Mnyika, Zitto na Regia: Tupeni mchanganuo wa hela zinazolipwa kwa Mbunge ili tujue

Msando.Heshima Mbele!How are you?

Nimeisoma sredi yako nimekupata,nimekuelewa.Kimsingi nakubaliana na hoja yako na uko sahihi kutaka kujua maslahi ya wabunge kwakuwa sisi ni wawakilishi wa wananchi.Lakini kwakuwa nchi yetu imejengwa kwa mgumo wa usiri katika mambo mengi na ndio maana utakuta hata mke hajui mshahara wa mumewe na wako kwenye ndoa zaidi ya miaka 50 na watoto nao hivyo hivyo hawajui kipato cha wazazi wao n.k.Kumekuwa na utamaduni wa watu kutokutaka kuweka wazi vipato vyao bila sababu za msingi.Binafsi huwa sielewi hasa kwanini iwe hivi.

Binafsi napenda sana kuweka wazi vyanzo vya mapato yangu na wakati nikiomba kura Kilombero niliweka wazi jumla ya mapato ya Mbunge kwa mwezi na kimsingi nilikuwa napingana na malipo haya.Hivi sasa nimekuwa Mbunge ninafungwa na Kanuni za Bunge za kutotoa siri za Bunge.Wakati tuko kwenye Semina Elekezi Ubungo Plaza tuliwekwa wazi kuhusu mapato ya Mbunge na Spika alisisitiza sana kuhusu usiri.Nilipata nafasi ya kuhoji kwanini kuwe na usiri katika mapato yetu sikupatiwa majibu ya kuridhisha,kimsingi hakuna hoja za msingi ila ni woga tu.Spika alisisitiza kwa yeyote atakayetoa siri atawajibishwa na Kamati ya Maadili.Lema aliweka wazi kuhusu mikopo ya Magari ya Shilingi milioni 90 analaumiwa sana including baadhi ya Wabunge wa CHADEMA.Kwa bahati mbaya sana sina ID nyingine humu JF zaidi ya hii ya jina alangu halisi hivyo siwezi kuweka wazi hapa mbele ya kadamnasi na kwakufahamu fika kuwa humu wako members wakila aina including wabunge na viongozi wengine hivyo nisije nikachukuliwa hatua za kinidhamu unnecessarily.Ila tukiwa nje ya jukwaa hili nitaweka wazi kila kitu iwe kwako au kwa mwingine yeyote atakayehitaji.

Naamini umenielewa na tutawasiliana kwa njia nyingine.

Aluta Continua.
Kutoka Ofisi za Bunge Dsm
Regia E Mtema
Waziri Kivuli Kazi na Ajira.

Regia,
Kwanza hongera kwa kujitokeza hapa. Umekuwa tofauti na wale wabunge wanaotumia blackberry na kuingia JF kila nusu saa lakini wameikacha thread hii muhimu.

Jibu lako linaonyesha ujasiri kwa sababu ni wazi kuwa na wewe utaingia kwenye kundi la kulaumiwa kama Mh. Lema. Anyway, hiyo ndio kazi ya kutumikia wananchi.

Katika jibu ulilitoa umedhihirisha kuwa hata wewe binafsi hauko tayari kufanya bidii ya kuhakikisha Mh. Diwani Msando anapata jibu la swali lake.
Sababu uliyotoa ya semina elekezi haina uzito, kwa sababu nchi inaendeshwa kwa sheria na sio kwa semina elekezi. Kama kuna sheria inayokukataza kufanya hivyo sote tutaiheshimu lakini sio wewe, wabunge wenzako na spika ku-connive katika kuhujumu wananchi.
Kumbuka Regia, uliposema uelewa wa watu wenye PhD Tanzania ni sawa na ule wa bachelor, spika alikupa "semina elekezi" kuwa ubadilishe msema wako; nilipenda sana jibu lako kwa spika - ulimwambia "mwa muono wangu mimi hivyo ndivyo ilivyo interms of thinking capacity". Kama uliweza kuikataa "semina elekezi" hadharani, ulishindwa vipi kuikataa semina elekezi za siri za Ubungo plaza?

Sababu nyingine uliyotoa kuwa huna ID nyingine nayo ni "danganya toto".ID za JF hazinunuliwi. Iwapo unaamini kuwa mh. Diwani anastahili kupata jibu la swali hili, unaweza kufungua ID nyingine au unaweza kumtumia PM.
Nakuomba umtumie Mh. Diwani PM ili yeye abebe barden ya kutujulisha wana JF wengine bila kusema kuwa wewe ndiye uliyemwambia, ili wabunge wanzako wasikulaumu, kwa sababu apparentlly lawama zao ni muhimu kuliko kulaumiwa na wananchi!

