Elections 2010 Mkutano Wa Hadhara Wa Wana-JF [Online]

Napendekeza kuwa vipaumbele katika Uchaguzi wa 2010 viwe kama vifuatavyo;


  1. Katiba: Katiba ya nchi ina mapungufu mengi na makubwa. Katiba ndio dira ya uongozi na ustawi wa jamii huru. Katiba haiwezi kutungwa kwa matakwa ya wachache wenye mahitaji ya kujitwalia kila lililo bora katika nchi. Katiba ni lazima ijenge usawa na haki kwa watu wote bila kujali nafasi zao katika jamii. Katiba lazima ijenge heshima kwa wananchi kati yao na kwa nchi yao. Katiba ni lazima ijenge uwajibikaji. Serikali ijayo ihakikishe kuwa wananchi wote wenye uwezo wa kushiriki katika kuandaa na kutunga Katiba wanashirikishwa (kwa kuchagua) katika utungaji wa Katiba ya nchi. Kuachia kundi la wanasiasa wachache kutunga Katiba ni kunyima haki na kuondoa usawa muhimu kwa Taifa.
  2. Afya: Jinsi gani serikali ijayo itakavyohakikisha afya za wananchi wake zinaboreshwa. Hii inahusu zaidi mapambano ya nguvu dhidi ya Malaria, maambukizo ya ukimwi, na magonjwa mengine, uboreshaji na uongezaji wa hali na idadi ya hospitali/zahanati, madaktari, vitendea kazi na dawa baridi
  3. Elimu: Jinsi gani serikali ijayo itakavyo hakikisha elimu inatolewa kwa wote wenye kuihitaji ili kuondokana na ujinga na kuongeza uwezo wa uzalishaji, ubunifu na kuepukana na umasikini. Wananchi wenye elimu nzuri wanaweza kuliingizia taifa mapato makubwa kwa kutumika katika juhudi za maendeleo na pia kukodisha wataalamu kwa nchi zinazohitaji utaalam huo.
  4. Miundombinu: Serikali ijayo inahakikisha vipi kuwa barabara, njia za reli na usalama wa majini zinaboreshwa na kuwa za viwango vya juu ili kuwezesha unafuu wa uchukuzi wa mazao ya kilimo na urahisi wa usambazaji wa huduma za jamii ikiwemo ulinzi na usalama, elimu na afya na kadhalika. Vile vile, ili kuwezesha kupunguza ajali zinazoligharimu Taifa kutokana na upotevu wa maisha ya wananchi wake, upungufu wa nguvu kazi kutokana na muda wa matibabu na hata kupunguza uwezo wa wahusika kwenye ajili hizo kuzalisha kwa kiwango kizuri kama inavyotakiwa.
  5. Kilimo cha kisasa: Kwa kuwa Taifa lina ardhi nzuri yenye rutuba na ukubwa wa kutosha, serikali ijayo ifanye jitihada kuhakikisha ardhi hiyo inatumika vizuri katika uzalishaji wa mazao ya kilimo na biashara ili kuwezesha nchi kuzalisha chakula cha kutosha na kuongeza pato la Taifa kutokana na kilimo. Kwa kutumia kilimo, wakulima wataweza kujikimu na hali ngumu ya maisha kwa kuweza kuhakikisha ustawi wa familia zao na kujemga Taifa huru zaidi lenye kujitosheleza kwa chakula na bidhaa nyinginezo za mashambani. Vile vile kilimo kitapunguza tabia ya watu kuwa wachuuzi kwa bidhaa zinazozalishwa nje ya nchi.
  6. Viwanda: Serikali ijayo itakuwa na mpango gani wa kuanzisha viwanda vya usindikaji wa mazao ya wakulima na uzalishaji wa bidhaa nyingine za majumbani, maofisini na sehemu nyingine kama zinavyohitajika na jamii? Kwa kukuza viwanda, serikali itaweza kuhakikishia wakulima soko la mazao yao, kuongeza ushindani na bidhaa za nje, kuongeza ajira kwa watu wake na kuongeza pato la Taifa. Vile vile, viwanda vitaifanya nchi iwe na heshima duniani kwa kuwa na watu wenye ujuzi na ubunifu na wenye kipato kinachoridhisha zaidi.
  7. Ulinzi na Usalama: Serikali ijayo inatakiwa iwe na uwezo wa kuhakikisha kuwa mali na hali za watu wake zinalindwa kila wakati ili kuwawezesha kuzalisha zaidi, kufurahia mafanikio yao na kujenga uzalendo kwa nchi yao. Nchi salama ina uwezo mkubwa zaidi ya kukua kiuchumi na kujenga jamii yenye umoja.
  8. Ushirikishwaji wa Umma: Tanzania itajengwa na watanzania. Serikali ijayo ihakikishe kuwa watanzania wa rika zote, wenye uwezo wa kushiriki katika ujenzi wa Taifa wanashirikishwa ipasavyo katika kuamua, kujenga na kufurahia matunda ya nchi yao.
  9. Na mengine yoyote kama yatakavyochangiwa na wengine.

