Kuna stori ya Mhehe mmoja zamani wakati wa Mwalimu Nyerere akiitwa Mwamwindi Ismani huko Iringa aliua sijui RC au DC yule Kleruu sababu ya kuaibishana au kuleteana dharau eti sababu tu ya ukubwa na madaraka.
Kama hili halitarekebishwa basi mfano unakuja.
Mkuu nakuelewa vyema kuna Sanaa na Sanaa, hizi za asili za kwetu sijui kama tumefikia wasaani nguli kwenye fani hiyo kuwa na ulazima wa kujua teknolojia za kisasa maana ubunifu wao hautegemee teknolojia. Nakuelewa sana Mkuu. Ila upande mwingine tudumishe Sanaa ie muziki wetu wa asili ambao ndio...
Kujua kutumia computer sio kigezo, sidhani utasema Marehemu Morris Nyunyusa ambae nina Imani hakuwa anajua kutumia computer au hata kama alikuwa na elimu hii ya kisasa, basi hakuwa msanii Gwiji!!! Hivyo naweza sema Marehemu Dr Hukwe Zawose, Marehemu Mwinamila na magwiji wengine wa Sanaa.
Naapa mabadiriko nayataka!!!! Lakini sio kwa kuongozwa na Lissu, hana kanuni na hii ya kudhani kuwapendeza Wazungu na kujitia maneno ya kashfa na kejeli dhidi ya Baba wa Taifa, nasema hata kama atashinda na kuchukua dola tutakuja zungumza mengine. Sio mkweli, tunza haya!!
Naona nivute subira...
WaTanzania hebu tuache huu upuuzi wa kuhusisha kujua lugha ya Kiingereza kama kigezo cha uelewa wa mtu…!!! Ni ushamba na ndio haswa tafsiri ya Utumwa. Inasikitisha sana kama mpaka karne hii bado tunajadili hili. Tunashindwa hata kujifunza kwa jamii za watu wengine waliopiga hatua kubwa sana...
Hili la kwenda nje na kuongea vibaya kuhusu Taifa letu sio siri limesumbua wengi hata wale tulio na hasira sana na chama tawala. Ina maana L alikuwa hajui analofanya au....? Na kuna lile la kumtukana na kumshutumu Baba wa Taifa!!!
Ngumu sana…….
Nakubaliana na wewe kuwa Marehemu Mabera ndio aliemleta Bitchuka Nuta. Sawa kabisa!!! Nuta pia kulikuwa na kijana mwingine mpiga gitaa la Rhythm akiitwa Abdallah "Dulla" Omar ambaye kwenye nyimbo kadhaa utamsikia Bitchuka akimwita, hususan wimbo wa Mume Wangu utamsikia Bitchuka akisema ahsante...
Mkuu kama nimemwelewa alieleta uzi alikuwa anauliza wanafunzi wa kwanza kwenye kitivo cha sheria. Prof Banyikwa (RIP) hakusoma sheria alikuwa wa Elimu Mimea (Botany). Au labda sio huyo...
Shukurani
Mtunzi na mpiga gitaa la solo mahili sana Mabera!!!! Mungu amlaze pema. Amefariki akiwa na umri gani? Tangu Enzi za Nuta Jazz nyimbo kama Nidhamu ya Kazi, Mpenzi Zarina, Nisingekukimbia Mpenzi na vibao vingine vingi Enzi hizo tutamkumbuka sana Said Mabera na wengine waliotangulia mbele za haki...
Ahsante sana kwa hii…..tuhimize tu maandiko yake yachapishwe ili yawafikie wengi na mitizamo yake ije ichangie kwenye kujenga fikira kwa kizazi kijacho cha Waafrika. Professa Wamba alikuwa kati ya wasomi wenye mitizamo asilia ya kiafrika itakuwa hasara sana kama fikira zake zitapotea pasipo...
Francis Da Don
Kabisa Aisee yaani ilikuwa kama kusema "mi naweza saini mikataba hiyo lakini kuna kizingiti, tukitoa hicho itakuwa poa sana"
Na baada ya kizingiti kutoka, kweli ikawa!!! Kutoka hapo Shamba la Bibi.
Tanzania itakuja siku watu watabidi wajibu maswali magumu sana hata kama watakuwa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.