Achana na ukawa, fanyakazi zako. Asimilia kubwa walioko upinzani walitoka CCM baada ya kuona mfumo wa CCM huwezi kuwaletea wananchi maendeleo. Unaona nini cha ajabu Lowasa kuhamia Chadema, hapa ni mabadiliko tu, na sio Magoli ya mikono na watu mnaotumiwa na CCM.
Kauli sitaawangusha inatakiwa itolewe tayari umechaguliwa. Vinginevyo wanatoa wanariadha au bondia, lakini kwa mgombea anaomba wapiga kura wasimuangushe.
Hizi ni kauli za mfa maji Haji kutapatapa, huu ni moto wa petroli hauzimwi kwa maji. Baba utawala mzuri, mjiandae kisaikolojia kuwa Chama cha upinzani.
Sikubaliani na mtazamo wako, mbona huisemei tbc ambayo ni ya Taifa lakini utafikiri ni ya CCM. Itv ni msema kweli na ni chaguo la wengi kwa Habari za uhakika.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.