Mnyika, Zitto na Regia: Tupeni mchanganuo wa hela zinazolipwa kwa Mbunge ili tujue

Ukweli upo wazi,mnalipwa pesa nyingi sana kulinganisha na kazi mnayowafanyia wananchi.
 
Mheshimiwa Regia,

Nakushukuru sana kwa maelezo yako mazuri. Sikutaka kuingia kwa kina baada ya maelezo yako ya mwanzo kwa sababu kuu moja, bado Zitto na Mnyika hwajajibu chochote ili tujue mawazo au maoni yao. Nimekuwa mgumu kuamini haraka haraka kwamba na wao wanaweza kuwa na mawazo au msimamo kama wako.

Kwa nini nimesubiri? Zitto ninayemjua mimi amekuwa mzoefu wa kufukuzwa na kuwajibishwa kila alipopita. Zitto alifukuzwa O'level akafukuzwa A'level na akafukuzwa Chuo Kikuu. Zitto alifukizwa/simamishwa Bungeni. Kufukuzwa kote huko ilikuwa ni kwa sababu alikuwa anasema ukweli na kupinga waziwazi yale aliyoyaamini. Bado nasubiri nione katika hili inakuwaje. Inawezekana sasa hivi approach yake ni tofauti lakini bado nitasubiri nilishuhudie hilo au alitolee maelezo. Ukimya wake kwa wengine unaweza ukaonekana kama ni woga au amebadilika. Sitakuwa mwepesi kuamini hivyo mpaka mwenyewe aseme au ukimya wake umaanishe hivyo.

Kuhus Mnyika na yeye natarajia atasema neno. Endapo hatasema ataelezea kwa nin hajasema neno katika hili. Namfahamu na wengi humu ndani wamemuona ni mtu wa aina gani. Suala la Kanuni kumbana sidhani kama linamsumbua sana. Angekuwa anajali kanuni na sheria asingenipokea mimi na Zitto tulipofukuzwa chuo mwaka 2003 na kutuhifadhi chumbani kwake almost wiki tatu. Angefuata kanuni na By Laws za Chuo. Pia asingeniafirisha usiku kutoka Morogoro mpaka Dar kukimbilia Mgomo mwaka 2004 huku akiwa kiongozi wa TYVA na YUNA kwani alivunja kanuni nyingi tu. Mbona hakuogopa kipindi hicho? Kwa nini aogope sasa hivi?

Tukirudi kwako wakati nasubiri bila kuchoka kuwasikia Zitto na Mnyika, je taarifa uliyoitoa kwa wananchi wako wa kilombero ilikuwa ni kwenye hadhara au uliwapa mmoja mmoja? Uliwatangazia wakati wa mchana kwenye mwanga au usiku? Najaribu kuangalia tofauti ya eneo la kutolea taarifa hiyo i.e kwenye jukwaa la siasa kwa maandishi na kwenye mkutano wa hadhara kwa maneno.

Kwenye JF hakuna ushahidi wowote ambao unaweza kupokelewa mahakamani au kwenye kamati ya maadili kuonyesha na kuthibitisha kwamba ni wewe umesema utakachosema. Ni nani atathibitisha ni wewe? Je kama nimechukua picha yako, nikaingia nayo humu ndani pamoja na jina lako nani atajua?? nani atapinga?? Mods watathibitisha vipi ni wewe?? Lakini bado siamini kwamba kipato cha Mbunge ni siri. Nikipata muda nitasoma kanuni za Bunge.

Ila ukisimama hadharani kila mtu anakuona, mashahidi watajitokeza, usalama wa taifa watakuona, waandishi watakupiga picha uthibitisho utakuwepo kwamba ni wewe umesema mbunge analipwa kiasi gani. Hapo unatakiwa uwe muoga zaidi.

Lakini, kwa sababu ninajua tutaonana au tutazungumza nje ya hapa naamini nitapata ufafanuzi zaidi. nitakuomba kama una nakala ya Kanuni za Bunge recent unitumie kwa email ili nizipitie na nitakuwa mshauri wako kuhusu masuala yote ya kanuni. Hii itasaidia kwa kiasi kikubwa kuhakikisha hazikufungi bila sababu.

Kwa sasa ninasubiri bila kuchoka kumsikia Zitto na Mnyika. Ukiwapata wafikishie salamu kwamba tunawasubiri humu.

Kila la kheri Mheshimiwa.

