Mnyika, Zitto na Regia: Tupeni mchanganuo wa hela zinazolipwa kwa Mbunge ili tujue

Ubunge kama vilivyo vyeo vyote vya kisiasa nchi hii ni uwekezaji unaolipa sana. Hawawezi kusema wanalipwaje. Tunagharamia sana SIASA kwa kisingizio cha demokrasia. Ndio maana mimi nasema tupunguze ukubwa wa Bunge letu. Ni kubwa mno. Zanzibar ina Wabunge wawili kila jimbo ingawa mwingine anajiita mwakilishi. Hapa kwetu kuna Halmashauri/ Manispaa/ Miji ina wabunge zaidi ya wawili kwa vigezo vya kijinga kabisa vya Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Kuna VITI MAALUM vya akina Regia zaidi ya 150. Chaguzi zenyewe na hatimaye Bunge lenyewe ndio hilo!
 
Ina maana tumekosa cha kujadili mpaka tuanze kupiga majungu kuhusu kipato cha mbunge! Mnawashabulia akina Waheshimiwa toka CDM kwa mfumo wa CCM? Hata yakiwa Mabilioni huwezi kuyapunguza kwa kupitia JF. Kumbuka kuwa Kila kitu Tanzania kimefanywa siri, mwisho wa siku tunaumia wananchi kwa kuwalipa wawekezaji uchwara!

Kwa sasa anza KUIFANYIA KITU TANZANIA ili uje ukumbukwe daima maana mchawi wa yote ni CCM!

Usitupotezee na post za majungu, tunataka mlete mikakati ya kuwatoa madarakani CCM kabla ya 2015!

Anko Sam, kwa hiyo unashauri tujadili nini?

Kwa upeo wangu sina haja ya kuleta mikakati ya kuiondoa CCM. Nitakuwa tayari kuleta mikakati ya kuisaidia kata ya Mabogini ipige hatua kimaendeleo. CCM itaondoka yenyewe.

Angalizo langu; uwazi kwa wabunge wetu utajenga imani kwa wananchi. Suala sio inasaidia nini kujua bali inatuweka kwenye nafasi gani kujadili nini kifanyike. Ukubwa wa Bunge letu ni jambo la kujadiliwa pia. Gharama tunazaoingia kama nchi ni kubwa, sasa wewe kama busara zako zinakutuma kusubiri 2015 ni sawa. Hatufanani kimawazo. Mimi nahitaji kujua.
 
Hivi kama mtu anataka kuleta mabadiliko lakini anaogopa kusemwa na kamati ya maadili, hapo nasikia kizunguzungu naomba msaada
 
Sijaridhika na jibu la Regia na sioni kwanini mnakazana kumpa sifa......kama kweli wapo serious hawa watu kuna njia nyingi za kutuletea hizi taarifa.....kwa mfano humu ndani angeweza kuingia kama anonymous na angemwaga mambo...its just a matter of few minutes!!!!kuna mambo mengi nyeti yalishamwagwa humu na watu hatuwajui ila taarifa ilifika.....iweje leo hii inakuwa ishu ngeni???....Ninachoamini mimi siku zote maslahi binafsi yanatangulia then mambo mengine sijui maslahi ya nchi,umaskini nk .ila tatizo letu ni unafiki tu !Tutaongea yote lakini likifika suala la maslahi,mambo yote yanabadilika!!!Fikiria wewe mwenyewe labda ni mkurugenzi na mwajiri wako anataka kukuongeza mshahara hata maradufu ,ambayo ni wazi kutakuwa na gap kubwa na watu wa chini yako ...je utahoji kwanini imekuwa hivi na kususa ???hapa cha kwanza kichwani ni maisha yako na familia yako yatakavyokuwa then upuuzi mwingine!! TUACHE UNAFIKI, HAO HAWASEMI NG'O !!!!
 
Hivi kama mtu anataka kuleta mabadiliko lakini anaogopa kusemwa na kamati ya maadili, hapo nasikia kizunguzungu naomba msaada

Pesa Mzee. Pesa, hela, fedha, njuluku, uchache, vijisenti,......, kwenye hili hakuna mbunge wa CHADEMA wala CCM.
 
Pesa Mzee. Pesa, hela, fedha, njuluku, uchache, vijisenti,......, kwenye hili hakuna mbunge wa CHADEMA wala CCM.

