Mkapa, Vincent na Madaraka: What Else?

sina hakika kama unajua hesabu mkuu mwalim aliekufa 1989 ni yupi? kama nyerere ni 1999 hyo ni mwalim wako wa primary au? tupeni jibu sisi 2tajuaje kama alikufa kwa canser au sumu? cha msingi nkpa atupe jibu sahihi

Mkuu umenifanya nicheke usiku huu, sijui watu wengine huwa wanapost vitu gani humu.
 
Duh yaani leo narushiwa virus kwenye Pc hadi mwenyewe nashika adabu...Jamani nazungumza kipi hadi mnaniwekea cookie ya ku trace na worms na kadhalika..tujadili tu wakubwa hakuna sababu ya kuharibiana Pc..
mkuu nipe na mm hayo maujanja, wanatupia vp hivyo virusi isije ikawa na mm huku wanavileta bila kujua maana naona pc yangu inasinzia sinzia km imekunywa dawa ya usingizi.
 
Tatizo hapa mnachanganya kati ya uzao wa Mwalimu na familia ya mwalimu. Wote tunafahamu kwamba kuwa mwanafamilia si lazima uwe uzao wa baba wa familia. Mtoto wa kuasili (adopted child) anakuwa moja kwa moja mwanafamilia. Na kwa ushahidi uliopo kwenye vyombo vingi vya habari MKapa aliasiliwa na Familia ya Mwalimu (hakuasiliwa na Ukoo wa kina Nyerere) na familia nzima inamchukulia kama ni mtoto wa "nyumbani"

Kwa hiyo MKapa si wa ukoo wa Nyerere lakini ameasiliwa (adopted) na Familia ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Baba wa Taifa la Tanzania. Na kwa ufahamu wangu alichosema yeye ni kwamba Vincent si mtoto wa Mwalimu (Kwa hili yuko sahihi kabisa) lakini hakuna sehemu amesema Vincent si wa ukoo wa Nyerere!!
Well put.
 
mkuu nipe na mm hayo maujanja, wanatupia vp hivyo virusi isije ikawa na mm huku wanavileta bila kujua maana naona pc yangu inasinzia sinzia km imekunywa dawa ya usingizi.
Dah sii umeona sikuwepo kwa karibu masaa manne.. natumia Anti virus tu mkuu lakini kila dakika napata warning..
 
- Hapo ndipo ninapo-question busara za CCM the giant kumpelekea kule, wakati wanao Vijana wengi sana ambao wangeweza kwenda huko na kukamilisha kazi, I mean I hope itakuwa lesson learned, kama Januari aliwea kushinda jimbo lake kwa kishindo, leo atashindwa nini kushinda huko Arumeru? Na ni lini hawa kina Januari watapewa nafasi hizi?

ES!
Do you mean CCM primaries? ninavyojua January alipita bila kupingwa.
 
Usdijibu PM za watu humu..... kuna mambo ya ajabu yamenitokea. But nawaambia mnapoteza muda.
Ma virus na malwarebytes..... acheni hizo!!
 
Kwa wale tuliokuwa watu wazima 1989 tunakumbuka Jinsi Mwalimu alivyolazwa Uingereza kwa matibabu ya Kansa (Saratani) ya damu ambayo hatimaye ndiyo ilikuja kumuua.

Hizi tabia za kusahau mambo ya msingi ndiyo imetufikisha hapa tulipo. Toka 1989 hadi leo 2012 imepita miaka 23 huyu Vincent alikuwa wapi kutuambia kwamba Mkapa amempa Mwalimu Sumu itakayokuja kumuua? Kama amejua siku za hivi karibuni ni nani aliyemwambia? Hivi mwaka 1989 wakati Mwalimu anafanyiwa Opresheni ya kuzuia kansa kusambaa mwilini mwake Mkapa alihusikaje?
Time is the best teacher, but unfortunately, it kills all of its students. Sasa wewe kwa kutumia uzamani unataka watu wasiseme? Kuna kesi huwa zinakaa hadi miaka 100 lakini watu wanazifufua, nina imani hata VN asingesema lazima tu kuna mtu angekuja kusema. Kesi hasa za mauaji huwa hazina muda maalumu unaweza kuua ukajificha ukafikiri umepona. Hujasikia mifupa imefukuliwa na kuhukumiwa.
 
Ukweli utabaki kuwa ukweli mkapa alipewa undugu wa akina nyerere kwasababu za kisiasa na hivyo undugu wa mkapa kwa akina madaraka hauna nguvu ila vicent atabaki kuwa mwanafamilia hiyo haiwezi kupingwa hata aje nani, vicent ni mtoto wa mwl full stop!
 
Ukweli utabaki kuwa ukweli mkapa alipewa undugu wa akina nyerere kwasababu za kisiasa na hivyo undugu wa mkapa kwa akina madaraka hauna nguvu ila vicent atabaki kuwa mwanafamilia hiyo haiwezi kupingwa hata aje nani, vicent ni mtoto wa mwl full stop!

Kwani Mkapa aliwaomba awe ndugu yao?
 