Msando nimekupata vyema.Nadhakin kina Mnyika wanaweza kuja kujibu kwani kila mmoja anamtazamo na misimamo yake.Wamechelewa may be kwasababu ya ubize,Zitto yuko Bagamoyo kwenye semina ya oversight commitees za Bunge nadhani akipata wasaa wakupita humu ataona na ataamunua la kufanya.Endelea kuvuta subira.Mnyika nae yawezekana bado hajapita humu nadhani atajibu na kwa ninavyomfahamu atasema neno.Mimi nimesimami msimamo wangu asa Regia.

Nadhani mimi na wewe hatjaelewana.Kwanini unataka iwe hapa kama lengo lako ni kujua?kwani ukimabiwa pembeni inakuwaje?Uko karibu na Lema,Zitto,Mnyika,Mbunge wako Ndesamburo na hata mimi unaweza kupata taarifa toka kwangu.

Kuhusu wananchi wa Kilombero nilisema kwenye mkutano wa hadhara mchana kweupe.Atleast Jimboni naweza nikajitetea wale niwapiga kura wangu wa moja kwa moja na nina uhakika nao.what abaout here,do i know them?nitajitetea nini kwamba nilikuwa namjibu Msando?Nikipewa adhabu yeyote kwaajili ya kuwaambia wapiga kura wangu ukweli niko tayari na siogopi hilo.Hpoja ya msingi hapa sio kuogopa adhabu,kwani sidhani kama mbunge anaweza kusimamishwa ama kufukuzwa kwaajili ya kusema mapato ya wabunge,hakuna adhabu itakayozidi kupewa onyo.Dont worry utajua tu ukweli.vuta subira.
 
Kipengele namba sita;Hutambui kuwa ukiwa kwenye public office you are accountable to the public?Sijui ni kivipi unafananisha ufahamu wa mume ama mke kuhusiana na mishahara yao vs wananchi kujua ni kiasi gani wanawalipa nyie kama viongozi wao?Ama ubunge ni private sector?

Mkuu nimetoa mfano mdogo tu kwamba kama kwenye ngazi ndogo ya familia tunashindwa kuwa wa wazi kwenye masuala ya fedha tena kwa familia yako sembuse kwa wananchi?Wenzetu nchi zilizoendelea wana uwzi mkubwa katika ngazi zote?charity begins at home.Ukinisoam vizuri utanielewa binafsi napinga usiri huu ndio maana wananchi wa Kilombero wanafahamu na hata mdada anayenisaidia kazi nyumbani anafahamu kama Mbunge ninalipwaje na hata kabla sijawa Mbunge alifahamu pia.Mimi sijasema hatulipwi pesa nyingi,nenda kasome comment yangu ya kwanza.N kweli Wabunge wanalipwa vizuri na ndio maana kila mtu anataka kuwa Mbunge hata kwa njia zilizo haramu.Ubunge tanzania ni kitega uchumi.Kuna fursa nyingi sana kwenye Ubunge,hivi hamshangai mtu miaka nenda rudi Mbunge na wala hawataki kaucha mpaka mfumo uwateme?
 
Mh.Regia umeshaelezea sana sasa hii hoja kiasi naona unaanza kurudia kila point uliyoongea awali, huenda pia umechoka!
Mi nashauri wenzangu, kwa hatua hii hakuna jipya tunaloweza kujazilizia hapa kabla ya kujua maslahi hayo yanaonekanaje...
Otherwise this is gonna be asking too much from Regia, ambapo mnaona wazi kuwa wenzake wapo bize, au wamesepa hoja!...At least we should appreciate that she has been hand to hand with us on this matter, naamini in no time doc itakuwa kwenye miliki yetu as JF!
 
Regia, kwa sasa nitasema nimekuelewa. Sitasema nimekuelewa nini.

Jambo moja, kuchagua kwangu Zitto, Mnyika na Wewe sio kwa sababu ya ukaribu ni kwa sababu nawaamini. Wabunge wako wengi wa CDM niko nao karibu lakini mimi binafsi katika hili nawaamini ninyi zaidi. Hii ni kwa sababu simuoni mbunge mwingine yeyote humu jamvini zaidi yako na Mnyika kwa sasa. Sijasoma post ya Mbunge yeyote mwingine zaidi yenu kwa hiyo ninyi ndio wawakilishi wetu tunaowaamini kwani tunawajua na kuwaona. Tunazungumza nanyi.

