Lakini alifanya mambo yaliyowafanya watanzania wenyewe wamsifie.
Hivi sasa hata wasanii wanapata shida kutunga nyimbo za kumsifia mama. sijui wanajistukia?
Kweli watu wanaodhani wana shida sana.
Kumbe Mke wake alikuwa naye anaumwa kiasi cha kushindwa kumuona mpenzi wake dakika za mwisho za uhai wake!
Sauti kubwa inasema hadi watoto wake walinyang'anywa simu.
Nadhani watoto pengine waliruhusiwa kumuona baba yao kwa sababu korona haikuzuia wapendwa...
Nadhani uwepo wa Janabi uliwafanya watu wahisi kuwa alikuwa na kazi maalum, hasa kutokana na kilichotokea baada ya kifo cha JPM. Yaani wale mzee Kinana kurudishwa ghafra kwenye uongozi wa chama na mtoto wa yule mzee mwenzake waliokuwa wakimtukana JPM kurudishiwa uwaziri na mtoto wa JK kuteuliwa...
Labda Mkapa na Mwinyi walinga mkono.
JK sidhani.
Lakini watu hutamani kiongozi fulani aendelee kutokana na utendaji wake unavyowagusa.
Mifano ni mingi
China ()Xi Jinping) Ujerumani (Angela merkel) Chadema (Freeman Mbowe) n.k
Kwamba Rais atatoka CCM hilo halina ubishi.
...ila tuwaombe tu kwa unyenyekevu CCM watupe mtu anayeeleweka
Tunahitaji Rais anayewaamini watanzania kuwa wanaweza, sio anayedhani wazungu au waarabu ndio wanaweza.
Hatutaki kurudishwa utumwani tena.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.