Mkapa, Vincent na Madaraka: What Else?

Kwa wale tuliokuwa watu wazima 1989 tunakumbuka Jinsi Mwalimu alivyolazwa Uingereza kwa matibabu ya Kansa (Saratani) ya damu ambayo hatimaye ndiyo ilikuja kumuua.

Hizi tabia za kusahau mambo ya msingi ndiyo imetufikisha hapa tulipo. Toka 1989 hadi leo 2012 imepita miaka 23 huyu Vincent alikuwa wapi kutuambia kwamba Mkapa amempa Mwalimu Sumu itakayokuja kumuua? Kama amejua siku za hivi karibuni ni nani aliyemwambia? Hivi mwaka 1989 wakati Mwalimu anafanyiwa Opresheni ya kuzuia kansa kusambaa mwilini mwake Mkapa alihusikaje?
Mh! Hapa umetuingiza chaka, hili tukio halijapata kutokea katika historia ya Mwalimu. Kansa yake iligunduliwa 1998, mwaka mmoja baada ya ile birthday yake maarufu ya 75 (mwaka 1997) ambako katika hotuba alikuwa amesema "....nitapiga makumi mawili manne, NINA HAKIKA! Nitamwona rais wetu wa nne, NINA HAKIKA" akimaanisha alikuwa na uhakika wa kuishi miaka zaidi ya themanini na kuchagua hadi rais wetu wa nne.

Na hiyo kansa alidumu nayo mwaka mmoja tu na kufariki akiwa na miaka 77, maskini hakuifikia ile 80 aliyokuwa amesema ana uhakika "angepiga"! Na wala hakuwahi kufanyiwa operesheni, haiko kwenye rekodi za maisha yake. Kama unazungumzia bone marrow biopsy hiyo ni diagnostic procedure, na wala siyo huo mwaka wa 1989, ni 1998 alipogunduliwa na Chronic Lymphocytic Leukemia.

Hakuna taarifa kuwa Mwalimu aliwahi kufanyiwa bone marrow transplant ambayo ni mojawapo ya tiba za uhakika za CLL, na hii ingefanana na operation, na ingemwezesha kuishi miaka isiyopungua 10 bila leukemia. Lingine ni kuwa prognosis ya CLL siyo mbaya kama ilivyotokea kwa Mwalimu Nyerere ambaye alidumu nayo kwa mwaka mmoja tu.
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji naiamini sana Hard Disk yako huwa inatupatia vitu adim sana hapa jukwaani. Nadhani ukiiscan inaweza kutupa japo fununu kuhusu kuhusika kwa Mkapa kwenye kifo cha mwalimu.
hebu tusaidie kutegua kitendawili hiki
 
CCM waliamini Mkapa atakua silaha kubwa ya maangamizi dhidi ya CDM ila Jinamizi la Mwalimu Nyerere limemvaa Mkapa na kugeuza kibao ambapo matokeo yake Mkapa kageuka kuwa silaha ya maangamizi dhidi ya chama chake CCM.
Damu ya Mwalimu iwaangamize wote walioshiriki kumzimisha mzee huyu.
 
- Ninajiuliza swali moja hawa wote ni Familia moja, sasa wanapochafuana huko Arumeru as they have done, linakuja swali moja kubwa je hawa wanafamilia moja wana siri ngapi zingine hawajatuambia wa-Tanzania? Au tusubiri kampeni nyingine ya siasa tuwapange tena tusikie zaidi? Just curious!

- Lakini hawa wana siri nyingi tunahitaji kuzijua Wananchi wa Tanzania!, sasa wapangwe tena another kampeni!, I mean kinachoendelea huko Arumeru ni serious business:

- HOWEVER: hivi kweli CCM haikuwa na mwingine wa kumpeleka Arumeru zaidi ya Mkapa? I mean kweli Viajna wote walioko CCM Why him?


FMEs!

kwa watu wote wa cccm waliobaki hakuna msafi-
eti kwao 'mkapa anaonekana msafi"-ndo maana wanampeleka yeye-maana hao wengine waliobaki wana madudu sana kiasi kwamba watachafua hali ya hewa kwenye kampeni kama hizi
 
Duh ama kweli wewe mgumu sana kuelewa. Sizungumzii alichoandika FMES isipokuwa ulichoandika wewe dhidi ya maneno ya Mkapa.. Mkapa alisema hivi:-“Nimefanya kazi na Mwalimu kwa miaka 25, nikiwa mwandishi wake, Waziri na katika muda huo, nimemzika yeye, kaka yake na mama yake mzazi, sijawahi kusikia jina la mtu kama huyo katika familia hiyo”.

