Kikwete: Waliochochea ukabila ndio wanachochea udini leo...

Status
Not open for further replies.
Hivi mama salma anaendeleaje ma kichanga chake?? Kweli rais tunaye!
cacico unataka kusema mzee kafanya mambo White House??

Atakuwa hana adabu namna hiyo. Kwanza umri umempita huyo atakuwa mtoto au mjukuu wake?
 
Last edited by a moderator:
najisikia vibaya lakini angeniuliza mimi nani wamekuza masuala ya ubaguzi wa dini na ukabila ningesema bila hiyana ni CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) na ndugu zetu WAISLAMU hasa washabiki wa PONDA ambao kila anachosema hawana muda wa kuchuja ..ndo ukweli.
 
KIKWETE kama suala la dini litamgusa kila mtu mimi nazani bora hvo ndo tutakapo heshimiana.lets fight each other
 
Kwasababu kawalaumu chadema kwa udini,statement hii hapo chini inaonyesha kwamba chadema ni chama cha kidini kisichozivumilia dini nyingine?chadema wamemyima nani uhuru wa kuabudu?Halafu chadema watakaaa kimya?
"Ndugu zangu, siku zote tumekuwa na dini zetu, kila mmoja akiwa na uhuru wake wa kuabudu anachokitaka na kukiamini na kwa namna anavyotaka yeye. Ni muhimu tuendelee kuheshimu tofauti zetu za dini bila kuzigeuza tofauti hizokuwa chimbuko na sababu ya ugomvi."
 
Jamani wana JF

Someni haya asemayo Kikwete sasa kuhusu udini na ukabila kisha mtafakari wenyewe.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


JK: Moto wa dini hautakuwa na mshindi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete jana, Jumapili, Oktoba 28, 2012, ameanza ziara ya siku nne kukagua shughuli na kuzindua miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Kilimanjaro kwa kuwaambia Watanzania kuwa moto wa dini ambao umeanza kujitokeza katika Tanzania hautakuwa na mshindi.

Rais Kikwete ameanzia ziara yake kwenye Wilaya ya Same ambako amehutubia mkutano wahadhara kwenye eneo la Stendi ya Mabasi ya mjini Same ambapo amewaambia mamia ya wananchi kuwa baada ya watu wasioitakia Tanzania mema kushindwa kuwafarakanisha Watanzania kwa kutumia ukabila sasa wamegeukia dini.

“Kuna watu hawana raha na utulivu na amani ya nchi yetu. Walijaribu kutufarakanisha kwa kutumia ukabila lakini hili lilishindikana na sasa wamegeukia dini. Lakinindugu zangu moto wa dini hautakuwa na wa kuuzima na hautakuwa na mshindi,” Rais Kikwete amewaambia wananchi kwenye mkutano huo.

Amewataka Watanzania kuendelea na utulivu wao wa kidini na wakatae kufarakanishwa kwa tofauti za dini.

“Ndugu zangu, siku zote tumekuwa na dini zetu, kila mmoja akiwa na uhuru wake wa kuabudu anachokitaka na kukiamini na kwa namna anavyotaka yeye. Ni muhimu tuendelee kuheshimu tofauti zetu za dini bila kuzigeuza tofauti hizokuwa chimbuko na sababu ya ugomvi.”

Rais Kikwete pia amewahakikishia wananchi wa Same kuwa Serikali imedhamiria kumaliza tatizo la maji katika maeneo ya wilaya hiyo na wilaya za jirani za Mwanga na Korogwe katika Mkoa wa Tanga.

Amesema kuwa mradi mkubwa wa kusambaza maji katika vijiji 34 katika wilaya hizo kutoka Bwawa la Nyumba ya Mungu utaanza kutekelezwa Februari mwakani. Mradi huo wenye thamani za dola za Marekani bilioni 34 utawahudumia wananchi katika vijiji 14vya Wilaya ya Same na utachukua kiasi cha miezi 18 kukamilika.

Rais Kikwete ataendelea na ziara yake leo, Jumatatu, Oktoba 29, 2012 kwa kuzindua Kiwanda cha Tangawizi kilichoko Mamba Miamba na kufanya mkutano hadhara na wananchi. Baadaye kesho, Rais Kikwete atazindua Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Asha-Rose Migiro iliyoko Mwanga.

Imetolewa na:
Kurugenziya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dares Salaam.
29Oktoba, 2012

My Take:
Hivi ni nani aliyekuwa anachochea ukabila kama sio CCM?? Kwahiyo na udini unachochewa na CCM? Je, JK anakishtaki chama chake kwa wananchi???

dola billion 34?matatzo ya mis-information cjui yataisha lin!
 
Kikwete atamaliza sarakasi zote lakini yeye ndiye mwasisi wa sera za udini na ukabila katika kutumia kanuni ya wagawe uwatawale, hawezi kukwepa kabisa.Hakika Kikwete ni janga kubwa kwa taifa letu.
 
kama kila mtu anahaki ya kuabudu anachokitaka na anachokiabu kiheshimiwe sasa kwann baadhi ya watu wanaingilia imani za wenzao mf: matukio kadhaa tumeyaskia ya kuchanwa kwa quran lkn mmeshindwa kuwachukulia hatua waliofanya badala yake mnasubiri matokeo ndomuachukulia hatua wanaopinga kudhalilishwa kitabu chao na kuitetea imani yao.Hv ni nani huyo unaemzungumzia anayeleta udini km sio ww na serikali yako? hv ni kiongozi gani asiyejua kua mtu yeyote kuingilia na kuikashifu imani ya mwenzie ni kosa la jinai? na viongozi wangapi wa taasisi na idara mbalili za serikali wanaonyesha udini wa wazi wazi ktk utendaji mf:necta na mmeshindwa kuwachukulia hatua yeyote badala yake mnaendelea kuwakumbatia na kuficha uchafu wao?
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Amesema kuwa mradi mkubwa wa kusambaza maji katika vijiji 34 katika wilaya hizo kutoka Bwawa la Nyumba ya Mungu utaanza kutekelezwa Februari mwakani. Mradi huo wenye thamani za dola za Marekani bilioni 34 utawahudumia wananchi katika vijiji 14vya Wilaya ya Same na utachukua kiasi cha miezi 18 kukamilika.
Imetolewa na:
Kurugenziya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dares Salaam.
29Oktoba, 2012

Salva naye atasema kateleza vidole?......dola bilioni 34? ama kweli ikulumawasiliano@yahoo.com
 
WTF!!!

Kurugenzi ya mawasiliano ikulu!!!

Mradi huo wenye thamani za dola za Marekani bilioni 34 utawahudumia wananchi katika vijiji 14vya Wilaya ya Same na utachukua kiasi cha miezi 18 kukamilika.
 
Nilisikia wakati fulani story ya mtoto fulani alizaliwaga na kichwa cha nazi huko Bagamoyo sijui ndiye huyuuu!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom