TANZIA Mwanamuziki mkongwe, Said Mabera afariki dunia

Mtunzi na mpiga gitaa la solo mahili sana Mabera!!!! Mungu amlaze pema. Amefariki akiwa na umri gani? Tangu Enzi za Nuta Jazz nyimbo kama Nidhamu ya Kazi, Mpenzi Zarina, Nisingekukimbia Mpenzi na vibao vingine vingi Enzi hizo tutamkumbuka sana Said Mabera na wengine waliotangulia mbele za haki.
Pole sana kwa familia na taasisi na bendi ya Msondo Ngoma.
 
Gwiji wa muziki wa dansi na Kiongozi wa bendi ya Msondo Ngoma, Saidi Mabera amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumanne Septemba 29, baada ya kuugua kwa zaidi ya miezi miwili. Mazishi yatafanyika leo saa 10 jioni nyumbani kwake Goba.

Msiba upo Nyumbani kwake Tegeta A maeneo ya Goba jijini Dar es Salaam.

===
SAID MABERA WA MSONDO NGOMA AFARIKI DUNIA

GWIJI wa ukung'utaji gitaa la solo hapa nchini na kiongozi wa bendi ya Msondo Ngoma, Said Mabera amefariki dunia jana saa 6 za usiku.

Mabera ambaye ameitumikia Msondo Ngoma tangu mwaka 1973 bila kuhama hata mara moja, amefariki baada ya kuugua kwa zaidi ya miezi miwili.

Mtoto wa marehemu, Mabera Said amesema kuwa msiba uko nyumbani kwao Goba jijini Dar es Salaam na mazishi yatafanyika leo saa 10 alasiri huko huko Goba.

RIP SAID MABELA
 
Upumzike kwa Amani Ndugu Yetu
Hakika mlitupa burudani na muziki wa Msondo Ngoma
"...... hapa nilipofika inatosha nisijefuga ugonjwa nikakosa dawa.... Maringo Binti Maringo......
Zilipendwa kitambo sana
Mungu akurehemu!
 
Gwiji wa muziki wa dansi na Kiongozi wa bendi ya Msondo Ngoma, Saidi Mabera amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumanne Septemba 29, baada ya kuugua kwa zaidi ya miezi miwili. Mazishi yatafanyika leo saa 10 jioni nyumbani kwake Goba.

Msiba upo Nyumbani kwake Tegeta A maeneo ya Goba jijini Dar es Salaam.

===
SAID MABERA WA MSONDO NGOMA AFARIKI DUNIA

GWIJI wa ukung'utaji gitaa la solo hapa nchini na kiongozi wa bendi ya Msondo Ngoma, Said Mabera amefariki dunia jana saa 6 za usiku.

Mabera ambaye ameitumikia Msondo Ngoma tangu mwaka 1973 bila kuhama hata mara moja, amefariki baada ya kuugua kwa zaidi ya miezi miwili.

Mtoto wa marehemu, Mabera Said amesema kuwa msiba uko nyumbani kwao Goba jijini Dar es Salaam na mazishi yatafanyika leo saa 10 alasiri huko huko Goba.
R.I.P
 
Nitakwenda na naani msondo ngooma, nitacheza na nani magoma kitakita.
Kalale mahali pema .
Athumani Momba,
Selemani Mbwembwe,
Maina,
TX Moshi William,
Muhidin Maalim Ngurumo na leo
Said Mabera.
Inatia uchungu sana.
 
Malizia na Isiaka Kibene.
Nitakwenda na naani msondo ngooma, nitacheza na nani magoma kitakita.
Kalale mahali pema .
Athumani Momba,
Selemani Mbwembwe,
Maina,
TX Moshi William,
Muhidin Maalim Ngurumo na leo
Said Mabera.
 
Miongoni mwa binadamu mlioletwa duniani kwa kusudi la kutoa huduma.
Hukupenda kunyenyekewa bali mwenyewe ulikuwa myenyekevu.
Ulikuja duniani kwa lengo la kuburudisha waliochoka na walio na msongo wa mawazo, lakini ukajipa wajibu mwingine wa kuonya, kufundisha na kutahadharisha.
Nenda Mabera, nenda baada ya kutekeleza vema ulichojaliwa na Mungu. Wafuate wenzio waliozitendea haki karama zao za burudani;
Gerry Nashon "Dudumizi",
Hemed Manet " Chiriku",
Moshi William "Tx"
Mbaraka Mwinshehe,
Abdalla Gama,
Remmy Ongalla "Dr"
Mohamed Kipande,
Abdalla Mgonahazelu,
Muhidin Ngurumo "Maalimu"
Seleman Mbwembwe,
Athman Momba,
 
Mtunzi na mpiga gitaa la solo mahili sana Mabera!!!! Mungu amlaze pema. Amefariki akiwa na umri gani? Tangu Enzi za Nuta Jazz nyimbo kama Nidhamu ya Kazi, Mpenzi Zarina, Nisingekukimbia Mpenzi na vibao vingine vingi Enzi hizo tutamkumbuka sana Said Mabera na wengine waliotangulia mbele za haki.
Pole sana kwa familia na taasisi na bendi ya Msondo Ngoma.

Mebera ndiye aliyemleta Hassan Rehan Bitchuka kweye band ya NUTA wakati huo Bitchuka alikuwa bado mdogo sana kiumri na wote wakawa wanamwita "bwana mdogo"
 
Back
Top Bottom