Nataka kuchepuka, njooni mnishauri

Mamy K

JF-Expert Member
Apr 30, 2017
2,868
9,919
Habari za mchana.

Mrejee kichwa cha habari tajwa, kuna mkaka hapa mtaani nimemuelewa, na yeye amenielewa ila yeye ni mume wa mtu na mimi ni mke wa mtu.

Jamani nipo kwenye ndoa huu mwaka wa 8 sijawahi kuchepuka, ila naona sasa shetani anaelekea kunizidi nguvu. Hebu nishaurini wale mlowahi kuchepuka....nipeni uzoefu.

Wababa wachepukaji karibuni pia kwa ushauri
 
Sikia mke wa mtu usitutafutie sababu ukatupa dhambi kwa kushiriki uzinzi wako,iko hivi wanawake sisi hatuchepuki kwa kuamua asili yetu sisi siyo wahuni kama jinsia pinzani,tunachepuka kutokana na sababu na kufanya lile tendo huwa ni hisia zaidi hapo ina maana kuwa wewe mapenzi na hisia kwa mumewe yamepungua yamehamia kwa mume wa mtu,najua hawa wenzetu wana maudhi sana kuna vitu vitakuwa vimesababisha mpaka kufikia hapo,unachotakiwa kufanya nendeni sehemu rudieni honeymoon mpendwa nendeni hata pale saadani kuna beach na wanyama ongeeni kaenjoy mkimaliza jifungieni garagaleni chumbani kama vile siku za kwanza mlivyoanzana hakika upendo utarudi tu au kama kuna vitu kapunguza muambie au kama kakukera kuambie nauhakika ipo sababu iliyokufanya ukawaze hayo.
Kwa huyo mume wa mtu mchepuko wako mpotezeee block kila mahali usimpe nafasi wala sababu ya kukusogelea niamini anataka akufunue mcheze tu mchezo wa kikubwa hana upendo na wewe hata kumbuka hawa wenzetu kungonoka kwao ni kamchezo tu yaani kamchezo tu karahisi sana hakahitaji chochote tofauti na wewe utahatarisha ndoa yako na mapenzi yako.
Mimi nimekusaidia tu kukuelewesha pia upunguze idadi ya tusiooolewa maana naona kabisa unajichimbia kaburi
 
Hakuna cha ajabu utakachokutana nacho Zaidi ya kujishushia heshima kwa uliyetembea nae na kwa mumeo akijua.


Kutembea nje ya ndoa kwa mwanamke naamini ni kumdhalilisha mumeo. Yule ulitembea nae hatamuheshimu mumeo hata mara moja.

Na utamfanya mumeo ajione si lolote mbele ya jamii. Tujaribu kuwapa heshima zao wanaotupa heshima ya kuwa wake zao.
 
Back
Top Bottom