Kuhusu 'wapiga kura' wako kwa uelewa wangu tafsiri ya CDM na CCM Wabunge wa Viti Maalumu ni wabunge wa 'nchi' nzima. Mimi naipinga na nitaipinga mahakamani very soon. Nakubali Mbunge wa Viti Maalumu ni kwa ajili ya pale alipoteuliwa (nominated) na sio popote anapopangiwa na chama chake. Kwa hiyo uko sahihi kwamba u r more responsible to kilombero residents then we follow after them.
 
Mkuu nimetoa mfano mdogo tu kwamba kama kwenye ngazi ndogo ya familia tunashindwa kuwa wa wazi kwenye masuala ya fedha tena kwa familia yako sembuse kwa wananchi?Wenzetu nchi zilizoendelea wana uwzi mkubwa katika ngazi zote?charity begins at home.Ukinisoam vizuri utanielewa binafsi napinga usiri huu ndio maana wananchi wa Kilombero wanafahamu na hata mdada anayenisaidia kazi nyumbani anafahamu kama Mbunge ninalipwaje na hata kabla sijawa Mbunge alifahamu pia.Mimi sijasema hatulipwi pesa nyingi,nenda kasome comment yangu ya kwanza.N kweli Wabunge wanalipwa vizuri na ndio maana kila mtu anataka kuwa Mbunge hata kwa njia zilizo haramu.Ubunge tanzania ni kitega uchumi.Kuna fursa nyingi sana kwenye Ubunge,hivi hamshangai mtu miaka nenda rudi Mbunge na wala hawataki kaucha mpaka mfumo uwateme?
Tanzania naisikitikia sana,juzi tu waziri mkuu ameenda kanisani kuhutubia kuwa ufisadi upo hadi kanisani as if kanisa lina uhusiano wowote ule na serikali,ama ufisadi wa serikalini ndiyo ufisadi wa kanisani!Yani huyo ni waziri mkuu ambaye ndiye mtendaji mkuu wa serikali...!Badala ya kuja na data za kuwa wamefanya nini kuumaliza ufisadi ie hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa dhidi ya ufisadi na mafisadi wa Taifa,yeye anaenda kulia kulia kanisani...

Tuna tatizo kubwa sana watanzania....Ukitizama kiundani,Pinda ni kama anasema kila mtu ni fisadi kwa kutolea mfano kuwa ufisadi humo hadi kanisani nk,ni kama kuwaambia hao viongozi wa dini "mnapiga kelele za nini kuhusu ufisadi na wakati kuna ufisadi kanisani?"na inaonyesha wao kina Pinda hawaoni kama ufisadi upo ama kama ni tatizo pale inapokuaja kwenye maendeleo ya Taifa letu....

Pia hiyo haijustify kutokuwachukulia hatua mafisadi wa mali za umma...Same applies to this issue,ofisi mnazoshikilia ni public ones,mko accountable to the public,kwa hiyo kutoa kisingizio eti kwasababu familia hazielezani mishahara ie btn mke na mume ama mzazi na mwanawe,basi then ni sawa kwa wananchi kutoelezwa mishahara ya viongozi wao,hapo sikubaliani.

Kama kweli viongozi especially nyie wa upinzani mna uchungu kiukweli na Taifa hili,basi unafahamu hatua mnazoweza kuchukua ili kuwaondolea wananchi huu mzigo!Kumbuka wananchi ndiyo wamewaajiri,yani mwananchi ndiyo mwajiri wako na wewe kina Zitto na wengineo ni waajiriwa wa wananchi!Kama ilivyo kwa waziri mkuu ambaye alitakiwa aelewe kuwa kuna hatua za kuwachuklia mafisadi na si kusema eti ufisadi humo hadi makanisani,sasa dini na serikali wapi na wapi?Na hata kama upo kanisani kwani ina maana viongozi wa dini si wananchi wenye haki ya kuuliza kuhusu ufisadi wa serikali?Ni sawa na kuwambia mwananchi kuwa hata humo uraiani kuna ufisadi ama wizi na kwahivyo wanaosimamia mali za serikali nao wanaweza kuiba!hata humo kwenye institutions kama dini,kuna hatua za kuwachukulia mafisadi....Hata kwenye private institutions nk!