Umenivunja mbavu mkuu. Unajua mimi hubaki hoi pale viongozi wetu wanapotoa sababu lainiiiii kwenye hoja ngumuuuu. Na pia pale sababu wanazozitoa zinakuwa na ukakasi wa kimantiki.

Hivi wabunge wa kamati ya maadili wakimsema Lema kwa kutoa siri ya mikopo ya magari maana yake ni nini? Lengo la Lema ni kuwaridhisha wabunge wenzake mafisadi au ni kupambana na dhuluma na ufisadi wenyewe? Kwa hiyo, which one is a noble cause, kuonekana mtiifu kwa wabunge wachache walafi mafisadi au kuokoa pesa hizo ili kuboresha maisha ya watanzania walio wengi?

Na sasa Regia anatuambia kwamba na yeye anaogopa kusemwa na wenzake.
 
Nadhani inajulikana kuwa posho ni kubwa na wanalipwa mara mbili wakati mwingine na iliwai kuongelewa katika bunge lililopita. Lakini what next baada ya kujua? Tutademand zipunguzwe? Je tutajuaje kuwa baada ya kupunguzwa zitaenda kwenye yale tuliyoyategemea? Maana kama PM anasema sitaki mashangingi linaletwa kwako analisusa linapelekwa kwa mwingine je amesaidia hapo? Hivyo hivyo posho hizi tunauhakika kuwa baada ya kupunguzwa zitaenda tulikotegemea?

Mimi nadhani kuwe na njia bora ya kupunguza matumizi ikiwemo chai iliyotengewa 20 billions ili hata wabunge wakikatwa tujue inakwenda wapi. Au iwekwe hadharani for the time being kuwa kila mbunge akatwe kiasi fulani kitumike kwenye kitu fualni au iwekwe motion bungeni hata hoja binafsi ya kureview hayo malipo ili hela hizo ziende kwenye vitu vya maendeleo. Maana kila mbunge akitoa Milion 1 tuna M 300 kwa mwezi, kwa mwaka 3.6 Bilion, hii inajenga madarasa kibao au hata barabara ya zaidi ya km 3 kiwango cha lami.(APPROXIMATE FIGURES)

ITAFUTWE JINSI YA KUPUNGUZWA TUNAJUA POSHO NI KUBWA SANA.
Umenikumbusha hivi zile pesa za EPA ziliporudishwa ziliperekwa wapi....
 
Pesa Mzee. Pesa, hela, fedha, njuluku, uchache, vijisenti,......, kwenye hili hakuna mbunge wa CHADEMA wala CCM.

Heri wewe umesema.

Pesa haina rangi, kabila, dini wala chama cha siasa, ni rahisi sana kuwalaumu akina Chenge, Rostam and Co lakini ni vigumu sana kujizuia pale mkawanyo usio sawa wa fedha za umma unapokunufaisha binafsi, Simshangaa Mnyika wala Regia wala hawa Wabunge vijana wa Chadema waliokuwa choka mbaya miezi michache iliyopita, wakati wao ni sasa.

Waliopo madaraka ni reflection ya wananchi wa Tanzania wa sasa, tunapigana sana na Watawala wetu pale wanapotuacha nje ya ulaji lakini tunasherehekea na kuzifurahia taratibu zao mbovu pale zinapotunufaisha sisi na familia zetu ata kama maslahi ya wananchi walio wengi hayakuzingatiwa.

Mwisho wa siku usiweke tumaini kubwa sana kwa wanasiasa, si January wala Mnyika...si Lowasa wala Mbowe....si Sugu wala Komba....si Lyatonga wala Slaa.....wanafanana!!

................Maslahi Binafsi Kwanza...................
 
Pengine la kujiuliza hapa ni kuwa hivi kweli UBUNGE ungegombewa namna hii kama mpira wa kona kama sio mapesa haya na uwaziri?
 
Labda ni mimi sijui wakuu...

Hivi Mbunge anafanya kazi gani nzito kumzidi Mkuu wa shule ya seko?...kwa kuangalia Mkuu wa seko ana wajibu mzito sana kulinganisha na Mbunge!...mbaya zaidi ni kwamba wengine ndio wanapata nafasi nzuri ya kusinzia mule ndani ya mjengo!

Au title ya "kuwakilisha jimbo" inaonekana nzito sana..mbona hata hivyo hatuwaoni majimboni?...au niile kugonga yale madawati kukubaliana na hoja?...ni kazi gani ya ziada wanafanya inayostahili kulipwa hela nyingi hivi na fringe benefits za kuudhi?