Du! Recta ulikuwa wapi muda wote huu toka jana?

Kwa kweli nondo zako ni makini sana na zimekamilika.

Hata hivyo ukipenda kuboresha zaidi unakaribishwa.

Hii issue ya Ulinzi na Usalama, unaweza ukaielezea kwa undani zaidi?
 
Sawa kwangu mimi naomba yafuatayo.

1. Katiba iandikwe upya kama wajumbe wengine walivyosema.

2. Nchi ianze kujengwa upya nikiwa na maana kuwa yaundwe mashirika yakishirikiana na mabenki ambayo yataanza kupanga upya miji. Sehemu zote ambazo ni unplanned zinakuwa bulldozed watu wanalipwa fidia zao na nyumba bora zinajengwa. Hii ni pamoja na miundombinu ya maji safi, maji taka, barabara, umeme, nk.

3. Jeshi la polisi liundwe upya, liwe na vifaa vya kutosha kama magari ya patrol kwenye highways na hayo magari yawe na mitandao ya satellite so they can be seen wherever they are ili kuepuka rushwa.

4. Mapato yapatikanayo na madini yahusike moja kwa moja kuhakikisha kuwa watoto wanasoma bure na watu wanapata matibabu kwa kuchangia kidogo sana.

HGoja yako ya 1 na ya 4 ziko vizuri. Hili la 2 na la 3 ni very interesting.

Unaweza ukalitolea ufafanuzi wa kina ili wadau walielewe vema?
 
Mkuu ni nani wa sasa anajali hili taifa. limebakia kama yatima! Kila mtu anajichukulia chake mapema tu. Ukiamka oooh yule ana meli, ooo huyu ana hotel ya 5 star south, ukienda kule ooh kiwira ni ya mang'anya. Tukubali tukatae hii nchi imebinafsishwa na hakuna mwenye uchungu nayo. Mwenyekiti allowance hakuna ama tufanye uzalendo tu? ni swali tu Mh. Munyakiti

Mwenyekiti Mwenza, hebu pitia hoja hizi uone kama hajatukana huyu mangi . . . haaa haaa
 
Teh teh teh! Akirudi Superman hapa utamueleza kwa nini umefanya mabadiliko! Kwani amekuachia full madaraka?

Balozi, naomba tu nukubali maana huyu DC alikubali, halafu akakataa kisha akaingia mitini. Mimi naona tunendelee tu na wewe unafanya kazi njema pia.

Asante san Msanii kwa uongozi makini.
 
Mwenyekiti kaingia mitini bila kuahirisha kikao wala kumuachia kaimu nini? Nasikia harufu ya futari, baadae kidogo.

jamani Msanii kaingia mitini naye? Ndo maana nimekuta fujo sana niliporudi.

Anyway katibu, pole na kazi nzito sasa tuendelee.
 
Ok nimepata taarifa toka kwa mwenyekiti wa dharura kuwa amepatwa na dharura hivyo atakuja kwa dharura baada ya kumaliza dharura. Ni majibu ya dharura baada ya dharura hii.

Mangi . . . Mangi . . . Vijana wa Kova wako hapa. Usinichakache mimi.
 
Mwenyekiti Asante sana,

Unajua hapa mjini tuna wale wadhamini wanaohahakikisha tunacheka mwisho wa mwezi. Tehe teh tehe.... nilikuwa nawajibika huko mkuu.

