Ni uzuzu tu. Kama unataka dini nenda nyumba ya ibada au kapigie kwako. Wabudha , wakristo, waislamu, wapagani nk kila mmoja akipiga numb za dini yake si itakuwa tafrani? Inahitaji ustaarabu tu wala sio nguvu nyingi kuelewa hili
Kuna haja management kujitafakari haraka sana. Dhana ya mwendokasi inakufa. Huduma haimvutii mtu mwenye gari yake kuiacha nyumbani atumie usafiri wa UDART. Wajitafakari kwa kweli
Sasa bila wafanyakazi kulipwa vizuri wakulima na wafanyabisshara watapatia wapi? Wafanyakazi wakilipwa vizuri watanunua vyakula mkulima afaidike, atanunua bidhaa mfanyabiashara aneemeke, atajenga fundi apate ajira nk. Sasa wafantakazi wasipolipwa vizuri hawa wengine wataneemekaje?
Hakuna nchi iliyoendelea ambayo hailindi baadhi ya viwanda vyake. Hoja labda iwe ni viwanda gani vilindwe. Huwezi kuachia uholela kila uchafu uingie nchini halafu utegemee kuimarisha viwanda vyako vifikie hatua ta ushindani. Acha wenye uwezo wanunue vya nje ili vya ndani vijitahidi kufikia ubora...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.