Ningepata POWERS leo hii Mbunge anapata mwisho wa mwezi mshahara sawa na wa AfisaElimu(W)...basi!

Naomba nisaidiwe hizo kazi, maana nahisi kupungukiwa ufahamu!

acha matusi wewe, mbunge anakazi kubwa kuliko mwalimu wa secondary......usimfananishe mkulima na daktari....sio tu kwa sababu mkulima anakaa kwenye jua siku nzima basi ndio mchapa kazi bora zaidi.

wabunge wanafanya maamuzi ambayo yana immediate effects kwa kila mwananchi.....si unaona DOWANS na mengineyo?
 
Pengine la kujiuliza hapa ni kuwa hivi kweli UBUNGE ungegombewa namna hii kama mpira wa kona kama sio mapesa haya na uwaziri?

Hili mbona sasa hivi liko wazi baada ya kikao hicho kilichopita mkuu. Waliokuwa na matumaini na wabunge wa chadema kwamba ni wakombozi, andika maumivu (ingawa bado kuna wachaaache sana ambao nasubiri niwapime tena kwenye vikao vijavyo)
 
JFwhere we dare talk openly!
Naona wanapata kigugumizi, watch this space tutaweka hapa mchanganuo wa marupurupu yao na wakileta za kuleta tunabandika na list ya wale wa 'posho mbili' bunge kililopita.
 
Hili mbona sasa hivi liko wazi baada ya kikao hicho kilichopita mkuu. Waliokuwa na matumaini na wabunge wa chadema kwamba ni wakombozi, andika maumivu (ingawa bado kuna wachaaache sana ambao nasubiri niwapime tena kwenye vikao vijavyo)
Tutazibadili vipi SIASA za NCHI yetu zisiwe uwekezaji?
 
Msando.Heshima Mbele!How are you?

Nimeisoma sredi yako nimekupata,nimekuelewa.Kimsingi nakubaliana na hoja yako na uko sahihi kutaka kujua maslahi ya wabunge kwakuwa sisi ni wawakilishi wa wananchi.Lakini kwakuwa nchi yetu imejengwa kwa mgumo wa usiri katika mambo mengi na ndio maana utakuta hata mke hajui mshahara wa mumewe na wako kwenye ndoa zaidi ya miaka 50 na watoto nao hivyo hivyo hawajui kipato cha wazazi wao n.k.Kumekuwa na utamaduni wa watu kutokutaka kuweka wazi vipato vyao bila sababu za msingi.Binafsi huwa sielewi hasa kwanini iwe hivi.

Binafsi napenda sana kuweka wazi vyanzo vya mapato yangu na wakati nikiomba kura Kilombero niliweka wazi jumla ya mapato ya Mbunge kwa mwezi na kimsingi nilikuwa napingana na malipo haya.Hivi sasa nimekuwa Mbunge ninafungwa na Kanuni za Bunge za kutotoa siri za Bunge.Wakati tuko kwenye Semina Elekezi Ubungo Plaza tuliwekwa wazi kuhusu mapato ya Mbunge na Spika alisisitiza sana kuhusu usiri.Nilipata nafasi ya kuhoji kwanini kuwe na usiri katika mapato yetu sikupatiwa majibu ya kuridhisha,kimsingi hakuna hoja za msingi ila ni woga tu.Spika alisisitiza kwa yeyote atakayetoa siri atawajibishwa na Kamati ya Maadili.Lema aliweka wazi kuhusu mikopo ya Magari ya Shilingi milioni 90 analaumiwa sana including baadhi ya Wabunge wa CHADEMA.Kwa bahati mbaya sana sina ID nyingine humu JF zaidi ya hii ya jina alangu halisi hivyo siwezi kuweka wazi hapa mbele ya kadamnasi na kwakufahamu fika kuwa humu wako members wakila aina including wabunge na viongozi wengine hivyo nisije nikachukuliwa hatua za kinidhamu unnecessarily.Ila tukiwa nje ya jukwaa hili nitaweka wazi kila kitu iwe kwako au kwa mwingine yeyote atakayehitaji.

Naamini umenielewa na tutawasiliana kwa njia nyingine.

Aluta Continua.
Kutoka Ofisi za Bunge Dsm
Regia E Mtema
Waziri Kivuli Kazi na Ajira.