Ndipo VN na Madaraka wakaingilia kati na kuweka habari hii sawa. Kwa kauli ya Mkapa alikuwa na maana Ukoo (katumia familia hiyo)maana kamhusisha hadi kaka na mama yake mwalimu ndio maana Madaraka na VN wakamwaga mboga.

Mkandara,

..nakubaliana na wewe 100% kwamba Mkapa alikuwa na lake jambo.

..Mkapa alilenga kumdhalilisha Vicent Nyerere. tatizo ni kwamba hawa ndugu zetu wa kutoka Mara dharau ni kitu ambacho hawa-entertain hata siku moja.

..nikupe kisa kimoja kilichonitokea mimi binafsi.

..yupo rafiki yangu mmoja tumeshibana sana toka shuleni. huyu bwana alihudhuria mkutano mmoja wa hadhara wilayani kwetu akakumbana na mtu ana jina kama langu. Yaani jina la kwanza na la ukoo!!!

..alichofanya huyu rafiki yangu ni kumtafuta yule jamaa mwenye jina kamili kama langu na kumdadisi kidogo undani wake. matokeo yake alikuja kufahamu kwamba yule alikuwa mtoto wa baba yangu mdogo!!!

..baadaye huyu jamaa yangu akanipigia simu na kunieleza kisa chote, na jinsi alivyopata mshituko kusikia mtu anajitambulisha kwa majina yangu. na mimi nikamhakikishia kwamba huyo aliyekutana naye ni ndugu yangu.

..alichotakiwa kufanya Mkapa ni kumdadisi Vicent Nyerere directly, kwa uungwana, au kuwatafuta kina Makongoro,Madaraka,Magige, na kuwauliza habari za Vicent.

NB:

..haiyumkiniki Mkapa akawa hamfahamu Josephat Kiboko Nyerere, baba mzazi wa Vicent Nyerere.
 
.... pamoja na yote yanayojulikana leo hii kuhusu UFISADI wa kutisha ambao umefanyika baada ya tukio la October 14, 1999 HAIPANDI akilini kwamba UFISADI HUO hauonewi aibu na wahusika. They remain as cocky albeit shameless as statesmen. Very strange!
 
..Mkapa alilenga kumdhalilisha Vicent Nyerere. tatizo ni kwamba hawa ndugu zetu wa kutoka Mara dharau ni kitu ambacho hawa-entertain hata siku moja.

..alichotakiwa kufanya Mkapa ni kumdadisi Vicent Nyerere directly, kwa uungwana, au kuwatafuta kina Makongoro,Madaraka,Magige, na kuwauliza habari za Vicent.

NB:

..haiyumkiniki Mkapa akawa hamfahamu Josephat Kiboko Nyerere, baba mzazi wa Vicent Nyerere.

Mkuu JokaKuu,

Kuna mwana familia mmoja wa Nyerere amesema kwamba, Marehemu Mzee Josephat Kiboko Nyerere (RIP) alipofariki, Mkapa alienda kuhudhuria mazishi. Kwa hiyo hisia kwamba Mkapa alikuwa hamfahamu Mzee Josephat Kiboko Nyerere haiko sahihi.

Bottom line ni kwamba Mkapa hakuwa na hoja/sera za kuwapa wana Arumeru Mashariki na ndipo alipoingiza sera mufilisi za madharau na kejeri akijua kwamba labda Vincent Nyerere angekaa kimya kwa kumheshimu.
 
- Wakuu ndio tatizo letu wa-Tanzania, mara ngapi wakati wa kumbu kumbu za Mwalimu tumesikia Familia ya Mwalimu wakisema Mkapa ni mwana-familia yao? Magazeti mengi sana yamewahi kusema haya kwamba Mkapa ni familia ya Mwalimu sasa why leo mnashangaa?

- Hebu atokee mwanafamilia ya Mwalimu aseme bila uoga kwamba hawajawahi kusema Mkapa ni member wa familia yao! Tuwakumbushe siku na tarehe na aliyeyasema na wapi, WA-Tanzania sio mabwege tena siku hizi, hawa ni familia moja bana! sasa watumabie what else they know au wanaficha kuhusu Taifa!


Es!

FMES,
Wewe ukienda safari Uingereza, ukapewa honorary citizenship haina maana kwamba wewe sasa ni raia wa Uingereza.
Kama Mkapa angekuwa real member wa family ya Nyerere angejua Vincent ni nani. Full stop.
 
