Wapo wanaothubutu kufanya hivyo -kuchimba visima, kuweka hayo matenki nk, lakini hao hao serikali na hayo mamlaka ya mabonde huwajia kuwakamata, kuwatisha au kuwekea utaratibu mgumu sana.
Haya ni maajabu sana.
Kipindi kile cha kampeni kila kona wimbo ulikuwa mmoja tu "hana deni, hatumdai, katimiza yote,,mara mitano tena"
Leo hii ni vilio tu kila kona, kwani wale waliokuwa wakiimba nyimbo za "hana deni, katimiza yote....." wako wapi waje watuambie walikuwa wanamaanisha nini...
Hoja yangu ilikuwa kwamba ni rahisi sana kupata taarifa (idadi) za ndoa za kidini zilizofungwa au kuvunjika nchini kwa sababu ya mfumo wake wa urasimishaji na utunzaji wa taarifa na kumbukumbu zake ambao haupo au kama upo sio lazima kuzingatiwa kwa ndoa za kimila.
Ndiyo maana nikasema kwamba...
Mkuu naheshimu mawazo yako.
Lakini siyo kwamba hizi ndoa za dini zinaonekana nyingi kuvunjika kwa sababu ya mfumo unaotumika kuzirasimisha zinapofungwa au zinapovunjika kuwa na mchakato mrefu na uwazi mkubwa?
Ndoa nyingi za kimila zinafungwa hakuna mfumo wa lazima wa kurasimisha (kusajili nk)...
Utapeli katika kiwango cha juu sana hugharimu maisha ya watu.
Hivi kwa nini hao wanaoitisha makongamano hayo wasiwatembelee watu hao vijijini na kuwasaidia huko huko badala ya kuwaingiza kwenye gharama na mateso ya kuja mjini?
Hakuna raia anayetaka kiongozi aishi masikini.
Watu wanachukizwa na viongozi ambao huchukua fedha za wananchi kufanyia mambo yao binafsi badala ya kutumika kwa ajili ya ustawi wao.
Viongozi ambao huuwa raia wao ili waingie madarakani kwa manufaa yao kwa kuwapanga ndugu zao kwenye safu...
Kumbe na wao hudai haki kabla ya kuhukumiwa?
Je wale wanaowateka na kuwaumiza/kuwauwa/kuwapoteza kwa nini wanahukumiwa bila haki?
Leo wanadai haki, siyo amani. Kwa hiyo ni wazi bila haki hakuna amani.
Kijana anadai haki yake hawezi kuwa na amani kama atanyang'anywa haki yake. Tutende haki.
Inashangaza sana,
Kwenye kupanda bei kiwango kilikuwa kikubwa sana , yaani kutoka elfu 2 hadi elfu 4.
Kwenye kushuka sasa, kidogo kidogo sana, mwezi huu wanashusha kwa senti 2, kesho kwa shillingi 1....
Halafu kwa nini nchi kama Uganda bei ya mafuta kwao ni ndogo kuliko sisi? Upigaji.
Ni hadaa na giza tu, hakuna chochote cha maana.
Kwani tangu kuanzishwa kwake mpaka leo kuna chochote cha kujivunia kama taifa kwamba kimetoka na hii hadaa ya kinachoitwa mwenge wa uhuru? Hakuna.
Kuna siku hadaa hii itakoma na kupotea kabisa.
Eti kisa ni kinachoitwa mwenge wa uhuru?
Hivi huu mwenge sijui wa uhuru una uhalisia wowote katika kutatua yale yote yanayonasibishwa nayo (kuondoa umasikini, kuleta matumaini, sijui kuzuia rushwa)?
Ni miaka 60 sasa hii hadaa ya kinachoitwa mwenge wa uhuru ikifanywa lakini hakuna uhalisia...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.