Usimfanyie mtoto haya kama unataka kuwa mzazi bora na sio bora mzazi

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,770
46,480
Usimlaze mtoto na wageni au ndugu wowote wa kiume ambao ni wakubwa kwake.

Usimtoboe masikio akiwa mdogo, muache aje kutoboa kwa hiari yake.

Usimfunge hirizi au kitovu mkononi, shingoni au kiuononi.Hiyo ni mizigo ya uchafu tu kwake, unaweza kuvaa wewe mzazi wake badala yake kama unazihusudu sana.

Usimlazimishe kwenda madrasa, msikitini au kanisani, akifikia umri wa kuchagua mwenyewe ataamua wapi pa kwenda.

Usimvalishe pia hijabu, kwa maeneo yenye joto kama Morogoro ni mateso makubwa sana.

Usimpake wanja mtoto mdogo anapendeza bila hayo makorokoro, kama ni kumkinga na jicho baya huo nao bado ni ushamba.Pia usimsuke nywele za kumtesa au kumnyoa viduku.

Usimuonjeshe pombe.

Akiwa anakataa kwenda shule au afurahii shule yake chunguza sababu ni zipi.

Usipende kuchapa mtoto msumbufu kuna watoto wenye matatizo ya Attention deficit hyperactivity disorder (ADHD), Dyslexia au autism

Usitumie viboko au vipigo kama njia kuu ya kumfundisha adabu au kutatua matatizo ya mtoto.Hii ikiwezekana acha nayo kabisa.
 
Mimi naona hata misosi pia tusiwape wakiamua wenyewe kula poa tu...
Na nguo pia kama vipi tangu anazaliwa unamuacha vilevile alivyokuja akikua ataamua mwenyewe avae au aliendeleze!..
 
kulala sawa mim mwneyew nipo against na mtoto kulala na yoyte yule awaye hata kama mdogo.na kuindoa hil we weka vitanda vya 3x6 .
kuhusu masuala ya din tena hapo wrong haupo sawa.mtoto mkunje angali mbichi.
hirizi nin sijui hayo mambo ya mila wachie wenyewe.
 
Kama hilo ni lazima kwako basi angalau usiwe unamlazimisha kwenda wakati ambapo hajisikii kwenda.
Najaribu kufikiria baba yangu angeniacha tu nifanye vitu mpaka "nitakapojisikia" je ningekua wapi leo hii

Kila nikifikiria hilo na njia nilizopitia nikanyooshwa na yule mzee basis na mwanangu atanyooshwa tu mpaka atakapofika kujitambua ndo atachagua mwenyewe na kufanya vitu pale "anapojisikia"

Ila akiwa kwangu bado,mikononi mwangu atanyooshwa mpaka awe kama rula
 
Kumuogesha ni muhimu, hii ni kanuni ya afya.

Kumpeleka shule ni muhimu,kila mtoto anahitaji kupata elimu,tena bora. Kama hafurahi kwenda shule,hatua ya kwanza ni kichunguza sababu zipi.

Mtoto kukataa kula ni sababu za kisayansi kwa sababu binadamu kwa asili anapenda kula kupitiliza. Kufikiri kwamba unaweza kumlazimisha kula ni ujuha wa kushindwa kutatua changamoto.
Hata kumuogesha pia tusimuogeshe,nashule pia tusimpeleke atakuja kwenda mwenyewe akiamua,akilia pia asibembelezwe,na akiikataa kula asiwe analazimishwa atakuja kula akiamua mwenyewe,Happ vipi mdau??
 
Back
Top Bottom