Na kwa upande wenu CDM,mnatakiwa muonyeshe utofauti kati yenu na ccm,mnapogombana just because kuna mwenye kuonyesha mapenzi ya kweli kwa wananchi(ie waliochukia hatua ya mbunge wa Arusha kuhusu 90 mil),then mnatufanya tujiulize maswali mengi sana.

Ofisi ya umma si mchezo ndugu zanguni,kama ni kweli mna nia ya kuwakomboa watanzania,ni lazima kwanza muanze kwa kubadili system na si kupiga kelele halafu mkishaingia ndani mnaona baadhi ya mambo kama haya ni sawa kwa vigezo vya "Semina elekezi"

Ama mishahara mnayolipwa na wananchi mnaona ni issue binafsi?
 
Ndugu zangu wanaJF. Salaam.
Nimesoma kila mchango kwenye sredi hii kwakuwa sredi hii inanihusu moja kwa moja.Ninaelewa hoja zenu na nina washukuru wote kabisa mlionielewa na msionielewa.Kuna mambo kadhaa naomba niyaweke sawa.
1.Kuna watu hapa baada ya kusoma post niliyorusha mmelaumu kwa kusema ninakwepa kusema ukweli.Kundi hili nadhani halikunielewa nilichosema,nimesema wazi kabisa nje ya jukwaa hili naweza kusema na nikampa fursa mrusha sredi anitafute kwa njia nyingine.Alberto ana access namimi kwa kiasi kikubwa tu angeweza kunipata na ningempa mchanganuo wote including access ya kiwango cha juu cha mkopo kwa Mbunge kwenye benk.

2. Kuna wengine wamesema nitumie au ningetumia ID ya siri na kuna wengine wamesema eti kutokuwa na ID nyingine ni danaganya toto lakini ukweli ni kwamba sina ID nyingine kwasababu zifuatazo ninaamini kabisa nikiwa na ID nyingine na nikawa na post sredi mbalimbali hapa ndani ya wiki mbili tu nitakuwa nimeshajulikana.Nilipokuwa natumia jina la siri enzi hizo kama Gender Sensitive kuna watu wengi tu walikuwa wameshafahamu GS ni nani.The problem niko muwazi sana na siwezi kujificha wala kupretend hivyo nitajisumbua tu kuwa na ID za siri,sioni sababu.Baada ya kuwa Mbunge kuna baadhi ya watu walinishauri niwe na hayo maID ya siri lakini nikaona nitakuwa mtumwa tu,kwnini nijifiche?namdanganya nani?naogopa nini?

3.Kuna watu hapa wanasema kuwa naogopa kuwajibishwa na Kamati ya Maadili inakuwaje naogopa kusemwa tu?ndugu zangu mnachukulia kuwa hili suala ni dogo sana,sio dogo kama mnavyodhani.Ninachokataa hapa nikuvunja kanuni kwenye forum kama hii.Nimesema wazi kuwa nje ya hapa sitaficha.

4.Kuna kitu nimejifunza hapa, kuna watu wanashangaa mimi kuogopa kuwajibishwa na kamati ya maadili lakini wengi wao wako na majina ya siri,kwanini mnajificha,manogopa nini?si angalau mimi niko na jina langu halisi na ninafahamu fika kwamba kila ninapopost kitu sio wote watakao kipokea positively,ninafahamu fika nitakumbana na changamoto mbalimbali but altleast siziogopi na ninaziface.Jamani tafakarini kwa kina.

5. Kuna watu hapa wamesema kuwa eti linapokja suala la fedha basi wote tunakuwa na sauti moja ndio maana sijasema mchanagnuo wa mapato ya Wabunge.Jamani hili si kweli.hivi mmetafakari kwa kina?hivi kwani nikisema hapa ndio hayo mapato ya wabunge yatasitishwa?kwani mjadala umeanza leo?kutosema kwangu hapa hakumaanishi kwamba eti nahofia mapato yangu la hasha.Mkumbuke maslahi ya wabunge yanaamuliwa kwa kiasi kikubwa na wabunge kupitia kamati husika then Rais ndio mwamuzi wa mwisho.Tunaweza kabisa kuja na hoja za msingi kabisa za kujipangia mapato manono kabisa na wananchi wakabaki kusononeka tu,everything can be justifiable.Hivi kuna mangapi humu tumeyajadili,je yametekelezeka?kiwapi kilio chetu cha DOWANS?Mijadala yetu humu imeiondoa DOWANS?jamani tuwe tunatafakari kwa kina,msituhukumu eti kwakuwa hatujasema posho zetu hapa basi hatufai.Tusem,tusiseme haitabadilisha.Tunafuata kanuni kwenye jukwaa kama hili.Nje ya hapa mimi sifichi ndio maana wananchi wangu wa Kilombero ambao walibahatika kuhudhuria kwenye mikutano yangu wanafahamu Mbunge wao ninalipwaje.

