni...
hivi siku hizi hakuna siri za familia eeh...mambo kama hayo ni yako ya ndan kaa na mwenzio mshaur afanye mazoez kwa hekima. ila naona umeoa ukiwa bado hujafika umri wew
sioni changamoto hapo, kama unampenda mkeo na unaijali familia yako usiangukie kwenye huo mtego.
hapo ndio mwanzo wa kuisambaratisha familia yako na kuharibu kazi, usitegemee ukimwajiri atakuwa na utendaji kazi mzuri wa kazi.
weka kazi mbele, ondoa tamaa kichwani.
kwanza kitendo cha kuzini na shemeji yako ndani ya kitanda mnacholala na mumeo ni dharau kubwa mno.
halaf unathubutu kumsifia, hivi kwanza unaanzaje kutamaniana na shem wako.
mi naomba na shetani ampitie mumeo huko aliko aje na mke mwingine
ndio maana huwa tunaambiwa kuna maisha baada ya matarumbeta kuzimika,
ndoa ina changamoto na kama umekubal kuingia lazima uwe tayar kukabiliaba nazo,
yeye atulie apokee mtoto walee maisha yasonge mbele
unaambiwa ukipenda boga upende na ua lake, mi huwa sielew kwann watu wanakuwa na chuki na watoto wa nje wa wenzi wao, mtoto ni mtoto tayar ni damu ya mumeo na ni sehem ya familia. tatizo tu ni kutojulishwa mapema, ila kama umempenda mtu mtoto sio kikwazo.
kama mlikuwa na mpango wa kuwa na watoto...
kwanza unataka kumkatili mwanao utakaomzaa haki yake ya kumjua baba yake ni nani na kufaidi malezi ya wazazi wote wawili,
si kweli kuwa unampenda huyo baba kiasi cha kutaka kumzalia ila ni tamaa tu zinakusumbua na unajua ukizaa utaendelea kutunzwa.
ushauri wangu, achana na huyo mume wa mwenzio...
Sasa wew unataka hadi mahusiano yaote sugu ndo akupeleke kwao , hiyo ni ishara nzur na kakuheshimu sana kukupa hiyo nafasi, ila kwa vile wew huna malengo mwambie dada wa watu ukweli atafute mtu anaestahili heshima hiyo
Ww utakua unataka kumrudia mtalaka wako ndio maana hutaki hata kumpa mwenzio nafas ya kujielezea , yani tuseme umepata pa kutokea, huwez jua labda ni utani tu na wala hana mahusiano nae vitu vingine ni vya kumkanya mtu maisha yakaendelea.
Ila ww kwavile unaonekana unataka legal wife arud haya...
Ww utakua unataka kumrudia mtalaka wako ndio maana hutaki hata kumpa mwenzio nafas ya kujielezea , yani tuseme umepata pa kutokea, huwez jua labda ni utani tu na wala hana mahusiano nae vitu vingine ni vya kumkanya mtu maisha yakaendelea.
Ila ww kwavile unaonekana unataka legal wife arud haya...
Hayo ndo malipo ya kuacha mke ndani na kukimbizana na vidada, hiyo pesa ungempa mkeo angweka stock ya chakula ndan mngekula mwezi.
Jifunze sasa usirudie
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.