Abunwasi
JF-Expert Member
- Jun 25, 2009
- 5,486
- 3,468
Pole mwanangu
Wivu siyo kitu kibaya hata kidogo. Ila wivu wako wewe unatokana na obsession na insecurity. Lakini inaelekea mwenzako analiona hilo na ndiyo maana ana ridhia mabadiliko unayoyafanya na vilevile kukuridhia utakalo. Lakini ninaomba nikutahadharishe kuwa uelewe kuwa naye ni binaadamu hivyo uhakikishe ile kamba inayowaunganisha ni imara na wewe ndiye wa kuhakikisha inakuwa hivyo maana kamba hiyo [inayojumuisha mapenzi/urafiki/mwenza/msiri/ nk] haikatiki kwa kumfanyia vitu ambavyo vitakuwa kero kubwa kwake. Kwani ikifikia hapo ataanza kubadilika tabia na vitendo na wewe bila kujua utadhani amepata mwingine na utafanya mambo ambayo yatazidi kuweka umbali kati yenu na mwishowe hatima ya mapenzi kwisha na kasheshe na visa kuanza.
Wivu siyo kitu kibaya hata kidogo. Ila wivu wako wewe unatokana na obsession na insecurity. Lakini inaelekea mwenzako analiona hilo na ndiyo maana ana ridhia mabadiliko unayoyafanya na vilevile kukuridhia utakalo. Lakini ninaomba nikutahadharishe kuwa uelewe kuwa naye ni binaadamu hivyo uhakikishe ile kamba inayowaunganisha ni imara na wewe ndiye wa kuhakikisha inakuwa hivyo maana kamba hiyo [inayojumuisha mapenzi/urafiki/mwenza/msiri/ nk] haikatiki kwa kumfanyia vitu ambavyo vitakuwa kero kubwa kwake. Kwani ikifikia hapo ataanza kubadilika tabia na vitendo na wewe bila kujua utadhani amepata mwingine na utafanya mambo ambayo yatazidi kuweka umbali kati yenu na mwishowe hatima ya mapenzi kwisha na kasheshe na visa kuanza.