Kwa mara nyingine asante sana, tuendelee kuwatumikia watanzania.
 
hivi ukishayajua maposho ya wabunge then what?....
i mean utafanya maamuzi gani mkuu mrusha thread
 
Tunachohitaji ni uwazi kuhusu maslahi (kama yapo) anayopata Mbunge ili tufanye maamuzi sahihi.

Mheshimiwa Diwani, uamuzi upi huo? kupunguza kama ni mengi au kuongeza kama ni madogo au kuandaa maandamano ya kupinga maslahi makubwa/madogo ya wabunge?
 
Basi kwa kuwa Zitto ni mzoefu atawasaidia wenzake katika kutuletea huo mchanganuo wa posho na kadhalika nyingine

Amini nakwambia, Zitto hawezi kutoa mchanganuo huo. Subiri uone kama atatoa!
Mnyika, sina hakika. Lakini naye kama anabadilika hivi! Sijui, ngoja tuone.
 
hivi ukishayajua maposho ya wabunge then what?....
i mean utafanya maamuzi gani mkuu mrusha thread

Ki batani cha senksi kimechakachuliwa nakugongea hapa hapa mkuu

The Following 1 User Say Thank You to Carina TI For This Useful Post: Mjepu(now)
 
Mheshimiwa Regia kwa kuwa umetambua kwamba usiri wa kutokuweka wazi mapato yote ya mbunge kmsingi hakuna hoja ya msingi bali ni woga tu, basi tunakuomba ujipambanue wazi kwa kuziacha hizo siasa za woga na usiri usio na tija ili utuwekee wazi hapa jamvini mapato yote ya Mbunge.
naomba hivi kama mlipa kodi nchini ambaye nina haki ya kujua wawakilishi wetu bungeni wanapata kiasi gani na katika mchanganuo upi, ili niweze kujiridhisha kwamba kweli kazi wanayoifanya ndani na nje ya mjengo inastahiki au haistahiki kiasi wanachopata, na ili niweze kujua kwamba kweli mkate wa Taifa unagawiwa haki bin haki au wengine wanastahiki zaidi kwa kuwa wameshakuwa Waheshimiwa "KWA MUJIBU WA SHERIA".
 
Dada Regia umekuwa mkweli kuliko ukweli wenyewe, na huo ndo uungwana kwani ni sisi ndiyo tunalipa mishahara yenu. Natamani siku moja tufahamu kile mheshimiwa diwani alichoongea
 
Msando.Heshima Mbele!How are you?

Nimeisoma sredi yako nimekupata,nimekuelewa.Kimsingi nakubaliana na hoja yako na uko sahihi kutaka kujua maslahi ya wabunge kwakuwa sisi ni wawakilishi wa wananchi.Lakini kwakuwa nchi yetu imejengwa kwa mgumo wa usiri katika mambo mengi na ndio maana utakuta hata mke hajui mshahara wa mumewe na wako kwenye ndoa zaidi ya miaka 50 na watoto nao hivyo hivyo hawajui kipato cha wazazi wao n.k.Kumekuwa na utamaduni wa watu kutokutaka kuweka wazi vipato vyao bila sababu za msingi.Binafsi huwa sielewi hasa kwanini iwe hivi.

Binafsi napenda sana kuweka wazi vyanzo vya mapato yangu na wakati nikiomba kura Kilombero niliweka wazi jumla ya mapato ya Mbunge kwa mwezi na kimsingi nilikuwa napingana na malipo haya.Hivi sasa nimekuwa Mbunge ninafungwa na Kanuni za Bunge za kutotoa siri za Bunge.Wakati tuko kwenye Semina Elekezi Ubungo Plaza tuliwekwa wazi kuhusu mapato ya Mbunge na Spika alisisitiza sana kuhusu usiri.Nilipata nafasi ya kuhoji kwanini kuwe na usiri katika mapato yetu sikupatiwa majibu ya kuridhisha,kimsingi hakuna hoja za msingi ila ni woga tu.Spika alisisitiza kwa yeyote atakayetoa siri atawajibishwa na Kamati ya Maadili.Lema aliweka wazi kuhusu mikopo ya Magari ya Shilingi milioni 90 analaumiwa sana including baadhi ya Wabunge wa CHADEMA.Kwa bahati mbaya sana sina ID nyingine humu JF zaidi ya hii ya jina alangu halisi hivyo siwezi kuweka wazi hapa mbele ya kadamnasi na kwakufahamu fika kuwa humu wako members wakila aina including wabunge na viongozi wengine hivyo nisije nikachukuliwa hatua za kinidhamu unnecessarily.Ila tukiwa nje ya jukwaa hili nitaweka wazi kila kitu iwe kwako au kwa mwingine yeyote atakayehitaji.