Dada unaweza kutumia proxy katika kuwasilisha ili tuweze kufikia estimates au na hizo pia hamruhusiwi?

Kwa mfano kama utaeleza mbunge kutokana na perdiem yake anauwezo wa kulipia five star hotel bado akabakiwa na kiasi cha kununua begi lashilingi kadhaa na viazi debe kadhaa, nyanya, vitunguu, mbuzi kilo kadhaa pale kibaigwa kwaajili ya zwadi arudipo nyumbani ndo kipato chake cha per diem kwa siku moja kinaisha...na from there sisi tota deduce what is most likely kuwa kipato cha mbunge as far as the per diem is concerned; au kurahisisha ukaweka in lump sum alafu ukasema kwa mwezi mbunge anaweza kulipa mshahara wa agriculture officer wanne wa grade II for example for example kama ataamua kuinvest pesa zake zote zinazobaki baada ya kutoa matumizi ya kawaida ya mtanzania wa kima cha kati kwenye kilimo kwanza katika shamba ambalo tayari analo; vitu kama hivyo ili tu pate tu estimate kwaajili ya mjadala....Hope hapo utakuwa umeruka kihunzi cha kanuni za bunge lakini uwe tayari na kanuni za kuchukiwa na kuingia kwenye intrigue za wachumia tumbo hahaaaa!
 
Nguvu ya Umma, overhaul the entire system
Siku ya pili baada ya mabomu kule Gongo la Mboto watu kila rika na jinsia walikuwa bado wanakimbia. Nguvu ya Umma inataka ujasiri, uthubutu, nguvu, msimamo,...., Watanzania hawa wa Mwalimu? Sijui.
 
Tushaliwa. siku zote ikifika kwenye swala la maslahi, wabunge wote huungana. hutajua mpinzani ni nani wala mtawala ni nani, thats what money can do to people.
 
Sijaridhika na jibu la Regia na sioni kwanini mnakazana kumpa sifa......kama kweli wapo serious hawa watu kuna njia nyingi za kutuletea hizi taarifa.....kwa mfano humu ndani angeweza kuingia kama anonymous na angemwaga mambo...its just a matter of few minutes!!!!kuna mambo mengi nyeti yalishamwagwa humu na watu hatuwajui ila taarifa ilifika.....iweje leo hii inakuwa ishu ngeni???....Ninachoamini mimi siku zote maslahi binafsi yanatangulia then mambo mengine sijui maslahi ya nchi,umaskini nk .ila tatizo letu ni unafiki tu !Tutaongea yote lakini likifika suala la maslahi,mambo yote yanabadilika!!!Fikiria wewe mwenyewe labda ni mkurugenzi na mwajiri wako anataka kukuongeza mshahara hata maradufu ,ambayo ni wazi kutakuwa na gap kubwa na watu wa chini yako ...je utahoji kwanini imekuwa hivi na kususa ???hapa cha kwanza kichwani ni maisha yako na familia yako yatakavyokuwa then upuuzi mwingine!! TUACHE UNAFIKI, HAO HAWASEMI NG'O !!!!
nagonga thanks hapa tena. thanks.
 
watanzania wanaishi under a dollar a day.....wabunge wanaishi under a thousand dollars a day.....kaazi kweli kweli
 
acha matusi wewe, mbunge anakazi kubwa kuliko mwalimu wa secondary......usimfananishe mkulima na daktari....sio tu kwa sababu mkulima anakaa kwenye jua siku nzima basi ndio mchapa kazi bora zaidi.

wabunge wanafanya maamuzi ambayo yana immediate effects kwa kila mwananchi.....si unaona DOWANS na mengineyo?
Kiongozi,
Kweli mvuruga nchi ni mwananchi!

Unathubutu kusema kuwa maamuzi ya wabunge yana immediate effect kwa wananchi, so hiyo ndiyo bottom-line ya wao kulipwa mishahara hiyo na posho lukuki, na gari la 90M?...GOOOOSH...my nose!

Unaweza kunieleza ni maamuzi gani beneficial waliyoamua wabunge eg kwenye bunge la 9?...can you mention any two?...any decision kuhusu kodi?...bei za mbolea?...mafuta ya petrol...elimu?...tiba?, plz tell me!
Unaposema immediate effect nitakuelewa tu kama unamaanisha immediate NEGATIVE effect, lakini si tofauti na hivyo!
Sasa je ni kwasababu hiyo unataka walipwe in that lavish manner?....
 
Back
Top Bottom