YAGHAMBA
JF-Expert Member
- Aug 8, 2012
- 545
- 147
Kauli ya J.K kuwa kuna watu walijaribu kuwagombanisha watanzania kwa kutumia ukabila wakashindwa na kwamba sasa wanatumia udini ni ishara kuwa Mungu ameamua CCM wajiumbue wenyewe kwani CCM na wapambe wao walikuwa mstari wa mbele kuwahadaa wananchi kuwa kuna vyama vya siasa vya ukabila dhana ambayo ilishindwa kama JK mwenyewe alivyokiri jana na hili la udini aliloliasisi mwaka 2010 na kulilea kwa serikali yake kuachia mihadhara ya kukashifu kanisa ikifanywa nchi nzima bila kificho ili mradi pia wahubiri hao wakikisema vibaya CHADEMA. Rais na serikali yake ya CCM waliona hilo halina madhara bora CHADEMA inasemwa vibaya na wahadhiri hao. Leo anapokuja JK na kusema hayo anayoyasema huo ni UNAFIKI, nchi imefika hapa ilipo kwa udhaifu wake na upuuzi wa CCM.
Naomba watanzania tuukatae unafiki huu. Tulikataa kugawanywa na CCM kwa ukabila na sasa tusikubali kugawanywa na CCM kwa udini.
Naomba watanzania tuukatae unafiki huu. Tulikataa kugawanywa na CCM kwa ukabila na sasa tusikubali kugawanywa na CCM kwa udini.