Naamini umenielewa na tutawasiliana kwa njia nyingine.

Aluta Continua.
Kutoka Ofisi za Bunge Dsm
Regia E Mtema
Waziri Kivuli Kazi na Ajira.
Asante sana dada yangu kwa kuwa mkweli. Kumbuka dada yangu kuwa msema kweli ni mpenzi wa mungu. Nimekumbuka sana ulipokuwa SUA hasa kule mlimani kwamba inatakiwa kusema ukweli hata ikibidi kufa maana ukweli ndio utakao tawala. Naomba uendelee kutuwakilisha kwenye kile kikundi chetu kwa kusema ukweli daima. Mungu akubariki sana.
 
Msando


Thanx for this thread,

Nashangazwa sana na usiri unaosisitizwa katika posho na maslai yao kama wabunge.Hii inaonesha wazi kwamba kuna wizi unafanyika kwani ni mwizi tu anaweza kufanya kitu kwa usiri wa namna hivyo ..( hadi kutumia semina elekezi)

Kama mbunge anaweza kusema atatoa asilimia 20 ya mshahara wake kuhusu mfuko flani wakati huohuo hicho ambacho kitatozwa hiyo asilimia 20 kikawa siri inakuwa jambo la ajabu kabisa. Wanafanya siri mapato yao na mbaya zaidi mapato yao hayatozwi kodi pia. Na kwa sababu kodi ni kwa maendeleo ya nchi hivyo ni sahihi kabisa kusema kwamba Wabunge hawachangii chochote kwenye maendeleo ya nchi hii ( wanakwepeshwa kodi ).

Mwongozo wa spika unaotakiwa kuombwa kwa sasa ni " mbunge anatakiwa kuchukua hatua gani kama ataona kuna kanuni zinazowanyonya wananchi? '' hii itasaidia kubadilisha vipengele kandamizi katika kanini za bunge.Itasaidia mishahara ya wabunge kutokuwa siri tena,wabunge wataongea ! Na wabunge tunataka walipe kodi . Mwalimu mwenye mshahara chini ya laki 2 analipa kodi iweje mbunge asilipe?

This nationa can not prosper for so long if it only favours those in high offices.Madai na mwamko wowote wa kudai majibu ya maswali haya ya msingi tuyaunge mkono ili tuweze kujua kama hawa wawakilishi wetu ni moja ya wanyonyaji .
 
Ina maana tumekosa cha kujadili mpaka tuanze kupiga majungu kuhusu kipato cha mbunge! Mnawashabulia akina Waheshimiwa toka CDM kwa mfumo wa CCM? Hata yakiwa Mabilioni huwezi kuyapunguza kwa kupitia JF. Kumbuka kuwa Kila kitu Tanzania kimefanywa siri, mwisho wa siku tunaumia wananchi kwa kuwalipa wawekezaji uchwara!

Kwa sasa anza KUIFANYIA KITU TANZANIA ili uje ukumbukwe daima maana mchawi wa yote ni CCM!

Usitupotezee na post za majungu, tunataka mlete mikakati ya kuwatoa madarakani CCM kabla ya 2015!
 
Anayeonewa ni masikini yule anayepata kima cha chini cha mshahara, maana mshahara wake yeye hutajwa hadharani kila mishahara inapopanda.
Kwa nini tusianze kuwa fair kwa kuufanya mshahara wa kima cha chini nao uwe siri?
 
Msando Ablert!...unaheshimika mzee!

Majibu ndio haya, na obviously amejibu kama nilivyodokeza awali kwenye post yangu No 14 juu!
Japokuwa mheshimiwa ameweka wazi kwamba tuwe na subira, yatakuja wekwa hadharani tu siku moja kwa namna nyingineyo tofauti na hapa.
So currently we have to reserve our comments.
sio kweli hayo uyasemayo, kanuni haikufungi wewe ni Mbunge wa kuchaguliwa sio wa kugeiwa, tupeni mapato yenu umma ujuwe na tuone ufukuzwe bunge kwa sababu hiyo ila tutaamini kuwa nanyi ni walafi kama ccm hamna tafauti yoyote kati yenu na hao mafisadi, tupeni mapato yenu hatutaki longo longo hapa.
 
.......
Tunataka mjadala wa posho za wabunge. Mjadala wa Katiba sawa, matamko kuhusu utendaji na uzembe wa serikali sawa ila kwa sasa tungependa kuanza na mjadala huu wa posho kwa wabunge.
Tuwekeeni hapa tujadili

Ukweli ni kwamba maslahi wanayopata wabunge kwa mtazamamo wangusiwezi ni kusema ni makubwa lakini ni kwamba hakuna uwiano wa maslahi yao na watendaji wengine muhumu wa serikali.

