Mtafiti Makini
Member
- Apr 11, 2011
- 14
- 5
Nimekuwa nikifuatilia weledi wa OCD Mwombeji ya kuwaita wa-Tanzania wenzake kuwa ni panya nimefadhaika sana na mifumo yetu ya Ulinzi na Usalama wa raia.Kwa hicho kitendo cha kuwatukana wa-Tanzania wenzake nilidhani muda huu tunaoongea angekuwa mahabusu uchunguzi ukifanyika. Polisi ametenda kosa inaundwa tena timu ya kipolisi kufanya uchunguzi kujua kama Mwombeji aliwatukana watu kuwa ni panya. Hicho kiburi na jeuri vinatoka wapi?Anapaswa kukumbuka hayo maneno yaliwahi kutolewa na Hayati/Marehemu Muammar Gadafi lakini leo yuko wapi?Mwombeji kama unataka uongozi wa kisiasa sema uvue gwanda la kipolisi. Huyu mwombeji namatangaza ni janaga la Usalama wa Raia hasa wenye mlengo na CHADEMA.Tumeshuhudia maandamano ya UVCCM na wakati wa kesi ya Ole Sendeka lakini Mwombeji hakuchukua hatua zozote. Anafikia hatua ya kumwambia Mh. Lemma kuwa kesi ya kupinga ubunge wake itamtia "neno baya..............."