6. Napenda kufahamu hivi humu ni wangapi wake au waume zao au watoto wao au wazazi wenu wanafahamu mishahara yao?

7. Kuna watu humu wametoa mfano niliposimamia msimamo wangu kuhusu tofauti ya PHD na First Degrees,Bungeni ninalindwa na Kanuni za Bunge,ninaweza kukubali au kukataa mwongozo wa Spika kama nilichokisema ndicho ninachokiamini na ndivyo ilivyokuwa.Hapa siwezi kuikwepa Kanuni ya kutotoa siri za Bunge.

Aluta Continua
Regia E Mtema
Waziri Kivuli Kazi na Ajira


Aise hapo namba tano (5) kunazidi kunifanya nizidi kufikilia ule usemi nilio usema mwanzo "if you can't beat them join them" mana kwenye vitu vingine mtaandamana mpk kupigwa virugu ila kwenye mapato kila mtu kimya.

Siasa za bongo bana,yan kila mtu ni mchumia tumbo sijaona mtu wa kutuondolea umasikini wetu kwa roho ya dhati kwa sasa ktk hawa wanasiasa wote.... "Beautiful ones are not yet born"
 
Hivi wakuu tunapohoji haya maslahi wanayopata wabunge kwa sasa kwa maana ya posho, mishahara, mashangingi nk, tumesahau 'vita' kubwa iliyokuwepo majimboni, kuanzia kura za maoni za CCM, hata ndani ya vyama vingine, ili tu kupata nafasi 'ya kuwakilisha' wananchi?

Tumesahau mapema hivi kwamba nyumba ya hoja ya uwakilishi, kuna motive ya personal gain na hili halikwepeki hasa kwa umaskini wetu?

Kwa nini, kuna wabunge wamekuwa 'wawakilishi wa wananchi' kwa miaka na bado hawataki kujitoa hadi 'kwa nguvu ya umma'


Mi kwa maoni yangu hakuna tija wala tutakachopata kwa eti kujua tu wanapata kiasi gani...wote tunajua kuwa wanachopata kinawazidi wafanyakazi/watumishi wengi nchini...Dr. Slaa mwaka jana alikuwa anapinga wabunge kulipwa mshara wa 7M kwa mwezi licha ya stahili nyinginezo, na huku wabunge wakitaka ipande hadi ifike 12M.

Ambacho hatujui hapa ni nini hasa?
 
Kama kweli dhamira yenu ni kuweka hadharani siamini kama mnashindwa kufanya hivyo. Kuna siri za Taifa ambazo huwa zinavuja na kufika kwenye Workstation ya Dr. PhD Slaa. Na huwa anaziweka hadharani. Serikali ya JK huwa inaona ni bora mshahara na marupurupu yake utangazwe kuliko kutoboa siri nyingine za serikali. Sasa iweje posho iwe mgogoro?

Kama mnaona tabu kutaja hapa, mpeni hizo nondo Saed Kubenea azitoe kwenye gazeti lake la Mwanahalisi. Mafanikio ya Chadema kwenye uchaguzi uliopita mojawapo ilikuwa kujipambanua na kuonekana tofauti na CCM, hata Shibuda analitambua hilo, sasa kwa kuwa tumeingia mjengoni basi twaweza kufananishwa na wao. Safari bado ndefu sana, Dr. Slaa aliwahi hata kuthubutu kutangaza mshahara wake, sasa iweje posho? Shauri yenu, watanzania wanarekodi haya yote, utakapofika wakati wa uchaguzi tena msije huzunika kwa kushindwa kujibu maswali ya msingi.

Mpigie Invisible mpeni aweke hapa hayo mapato yenu kama mnaogopa kunyooshewa vidole na dikteta Makinda (Dkt. Makinda)
 
Kipengele namba sita;Hutambui kuwa ukiwa kwenye public office you are accountable to the public?Sijui ni kivipi unafananisha ufahamu wa mume ama mke kuhusiana na mishahara yao vs wananchi kujua ni kiasi gani wanawalipa nyie kama viongozi wao?Ama ubunge ni private sector?