ELIMU.
M/Kiti, ukiangalia mfumo wa elimu kwetu utashindwa hata ku-define objective ni nini!! Kuanzia timing kwenye mitaala, muda wa temu za shule, etc utachoka. Siku hizi Dar kumezuka wimbi la watoto kupelekwa shule za ST NANIII...; kuna watu ambao wanalazimika kufanya hivyo simply because watoto wa jirani zake wanasababisha watoto wake wachukie kwenda shule kwa kuwa wa jirani wakiwa likizo wake (wanaosoma shule zetu za msondo) wanaenda shule. Its just likizo za st nanii na shule za msondo ni tofauti!! Serikali ni lazima ilione hili kwa macho matatu, kwanza kuwe na uthibiti wa ada (for private) na pia term ziwe sawa, Wizara ya Elkimu ndo ielekeze mitaala ya kufindishia na itumike kwa shule zote. Hii itasaidia kuwa na mfumo sawa tofauti na sasa, st nanii wanatumia mitaala yao, kila mtu na lake, mwisho tutakuwa na elimu isiyokuwa na standard moja. Nasisitiza mfumo uwe mmoja kwa shile zote!!

VOCATIONAL TRAININGS
M/Kiti hii zamani ilikuwepo na ilikuwa derfined vizuri tu, ni serikali ya CCM ndo ilivuruga mambo. Kulikuwa na a good selections kwa watoto kwenda vocational trainings, technical schools, ualimu etc. Hawa jamaa wamevuruga, mwishowe siku hizi imekuwa failures ndo wanaoenda tech schools na vocationals!! Mfumo wa elimu unapswa kuwa na mechanism ya kuchagua wanafunzi wa high schools, tech schools voct schools etc. Hii itasaidia kila mtoto kwenda kwenye fani anayopenda, maana wanafunzi wapo wa aina nyingi, kuna ambao ni artist by nature, vipaji vitakuzwa toka chini!!

Mkuu kwa sasa naomba niwakilishe.

Mkuu, hoja zako ni nzuri sana. Ila tuepuke kutaja vyama maana huu ni mkutano wa Kitaifa zaidi.

Hoja zako ni za nguvu na tutaziweka kwenye majumuisho.
 
Mbona sioni hoja nyingi lakini porojo ndiyo nyingi. Mimi vipaumbele vyangu ni;
1 Kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja (Micro economy) Uwezeshaji kwa wanaotaka kujikwamua kimaisha uanzishwe mfuko wa uwezeshaji uchangiwe na wadau ,wananchi, NGO, Serikali na wafadhili usimamiwe na bodi huru ili usitafunwe na wajanja mfuko utoe mikopo na ruzuku kwa wenye kipato kidogo.
2. Kuendeleza elimu ya juu siyo kufuta ujinga, Huduma bora za jamii elimu,afya,nk siyo bora huduma
3. Kuboresha miundombinu
4. Kodi inayotozwa na TRA iangaliwe wanaoumia ni wafanyakazi wafanya biashara hasa wakubwa Mhhh.
5. Utawala bora uboreshwe zaidi Vita ya rushwa iimarishwe na sheria ziwe kali bila kujali ruswha ndogo au kubwa.
Ni hayo tu wakuu

Baba lao hoja zako No. 2 hadi 5 zinakubalika na umeziuongelea vizuri sana. tayari ziko kwenye mchakato wa majumuisho.

Hili la kwana linavutia sana na kuna ubunifu zaidi. unaweza ukalitolea ufafanuzi wa kina?
 
Mwenyekiti, actuale can yangu iliisha nimeenda kurefeel (koh koh koh)

Halafu nimeisikiam hoja ya Eeka Mangi ya sitting allowance naomba uitolee tamko maana inahusu,,,,,,

Sasa ambalo ningependa pia tuliweke wazi ni kwamba tuwe na ukomo wa vipindi vya bunge tukirekebisha katibu, mwisho vipindi 2 vya miaka mitano2,,,,

Hili la Ukomo kwa wabunge nadhani ni hoja nzuri sana. Hebu iweke vuzuri kwa undani wadau waifahamu.

Hili la sitting allowance WoS alishalitolea ufafanuzi.