Alipewa heshima hiyo na wanafamilia. Soma kipande hiki cha gazeti la ThisDay la jumapili, tarehe 27 April 2008(online version):



Ofcourse, kwa heshima hiyo tu huwezi kumwita Mkapa Nyerere! FMEs nadhani ameandika ki fasihi zaidi kunogesha kile anachotaka kusema.


hakuna cha familia wala nini!!! mbona jk anatembelea iringa wahehe wanamvalisha kikwete mavazi ya kichifu na kusema kuwa kuanzia leo jk ni miongoni mwa machifu wetu je jk anabalika kutoka UKWERE kwenda UHEHE? Lahasha!!! kwa minajili hiyo Mkapa kapewa title tu na hakuna uhalisia
 
Mkuu FMES,

Habari za Nyerere kumalizwa na Mkapa tulishasikia miaka mingi iliyopita Vicent karudia tena vyombo vya habari vimeamua kuipatia umuhimu kwasababu aliyesema ni mwanaukoo wa Nyerere.Mkuu FMES hakuna siri nyingine zaidi ya hii kwamba Nyerere alitangulizwa kabla ya siku zake ili wauze benk yetu ya NBC kwa bei poa,waingie mikataba mibovu ya uchimbaji wa madini,wanunue ndege ya rais ikibidi tule majani,wanunue rada kwa bei kubwa kupita kiasi na wauze viwanda vyetu kwa marafiki zao kwa bei poa.

Yote haya yasingefanyika kama Nyerere asingetangulizwa mapema,bahati mbaya Nyerere hakumjua Mkapa hadi aliposhiriki kumuingiza magogoni kwa gharama kubwa sana ikiwemo kuwapakazia na kuwachafua washindani wake ndani ya CCM na nje ya CCM.

Mkuu, umeniacha nikasimama nikisoma bila kujijua! sasa kama mambo ndiyo haya Tanzania tutapona kweli? Laana hii si hatari?
Lakini dalili za mvua ni mawingu. Mungu huonyesha ishara za vitu lakini binadamu mgumu kuelewa au dhaifu kutafakari. Mtu unashika nchi, meli inageuka juu chini kama ndoo kule Victoria maelfu wanaangamia tunaangalia hivi hivi? Hatukuweza kufanya lolote kuokoa hata binadamu mmoja? Loh!
 
- Wakuu ndio tatizo letu wa-Tanzania, mara ngapi wakati wa kumbu kumbu za Mwalimu tumesikia Familia ya Mwalimu wakisema Mkapa ni mwana-familia yao? Magazeti mengi sana yamewahi kusema haya kwamba Mkapa ni familia ya Mwalimu sasa why leo mnashangaa?

- Hebu atokee mwanafamilia ya Mwalimu aseme bila uoga kwamba hawajawahi kusema Mkapa ni member wa familia yao! Tuwakumbushe siku na tarehe na aliyeyasema na wapi, WA-Tanzania sio mabwege tena siku hizi, hawa ni familia moja bana! sasa watumabie what else they know au wanaficha kuhusu Taifa!


Es!

Wakuu, Mkapa ana undugu wa "heshima" katika ukoo wa Nyerere aliotunukiwa mwaka 2000, nadhani ni kwa sababu hii aliweza kuwa na confidence hata akasema hamtambui Vicent...ilhali ndiye aliyemkabidhi pesa za ubani wa msiba wa mdogo wake Mwalimu mwaka 2000....
 
Ha ha ha, mkapa-nyerere, mhhhhhh nyerere-mkapa. Tutawapima dna sasa.

Julius kambarage nyerere
benjamini willium mkapa

labda kama waliwahi kuoa nyumba moja, ila kwa hili- mkapa atafute ndugu wengine, sio nyerere.
 
- Ninajiuliza swali moja hawa wote ni Familia moja, sasa wanapochafuana huko Arumeru as they have done, linakuja swali moja kubwa je hawa wanafamilia moja wana siri ngapi zingine hawajatuambia wa-Tanzania? Au tusubiri kampeni nyingine ya siasa tuwapange tena tusikie zaidi? Just curious!

- Lakini hawa wana siri nyingi tunahitaji kuzijua Wananchi wa Tanzania!, sasa wapangwe tena another kampeni!, I mean kinachoendelea huko Arumeru ni serious business:

- HOWEVER: hivi kweli CCM haikuwa na mwingine wa kumpeleka Arumeru zaidi ya Mkapa? I mean kweli Viajna wote walioko CCM Why him?


FMEs!

Mkapa kalikoroga kwa sababu hakutaka kwenda Arusha........
 
Huu ni mwisho wa ccm.Mtaona mengi sana.Maana Mwenyezi mungu ameona sasa hawa jamaa basi.Kwa hiyo watanzania .tupambane watoke hawa jamaa,mafisadi.Waana sera za zamani sana.Wameishiwa nini waseme.
 
Watu wanashangaa hili, Basi niwaambie jingine.. Watu wa Mara kimila anaweza kuoa mke kisha huyo mke akatembea nje ya ndoa na kuzaa mtoto, huyo mtoto bado atakuwa wa mume ktk ndoa japo sii damu yake..
 
I have feelings that former Pres. Mkapa was kinda drunk.. (kwa wale mnaomfahamu kwa karibu mtaelewa)! Kama angekuwa sober asingeweza kuongea kipuuzi kwenye mkutano wa kampeni kama alivyofanya.. He is too experienced to behave like that!
 
Back
Top Bottom