Mkuu nimetoa mfano mdogo tu kwamba kama kwenye ngazi ndogo ya familia tunashindwa kuwa wa wazi kwenye masuala ya fedha tena kwa familia yako sembuse kwa wananchi?Wenzetu nchi zilizoendelea wana uwzi mkubwa katika ngazi zote?charity begins at home.Ukinisoam vizuri utanielewa binafsi napinga usiri huu ndio maana wananchi wa Kilombero wanafahamu na hata mdada anayenisaidia kazi nyumbani anafahamu kama Mbunge ninalipwaje na hata kabla sijawa Mbunge alifahamu pia.Mimi sijasema hatulipwi pesa nyingi,nenda kasome comment yangu ya kwanza.N kweli Wabunge wanalipwa vizuri na ndio maana kila mtu anataka kuwa Mbunge hata kwa njia zilizo haramu.Ubunge tanzania ni kitega uchumi.Kuna fursa nyingi sana kwenye Ubunge,hivi hamshangai mtu miaka nenda rudi Mbunge na wala hawataki kaucha mpaka mfumo uwateme?

Mh Mtema,
Hivi ni vitu viwili usivyoweza kufananisha. Ni kama unalinganisha maembe na machungwa. Ndoa ni mkataba. Hivyo kama wao wenyewe wameamua kuishi bila kujua mishahara yao...ni haki yao.
Lakini serikali ni lazima kuniongoza mimi. Kwangu mimi NI LAZIMA KULIPA KODI serikalini. Na kukataa kulipa ni kosa la jinai. Sasa kwa nini mimi mwananchi nashindwa kujua ukweli wa matumizi ya hiyo pesa yangu.
Nimekuelewa kwa point zako nyingine. Na nina swali moja, je nikiomba uniambia, alafu nikazimwaga hapa jamvini, nitakuwa nimefanya kosa lolote? na penalty yake ni nini?

Tanzania naisikitikia sana,juzi tu waziri mkuu ameenda kanisani kuhutubia kuwa ufisadi upo hadi kanisani as if kanisa lina uhusiano wowote ule na serikali,ama ufisadi wa serikalini ndiyo ufisadi wa kanisani!Yani huyo ni waziri mkuu ambaye ndiye mtendaji mkuu wa serikali...!Badala ya kuja na data za kuwa wamefanya nini kuumaliza ufisadi ie hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa dhidi ya ufisadi na mafisadi wa Taifa,yeye anaenda kulia kulia kanisani...

Tuna tatizo kubwa sana watanzania....Ukitizama kiundani,Pinda ni kama anasema kila mtu ni fisadi kwa kutolea mfano kuwa ufisadi humo hadi kanisani nk,ni kama kuwaambia hao viongozi wa dini "mnapiga kelele za nini kuhusu ufisadi na wakati kuna ufisadi kanisani?"na inaonyesha wao kina Pinda hawaoni kama ufisadi upo ama kama ni tatizo pale inapokuaja kwenye maendeleo ya Taifa letu....

Pia hiyo haijustify kutokuwachukulia hatua mafisadi wa mali za umma...Same applies to this issue,ofisi mnazoshikilia ni public ones,mko accountable to the public,kwa hiyo kutoa kisingizio eti kwasababu familia hazielezani mishahara ie btn mke na mume ama mzazi na mwanawe,basi then ni sawa kwa wananchi kutoelezwa mishahara ya viongozi wao,hapo sikubaliani.

Kama kweli viongozi especially nyie wa upinzani mna uchungu kiukweli na Taifa hili,basi unafahamu hatua mnazoweza kuchukua ili kuwaondolea wananchi huu mzigo!Kumbuka wananchi ndiyo wamewaajiri,yani mwananchi ndiyo mwajiri wako na wewe kina Zitto na wengineo ni waajiriwa wa wananchi!Kama ilivyo kwa waziri mkuu ambaye alitakiwa aelewe kuwa kuna hatua za kuwachuklia mafisadi na si kusema eti ufisadi humo hadi makanisani,sasa dini na serikali wapi na wapi?Na hata kama upo kanisani kwani ina maana viongozi wa dini si wananchi wenye haki ya kuuliza kuhusu ufisadi wa serikali?Ni sawa na kuwambia mwananchi kuwa hata humo uraiani kuna ufisadi ama wizi na kwahivyo wanaosimamia mali za serikali nao wanaweza kuiba!hata humo kwenye institutions kama dini,kuna hatua za kuwachukulia mafisadi....Hata kwenye private institutions nk!

