Acha kujiondoa ufahamu mkuu,. Hivi nikuulize Kuna haja gani ya kuwepo vyama vingi, wakati vinazuiwa kufanya hata mikutano!!, hivi nini mantiki ya uwepo wake!!, wakati uhai wake unakuwepo kwa kuitisha mikutano??
Watu kama nyie mna matatizo sana,. Hakuna kitu kinachoitwa kibali, kinachotakiwa ni taarifa kwa ajili ya kupata ulinzi basi, ndani ya masaa 48, usiongee ki kereketwa mkuu, hii nchi ni ya watanzania wote, hakuna mwenye hati miliki, vinginevyo futeni vyama vingi mueleweke.
Lkn jamaani, mtu amehitaji cv ya nini kumkashifu??, kuuliza cv ni mhimu, sehemu yoyote ukiomba kazi lazima uambatanishe na cv yako. Kama hakuna jibu ni bora kukaa kimya.
Tatizo maelezo yako yamejaa ushabiki zaidi kuliko hoja. Unaposema alienda huko kwa maslahi yake au mradi wake unamaana gani!!. Na je kwa kwanini unadhani ataachana au atarudi alikotoka??, mi nadhani hayo hayatuhusu ni juu yao wao.
Watu kama nyie ndo bado mnaamini mtu akitoka ccm basi amejichumia majanga na hivyo hatofanikiwa kwa namna yoyote. Haya mawazo yamepitwa na wakati dada, maisha ni popote.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.