JS
JF-Expert Member
- Sep 29, 2009
- 2,064
- 499
Shauri yenu, Geoff hayuko mbali. Tutadumisha MILA na nyie! Jaribuni muone!
Mila ipi hiyo wewe??acha maneno yako bana tuanze na wewe
Shauri yenu, Geoff hayuko mbali. Tutadumisha MILA na nyie! Jaribuni muone!
kwa nini machale yanakucheza????
kule ukienda lazima hiyo mboga ule even wizaut yua nolegi mzee!!!
Nimemkumbuka MC Lema! Mdumisha mila mwenzetu! We JS Huna wivu wewe?Mila ipi hiyo wewe??acha maneno yako bana tuanze na wewe
Kuku wangu mwenyewe manati ya nini?
Hahaha! Kesi ya mbuzi hakimu simba mwenye njaa ya siku nne?Unaona ulivyo mchokozi nani kuku wako? nakusemea kwa BHT sasa hivi......
Hahaha! Kesi ya mbuzi hakimu simba mwenye njaa ya siku nne?
where is ZD???? jeuri yako ya kuapproach ni wakati yeye hayupo tu akiwepo hapa unaufyata!!!
tumekutetea kakupunguzia kazi za nyumbani sasa unaleta jeuri si ndio eeeeh!!! endelea sasa uone vile ntanareti nikirudi home leo!!!
tunashukuru pia Annina kwa hiyo utapunguza wivu au??Nawashukuru wote kwa mawazo mazuri. Mniwie radhi sikuwa hewani wakati mnachangia. Kwa wale wanaouliza jinsia mimi ni She.
Nilitegemea kupata mawazo tofauti tofauti, sikuwa na aina ya ushauri nilioutegemea kutoka kwenu, vinginevyo kusingekuwa na haja ya kuomba ushauri! Once again, nawashukuru sana sana
Annina
Mwenzenu yuko matenite livu nyie mnachonga tu! Mmesahau alikuwa anatema mate hovyo majuzi kati hapa?
Matarajio yake yalikuwa nini? Apewe mbinu za kuongeza wivu siyo?
Apunguze au aongeze? Ongeza mwayego!tunashukuru pia Annina kwa hiyo utapunguza wivu au??
tunashukuru pia Annina kwa hiyo utapunguza wivu au??
Wapendwa,
Nipo kwenye serious mahusiano na kwa mapenzi ya Mungu tunaweza kufunga ndoa. Tatizo nina wivu kupita maelezo, yaani saa zote nahisi kuibiwa...kwa mfano kuna siku nilikuta amempa lift zilipendwa wake na alikuwa amekaa kwenye siti ya mbele ya abiria, niliumia kupitiliza nikaacha kuitumia ile siti, kuanzia siku ile nikawa nakaa siti ya nyuma kama balozi! Baada ya muda akabadili gari -thanx God sasa nakalia siti yangu!
Nyumba anayoishi nimebadili karibu kila kitu kwani nahisi vina uhusiano na mpenzi wake aliyepita na vinaweza kumkumbusha waliyokuwa wakifanya - siwezi kuvumilia, nimembadili hata yeye - mavazi, perfume, sehemu za kutembelea nk nk yote hii ni kuhakikisha mimi ndio natawala mawazo yake na si vinginevyo, lengo ni kwamba kila kitu kinachomzunguka kiwe kinamkumbusha mimi! Akisafiri tunakesha kwa PC na simu... kuhakikisha yupo peke yake nitamtaka afanye mambo kadhaa ili nijiridhishe siibiwi... msg zikiingia kwenye simu yake mapigo ya moyo yanabadilika...huwa najitahidi kujizuia kusoma msg hizo lakini asiponiambia nani ametuma na kuniruhusu kusoma naweza kukosa usingizi siku kadhaa!
Jamani nisaidieni, ni mimi tu au na wengine wako hivi? Nina wasiwasi atachoka, kuna wakati naona namnyima uhuru, najaribu kujizuia lakini nashindwa, nifanyeje?
Annina
Ndo kusema hataki mwenzie accomunicate na mtu mwingine yeyote?
Pls Annina, note kwamba jamaa yako asipokuwa na marafiki wengine wa kuccomunicate nao ila wewe tu kila wakati mmegandanda mtachokana mapema sana, si unajua itafika kipindi hata hakuna jipya kati yenu coz you are not in touch with the outside world, yani kama huwa unawashangaa wale ambao wanaendesha gari wamechuniana njia nzima ndo hivi, kisa hamna cha kuongea, so take care mama, let him be free.
Achana na simu yake ila uwe unaichungulia kijanja mfano akienda kuoga hivi.Abiria chunga mzigo wako.Ila usimwonyeshe kuwa unamind saana mfano achana na kuuliza nani kamuandikia sms au kumpigia.wewe chunguza kiujanja asijue.Abiria chunga mzigo wakoAsante sana Carmel,
Nimefikiri juu ya hili pia wakati najifanyia self asssessment with regard to mahusiano niliyonayo, ndio maana nikasema nahisi namnyima uhuru. Sio kwamba hana marafiki, anao na anawasiliana nao -sina tatizo na hilo. Shida ni pale nisipoambiwa sms imetoka kwa nani na niruhusiwe kuisoma... cha ajabu si mara zote nasoma hizo sms baada ya kuruhusiwa - huwa naridhika kwa kuambiwa na kupata ruhusa tu!
Annina
Asante Chrispin,
Nimegundua nina tatizo, natafuta namna ya kujikwamua sio kuongeza - ndio maana naomba ushauri wenu. Binaadamu tuna mapungufu yetu, mimi nina wivu, wengine uongo, wizi, uzinzi, uchawi, fitina, ubahili nk nk. kujitambua ni hatua kubwa kama wengine walivyoniambia, hatua inayofuata ni kujitahidi kubadilika, hakuna aliyemkamilifu.
Wivu kupitiliza ni tatizo na linaweza kupunguza mapenzi - lakini hii haimaanishi ndio kitu pekee kinachoweza kupunguza mapenzi, tabia nyingine pia zina uzito sawa, sio kweli kwamba wote wanoachana sababu pekee ni wivu. Nakubali mapungufu na najitahidi kupunguza ili angalau nifike kwenye kiwango kinachovumilika...
Asante sana,
Annina