Sitting allowance wakati umesimama! wewe vipi?Jangwani hakuna sitting, standing wala sleeping allowance!
Mwenyekiti..naomba hili la mshiko nalo liwe mojaya ajenda ili mkakati wa kuondoa hizi rushwa halali uwekwe. Watu wameajiriwa kufanya kazi na sio kupokea malipo kwa kukaa!

Mkuu, ungesubiri mkutano uishe basi ndo uendelee na Vi-cans vyako. ama?
 
Kiby nashukuru sana kwa hoja zako:

Unajua toka tumeanza kikao jinsia ile nyingine walikuwa hawapo. Akaja Mchungaji moja hapa siju ni padre anajiita Rev. Masanilo, akagoma tusianze kikao hadi ile jinsia nyingine iwepo. Sasa maranyingi nawaona kwenye hilo jukwaa ulilosema. Na vijana wote wanashinda huko.

Ndo maana nimweka msisitizo sana waje.

Sasa wale nao wana vipau mbele vyao. Ila sina uhakika kama vipaumbele vya taifa tukivihusisha na mapenzi hatuwezi kuchakachua.

Au wewe unaonaje?

.
Nimekupa mheshimiwi m/kiti. Uchakachuaji wa mapenzi tunaweza tukauthibiti ikiwa ya kwamba dhamira zetu kama taifa zitasukumwa na nia ya dhati ya kusimamia maadili na utamaduni wa mwafrika.
Haya tutayafanya je? Ni lazima tutenganishe dini na serikali. Na kufanikisha hili napendekeza kuwepo na baraza linalowahusisha wakuu wote wa kidini ili waweze kutoa ufafanuzi kwa vyombo vya kisheria vya serikali pale itakapotokea mtafaruku wa mapenzi na mahusiano kwa hizi jinsia mbili. Kuna wanaoruhusika kuwa na mke mmoja, na pia kuna wanaoruhusika kuwa na mke zaidi ya mmoja na hii ni kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizo ndani ya dini zao. Hakuna kitabu chochote cha dini yoyote ya Mungu wa kweli, kinachosema mke aweza kuwa wa jinsia moja ni mme.
Mkuu wa meza nawakilisha.
 
Kiby; Kiby Kiby! Out . . . . kupumulia ndiyo nini?

Nyie vijana wa lile jukwaa mmeanza . . . Ohooooo, unaona sasa wamekata matangazo TBC?

Kunong'oneza gani huko unaongelea kwenye MIC na mkutano uko live TBC.

Kova ondoka naye huyu . . . .

(Haaa haaa du! Nimecheka sana)

.
Aaah bana, nchi hii kuna linaloshindikana? Mmenikabizi kwa Kova, tukiwa njiani kuelekea kituoni ilinilazimu kuongea kwa herufi kubwa. Ameniachia na ndio maana mnaniona hapa mkutanoni.
Japo nimeonywa kubadilika, lakini ni nani aliye ndani ya moyo wangu ajue kama nimebadili msimamo? M/kiti utanikabizi MIC mara moja tena kabla ya mkutano kufungwa?
 
Elimu, afya, kilimo ni std. & general agenda ambazo zinaimbwa kama vibwagizo kila mwaka wa uchaguzi.

Nadhani tunahitaji more pragmatic agenda ambazo tunaweza kuona matokeo baada ya miaka mitano kama vile:
  • Kuboresha mji wa Dar (Dar ndiyo ''reception hall'' ya TZ). Ni chafu, hamna maji, haina mpangilio, misongamano, n.k.
  • Kutokomeza malaria TZ (manageable)
  • Constitution inayoeleweka (piece of cake kukiwa na utashi ..) na agenda zingine specific na zinazotekelezeka kama hizi
 
Ooh! Mwenyekiti Mwenza kuwa huru tu, in fwakti unanisaidia sana na umeonyesha mshikamano wa hali ya juu kuendesha mkutano huu wa wadau wa JF.