Na kwa upande wenu CDM,mnatakiwa muonyeshe utofauti kati yenu na ccm,mnapogombana just because kuna mwenye kuonyesha mapenzi ya kweli kwa wananchi(ie waliochukia hatua ya mbunge wa Arusha kuhusu 90 mil),then mnatufanya tujiulize maswali mengi sana.

Ofisi ya umma si mchezo ndugu zanguni,kama ni kweli mna nia ya kuwakomboa watanzania,ni lazima kwanza muanze kwa kubadili system na si kupiga kelele halafu mkishaingia ndani mnaona baadhi ya mambo kama haya ni sawa kwa vigezo vya "Semina elekezi"

Ama mishahara mnayolipwa na wananchi mnaona ni issue binafsi?

Mkuu....wewe kweli umeona mbali. Tungepata design yako kumi, Tanzania ingekuwa mbali mno. Big up...
 
Tungependa kujua mishahara ya Rais na viongozi wengine mbalimbali. Pia kama mnaweza kutuwekea zile level za mishahara za serikali. Tungefurahi mno.
Usiri ndo unajenga ufisadi. Leo hii tungeweza kumdadisi mtu kama Lowassa ambaye amefanya kazi serikalini miaka yote lakini ameweza ku-accumulate wealth kubwa ivyo.
 
Nadhani itakuwa vizuri pia tuwaombe wale wabunge 'wataalam wa kubadili kanuni za bunge' washinikize hizi kanunu za kinafiki za usiri zifutwe.. au kwa hizi wanakuwa vipofu hawazioni???
 
Mh. Regia
Naona umejitahidi sana kujibu hoja ..lakini huu mzigo ni mzito kwako sababu tatizo lililopo la kimfumo zaidi(kisiasa, kiuchumi,kijamii na kimaisha) na wewe huwezi kwenda kinyume na mfumo uliopo....jiangalieni nyie wapinzani ni wangapi kweli 'KWA DHATI' wanathubutu kwenda kinyume na mfumo linapofika suala la maslahi??? ona maprofesa ,madokta,matajiri nk wanavyohangaika kuupata ubunge au kuwa karibu tu na mbunge....naamini kabisa hampo pamoja katika hili...99% ni maslahi zaidi....mfano mdogo,ndani ya mfumo wa kijamii na kimaisha jamii inayotuzunguka ina matatizo kibao ambayo yanategemea mfumo mzuri wa kiuchumi ili kuyatatua,hii inapelekea mtu akishaukwaa ubunge kitu cha kwanza ni kujipanga upya kimaslahi na hata jamii inayomzunguka kukaa mkao wa kunufaika.Ndio maana huwa mnapongezwwa na ndugu ,jamaa,marafiki ,majirani nk wote hawa siyo bure ...(najua unajua ninachomaanisha).....Mwisho wa siku lazima mlinde maslahi yenu kwanza ,ndio mfumo unavyotaka.....bado tunaona sisi tunao wachangia hayo malipo/posho tuna haki ya kujua kwani information is knowledge and knowledge is power! Njia itakayotumika kufikisha ujumbe Its not an issue here!
 
Kweli linapofika suala la maslahi maji na mafuta vimechangamana .
, hiyo sheria ya kumhukumu mtu kutaja mshahara wake iko kwenye katiba ipi hapa MSANDO nisaidie
ila mimi nimejaribu kumchimba mbunge mmoja ameniambia kwa mwezi wanapata 12 . ikijumuisha mshahara wake , mshahara wa driver , mshahara wa msaidizi , mafuta lita 420 @ 2,500 , matengenezo ya gari na nyumba .
na kila kikao wanachohudhuria wanalipwa posho ya 150,000 kwa siku .
Regia wanawake sisi ni waungwana na wakweli na kwa sasa tunazidi kukimbilia sifa nyingine ya kujiamini ukifanya matendo yanayofanana na wanafiki haipendezi .
Dr Slaa mara zote alikuwa akitangaza mshara wake tokea wabunge walipokuwa wakilipwa 2.1 mpaka ilipofika 6 m na hatukuwahi kusikia akihukumiwa kwa kuwa hakuwa akisema wabunge wanalipwa bali alikuwa akisema mimi Slaa ninalipwa
Dada yangu mpenzi ni mapema mno kuacha kusimamia maslahi ya wananchi na kusimamia maslahi ya wabunge
 