Mbunge anamzidi

  • Mganga mkuu wa wilaya au mkoa
  • afisa kilimo mkuu wa wilaya au mkoa
  • Afisa Elimu mkuuu wa mkoa au wilaya
  • Afisa Madini wa mkoa au wilaya
  • Afisa Maji wa mkoa au wilaya
  • Afisa Nishati wa mkoa au wilaya
  • Afisa Ustawi wa jamii
  • Mhandisi mkuu wa wilaya au mkoa
  • RPC wa mkoa
Kama kweli wabunge wataka taifa lenye maeldelo wahakikishe wanachopata watu hawa ni zaidi ya kile wanachopta wabunge. Leo hii tunaona madakari, wasomi chuo kikuu wote ndoto zao ni kuwa wabunge.

Kwa nini siasa iwe ni best paid job jimboni? Watu au ajira za watu wanao takiwa k uwafrontline kuleta maedeleo ni hawa maafisa kilimo, afya madini, nyuki, etc na sio wabunge.

Kweli wabunge wanatkiwa kuwacha ubinafsi sisemi wapunguziwe nachosema hawa wengine wapate zaidi yao kama si sawa na wao.

Ilivyo sasa Tanzania best carreee ni politics. Sasa tunakwenda wapi? Na ni hatari. Je hao tunaowaiga US USA, UK, Norway Canada ndivyo ilivyo?
 
Waheshimiwa Mnyika, Zitto na Regia,

Salaam,

Naamini kabisa mtasoma na kuitikia ombi langu. Baada ya kusikia taarifa ya Mh. Makinda kuhusu posho za wabunge na upokeaji wa posho mara mbili ni vyema mkatueleza bila kificho ni kiasi gani Mbunge anapokea kila mwezi na kwa kila kikao. Vikao ikiwa ni pamoja na vikao vya kamati, safari na kadhalika. Pia mikopo, gharama za matibabu nk.

Tunataka mjadala wa posho za wabunge. Mjadala wa Katiba sawa, matamko kuhusu utendaji na uzembe wa serikali sawa ila kwa sasa tungependa kuanza na mjadala huu wa posho kwa wabunge.

Tunachohitaji ni uwazi kuhusu maslahi (kama yapo) anayopata Mbunge ili tufanye maamuzi sahihi.

... Shillingi millioni 37 na ushee alizotoa Spika kama mchango kwa waathirika wa mambo ya Gongo la Mboto ni posho ya siku moja tu hiyo. They did forefeit for a day! POSHO YA SIKU MOJA TU! Hivi sis maskini wa kweli au wa kudanganywa?
Need details?
 
[COLOR=wheat said:
MsandoAlberto;1656496]Huu ndio ushabiki wa kijinga ambao unaturudisha nyuma. Tunaongelea Chama au Wabunge? Tofautisha Chama makini na Wabunge Makini. Kwani Regia ni Mbunge wa Chama gani? Mimi ni Diwani wa Chama gani?

Kama mtu akikosea na ni mwanachama wetu tuna kila sababu ya kutokumuonea aibu, hicho ndicho chama makini. Chadema hakisimamii posho kubwa kwa wabunge. Kumbuka vita na maneno ya Dr. Slaa katika hili. Uliza msimamo wa Chama kuhusu hili. [/COLOR]

Jitahidi siku zote katika maisha yako kuwa wa msaada kwa nchi yako na nafsi yako mwenyewe. Unapoamua kuandika kitu fikiria ni msaada gani unaoutoa kwa nchi yako na nafsi yako. Huo ndio uwe muongozo wako. Ushabiki usiwe muongozo wako. Hata kama nia ni kuirekebisha CDM sio kwa njia ya kulalama na kukatisha tamaa watanzania kwa maneno 'tumeliwa' nk. Jenga hoja yako vizuri na ujumbe wako utafika.

that is true my brother Msando,some time people let their emotions doing their thinking instead of using their brain to think harder,let talk about facts and not opinion,kufanya siri malipo ya mbunge ni kujihami na nini?. kwangu mimi haingii akilini kabisi na ni kujilinda kwa kuwa wapuuzi ndio maana bunge limediriki kufanya siri.
 
viongozi wa USA hadi mshahara wa rais unajulika, kenya mishahara ya wabunge na rais inajulika na iko public kabisa,
je kwa nini tz kila kitu ni chini ya pazia?
hawa wanafanya shughli kwa ajiri ya wananchi, ndio maana wananchi hao hao waliowaweka madarakani wanataka wajue posho zao ni kiasi gani.
na wewe unaweza kutoa mchanganuo wa mshahara wako kwanza?
 
Back
Top Bottom