Mimi nadhani hili suala itabidi liingie katika katiba ili lisichakachuliwe. kama vipi basi UwT ivunjwe na iundwe upya huku kikiwa ni chombo huru na nidhamu kikijali maslahi ya taifa na bila kujiingiza katika siasa.
Mkuu umeiboresha vyema sana hii kitu. Naunga mkono kuwa hoja kuhusu UwT ni kuitazama sheria inayoiunda kisha kutafakari kwa kina namna ya kuifanya iwe bora zaidi kwa taifa hili. Hivyo serikali itakayoingia madarakani inapaswa kufahamu kwamba UZALENDO si kuwalinda viongozi bali kulitumikia TAIFA na kulifia TAIFA.
Thanx mwenyekiti umerudi
 
.
Nimekupa mheshimiwi m/kiti. Uchakachuaji wa mapenzi tunaweza tukauthibiti ikiwa ya kwamba dhamira zetu kama taifa zitasukumwa na nia ya dhati ya kusimamia maadili na utamaduni wa mwafrika.
Haya tutayafanya je? Ni lazima tutenganishe dini na serikali. Na kufanikisha hili napendekeza kuwepo na baraza linalowahusisha wakuu wote wa kidini ili waweze kutoa ufafanuzi kwa vyombo vya kisheria vya serikali pale itakapotokea mtafaruku wa mapenzi na mahusiano kwa hizi jinsia mbili. Kuna wanaoruhusika kuwa na mke mmoja, na pia kuna wanaoruhusika kuwa na mke zaidi ya mmoja na hii ni kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizo ndani ya dini zao. Hakuna kitabu chochote cha dini yoyote ya Mungu wa kweli, kinachosema mke aweza kuwa wa jinsia moja ni mme.
Mkuu wa meza nawakilisha.

Kiby hii issue uliyoianzisha ni nzito saaana. Imejikita katika sehemu tatu: Haki Za Binadamu; Maadili Na Dini.

Labda bila kwenda ndani sana linaweza likaingizwa katika katiba likiwa chini ya haki za binadamu "Kwamba Kila Mtu ana Haki ya Kupenda na Kupenda"

Sijui unaonaje?
 
.
Aaah bana, nchi hii kuna linaloshindikana? Mmenikabizi kwa Kova, tukiwa njiani kuelekea kituoni ilinilazimu kuongea kwa herufi kubwa. Ameniachia na ndio maana mnaniona hapa mkutanoni.
Japo nimeonywa kubadilika, lakini ni nani aliye ndani ya moyo wangu ajue kama nimebadili msimamo? M/kiti utanikabizi MIC mara moja tena kabla ya mkutano kufungwa?


Kijana wangu usiniambie kuwa umetoa rushwa na Kova kapokea? Hilo ni kosa kwa mujibu wa sheria.

Tutafika kweli? Tufanyeje ili kumaliza tatizo hili la Rushwa iliyokithiri?


Haya Kamata Mic umalizie hoja zako.
 
Elimu, afya, kilimo ni std. & general agenda ambazo zinaimbwa kama vibwagizo kila mwaka wa uchaguzi.

Nadhani tunahitaji more pragmatic agenda ambazo tunaweza kuona matokeo baada ya miaka mitano kama vile:
  • Kuboresha mji wa Dar (Dar ndiyo ''reception hall'' ya TZ). Ni chafu, hamna maji, haina mpangilio, misongamano, n.k.
  • Kutokomeza malaria TZ (manageable)
  • Constitution inayoeleweka (piece of cake kukiwa na utashi ..) na agenda zingine specific na zinazotekelezeka kama hizi

Mkuu Cynic unajua agenda ulizozitaja ni kali sana na mpaka sasa hakuna aliyezitaja:

Unaweza ukazielezea kwa undani ili Wana-JF waweze kulielewa vema?

Hongera sana. Please kamata Mic.
 
Mkuu umeiboresha vyema sana hii kitu. Naunga mkono kuwa hoja kuhusu UwT ni kuitazama sheria inayoiunda kisha kutafakari kwa kina namna ya kuifanya iwe bora zaidi kwa taifa hili. Hivyo serikali itakayoingia madarakani inapaswa kufahamu kwamba UZALENDO si kuwalinda viongozi bali kulitumikia TAIFA na kulifia TAIFA.
Thanx mwenyekiti umerudi

kamnanda Tuko pamoja.

Unajua nafasi ya UwT katika uendeshaji wa Serikali na kusimamia Maslahi ya Nchi ni kubwa sana. Ni vema wasijihusishe na siasa kabisa.
 
Back
Top Bottom