Ni sawa lakini kuna uhakika wa kipato kwa anyefanya kazi na ana nidhamu ya pesa. 2018 mmoja wa jamaa zangu alinialika pale New Orleans na nikapata wasaa wa kuwatembelea marafiki walioko huko, wengi wao wako vuzri, hawana nyumba kule lakini hapa bongo wamewekeza sana. Ni ajabu kuipondea ile nchi...
Nani anayefikiri hivyo, ukweli ni kuwa kule kuna fursa nyingi kama umeingia kwa njia halali. Utapambana lakini inakulipa. Hapa unashindia shamba unalima ufuta, utakachokipata hakitoboi hata miezi mitatu. Unaanza msoto mpaka msimu ujao. Bongo watu wanapambana sana ila tija ni ndogo sana.
Mbona wewe unataka kupangia watu maisha?. Nina ndugu na maclass mate wako huko tangu 1990s, na familia zao wako njema na jamaa wamewekeza. Acha kugeneralised mambo mkuu.
Punguza ujuaji mkuu, yaani 400K uibane hadi ujenge? Labda uwe unaishi sayari ya Mars. Hiyo elimu tunaijua sana, tatizo kwa hiyo pesa hesabu hazikubali kabisa.
Siku nilipomuona aliyekuwa nadhani waziri mkuu wa Uholanzi akienda kukabidhi ofisi kwa usafiri wa baiskeli, nilishangaa sana. Makabidhiano yenyewe utafikiri mwalimu mkuu wa shule ya msingi anakabidhi ofisi, yaani ni dakika chache tu wamemaliza
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.