Kweli linapofika suala la maslahi maji na mafuta vimechangamana .
, hiyo sheria ya kumhukumu mtu kutaja mshahara wake iko kwenye katiba ipi hapa MSANDO nisaidie
ila mimi nimejaribu kumchimba mbunge mmoja ameniambia kwa mwezi wanapata 12 . ikijumuisha mshahara wake , mshahara wa driver , mshahara wa msaidizi , mafuta lita 420 @ 2,500 , matengenezo ya gari na nyumba .
na kila kikao wanachohudhuria wanalipwa posho ya 150,000 kwa siku .
Regia wanawake sisi ni waungwana na wakweli na kwa sasa tunazidi kukimbilia sifa nyingine ya kujiamini ukifanya matendo yanayofanana na wanafiki haipendezi .
Dr Slaa mara zote alikuwa akitangaza mshara wake tokea wabunge walipokuwa wakilipwa 2.1 mpaka ilipofika 6 m na hatukuwahi kusikia akihukumiwa kwa kuwa hakuwa akisema wabunge wanalipwa bali alikuwa akisema mimi Slaa ninalipwa
Dada yangu mpenzi ni mapema mno kuacha kusimamia maslahi ya wananchi na kusimamia maslahi ya wabunge

Nimelazimika kujiuliza, je ni vipi sheria au kanuni inaweza kutungwa kukuzuia kusema unalipwa au unapokea nini kama Mbunge? Kanuni hii inasemaje? Mpaka sasa bado sijaipata hiyo kanuni inayosema 'ni marufuku kwa Mbunge kumwambia mtu yeyote kiasi cha mshahara anachokipokea' au 'ni marufuku kwa Mbunge kutaja hadharani kiasi cha fedha anachopokea kwa nafasi yake ya ubunge'. Bado sijakiona kipengele au kifungu hicho.

Mh. Mbunge yeyote aliyemo humu jamvini au mtendaji wa bunge yeyote naomba anipatie kanuni, kifungu au kipengele hicho. Vinginevyo bado nasubiri kama Waheshimiwa zitto na mnyika watachangia hii hoja. Au kama kuna Mbunge mwingine anayeweza kutujuza afanye hivyo.
 
haya wapenzi wa vyama vingi na vyama vyenu njooni mnywe chungu ya ukweli hapa! watu wakigoma kupiga kura mnajiuliza why?

hawaipendi CCM, lakini hawana imani na upinzani..kwishney!
 
Ukombozi wa kweli bado kupatakana!

Si Chadema, Ccm, Cuf, Tlp, Nccr wala Udp. Ifikapo kwenye masilahi yao, wote usahau kuwa sisi wananchi tuna tabu!
 
Nimelazimika kujiuliza, je ni vipi sheria au kanuni inaweza kutungwa kukuzuia kusema unalipwa au unapokea nini kama Mbunge? Kanuni hii inasemaje? Mpaka sasa bado sijaipata hiyo kanuni inayosema 'ni marufuku kwa Mbunge kumwambia mtu yeyote kiasi cha mshahara anachokipokea' au 'ni marufuku kwa Mbunge kutaja hadharani kiasi cha fedha anachopokea kwa nafasi yake ya ubunge'. Bado sijakiona kipengele au kifungu hicho.

Mh. Mbunge yeyote aliyemo humu jamvini au mtendaji wa bunge yeyote naomba anipatie kanuni, kifungu au kipengele hicho. Vinginevyo bado nasubiri kama Waheshimiwa zitto na mnyika watachangia hii hoja. Au kama kuna Mbunge mwingine anayeweza kutujuza afanye hivyo.

Regia atueleze ni kanuni namba ngapi, mimi nimeitafuta sijaiona. Na haya ni mambo ya transparency, kama mbunge hawezi kuwa transparent halafu eti kazi yake ni kusimamia serikali iwe transparent. What a contradiction? Kila huyu mama akijieleza mi nasikia kichefuchefu na kizunguzungu kwa pamoja.

Alishaambiwa kama kweli ana nia nzuri atengeneze ID nyingine amwage taarifa hapa.
 
Back
Top Bottom