Ufamilia wa Mkapa ni wa kutunukiwa tu, kama ilivyo kwa udokta wa kutunukiwa nk.

Dokta wa ukweli ni tofauti na dokta wa kutunukiwa, vivyo hivyo kwa ndugu, yani ndugu wa ukweli ni tofauti na yule wa kutunukiwa regardless of the customs.

Status ya undugu itakuwa enforced kutokana na customs za kabila husika, lakini kiukweli there is lots of differences btn the two.
 
asanteni chadema kwakumchagua vincent nyerere kuwa meneja kampeni mana angekuwa muheshimiwa mwingine haya yote tusingeyajua..
 
Wasiwasi wa Mkapa ni Kwamba now hana Uhakika Familia ya Nyerere inasemaje juu ya Kifo Cha Mwalimu. Yawezekana kabisa Kilichosemwa na Vicent ni Manung'uniko katika Familia ya Mwalimu ya Kifo cha Mwalimu. Kwamba Vicent amezungumza Hadharani kile kinachozungumzwa kwa Kificho huko Butiama.

Kwa Kifupi Mkapa Atakuwa amegundua kwamba HAAMINI ndani ya Familia ya Nyerere
 
Mkuu FMES,

Habari za Nyerere kumalizwa na Mkapa tulishasikia miaka mingi iliyopita Vicent karudia tena vyombo vya habari vimeamua kuipatia umuhimu kwasababu aliyesema ni mwanaukoo wa Nyerere.Mkuu FMES hakuna siri nyingine zaidi ya hii kwamba Nyerere alitangulizwa kabla ya siku zake ili wauze benk yetu ya NBC kwa bei poa,waingie mikataba mibovu ya uchimbaji wa madini,wanunue ndege ya rais ikibidi tule majani,wanunue rada kwa bei kubwa kupita kiasi na wauze viwanda vyetu kwa marafiki zao kwa bei poa.

Yote haya yasingefanyika kama Nyerere asingetangulizwa mapema,bahati mbaya Nyerere hakumjua Mkapa hadi aliposhiriki kumuingiza magogoni kwa gharama kubwa sana ikiwemo kuwapakazia na kuwachafua washindani wake ndani ya CCM na nje ya CCM.
Ahaaaa kumbee
Ndo maana ufisadi wote uliofanyika kipindi cha Mkapa ni baada ya kumuua Nyerere

ANNBEN kuanziswa ikulu, kuuza dhahabu yetu bure kwa manufaa binafsi, kuuza mashirika ya umma , kujikwapulia majengo na viwanja vya TTCL kupitia mwanae aliyekuwa MD SIMUE2000 waliopewa dhamana ya real estate za TTCL

Na ushenzi mwingine wa mkapa ni baada ya kummaliza aliyekuwa kikwazo , JKN
 
- Wakuu ndio tatizo letu wa-Tanzania, mara ngapi wakati wa kumbu kumbu za Mwalimu tumesikia Familia ya Mwalimu wakisema Mkapa ni mwana-familia yao? Magazeti mengi sana yamewahi kusema haya kwamba Mkapa ni familia ya Mwalimu sasa why leo mnashangaa?

- Hebu atokee mwanafamilia ya Mwalimu aseme bila uoga kwamba hawajawahi kusema Mkapa ni member wa familia yao! Tuwakumbushe siku na tarehe na aliyeyasema na wapi, WA-Tanzania sio mabwege tena siku hizi, hawa ni familia moja bana! sasa watumabie what else they know au wanaficha kuhusu Taifa!


Es!

kwa hiyo wameamua kuweka siri za mwanafamilia hadharani sio? wanamkumbatia mwanafamilia muuaji sio?
 
wanajf,hakuna jipya wanarudia rudia tu,mod maliza mjadala kama ile ya ubadhilifu ya cdm,mod be fair
 
wanajf,hakuna jipya wanarudia rudia tu,mod maliza mjadala kama ile ya ubadhilifu ya cdm,mod be fair
Lakini mkuu wangu sii aliyefungua mjadala ni Mkapa mwenyewe..sasa tatizo liko wapi kumjadili mwanafamilia ambaye sisi hatukujua?..
 
Duh yaani leo narushiwa virus kwenye Pc hadi mwenyewe nashika adabu...Jamani nazungumza kipi hadi mnaniwekea cookie ya ku trace na worms na kadhalika..tujadili tu wakubwa hakuna sababu ya kuharibiana Pc..
 
Back
Top Bottom