Wimbo uliounukuu haujatoka nchi jirani ila tuliumba sana hapa nchini miaka ya 60s na 70s mashuleni na JKT wakati wa kukimbia machakamchaka. Nyimbo nyingine maarufu zilikuwa za kumlaani nduli Iddi Amin na Banda wa Malawi pia kuna nyingine na vibwagizo kibao kama "kaburu akija chija"
Ikulu ipo katikati ya barabara ya Luthuli na Barack Obama (zamani Ocean road) na kwa pande zote kuna mageti ya kuingilia. Pia upande mwingine kuna barabara ya Magogoni ndio maana wengine huiita Ikulu ya Magogoni.
Hakuna mkoa wa Moshi, Songea wala Musoma bali hiyo ni miji katika mikoa ya Kilimanjaro, Ruvuma na Mara. Nilikuwa natoa tu elimu ya jiografia ya nchi yetu.
Mdau kabla hujatuma kitu jaribu kwanza kufanya utafiti ili usijiabishe. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii sio ya muungano, SMZ wanayo wizara yao ya afya na inaongozwa na Mhe Juma Duni Haji.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.