zomea zomea ya washabiki:tafsiri yangu

zomea zomea ya washabiki:tafsiri yangu

funaku

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2011
Posts
38,535
Reaction score
31,199
naamini wengi wetu tumeangalia mechi ya leo kati ya kili stars vs uganda cranes.mechi ilikuwa nzuri na timu yetu ya taifa ilipigana kufa na kupona lakini walizidiwa kimchezo.kitu cha kusikitisha mashabiki wetu hawakuonyesha uzalendo hata kidogo.walikuwa wanazomea kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa mchezo.
swali la kujiuliza je ni kipi kimewasibu mashabiki hawa?
Tafsiri yangu:kwa ujumla wananchi hawaridhishwi na mwenendo wa mambo nchini kama,ubinafsi,ufisadi na dharau za viongozi kwa wananchi.
 
Viongozi wetu wameshindwa uzalendo kwa nchi yao na kukumbatia vitendo vichafu dhidi ya raia wake itakuwaje wahabeki dhidi ya timu yao mbovu
 
Kuna dis-satisfication kubwa kuhusu mwenendo mzima wa timu ya taifa na mpira kuchezwa mdomoni zaidi bila mikakati ya kiscience ya kuendeleza kabubumbu nchini
 
kwa nini rwanda kila kitu wanatuzidi?why?why?maambuki ya vvu rate yao 3 per sisi 7 per,michezo,export ya chai kahawa,uchumi kukua,elimu kila mtoto laptop,usafi,rushwa ipo chini,omba omba sisi tunaongoza,lugha wao wana 4 english,french,nyarwanda,hutu or tusi sisi tunakipiga vita english tubaki na swahili tuu maana kikabila watoto wetu hawakijui kabisa
 
Ni taarifa kwa TFF na wizara ya michezo kwamba watanzania walishaacha kushabikia timu za ndani ni mashabiki wakubwa wa timu za nje km man u, Barca, zimbabwe, uganda, Rwanda nk. Utaona watakavyofurika uwanja wa taifa siku ya fainali.
 
Ni taarifa kwa TFF na wizara ya michezo kwamba watanzania walishaacha kushabikia timu za ndani ni mashabiki wakubwa wa timu za nje km man u, Barca, zimbabwe, uganda, Rwanda nk. Utaona watakavyofurika uwanja wa taifa siku ya fainali.

Inasikitisha sana! Nilichogundua ni kwamba ignorance level kwa wapenzi wa
 
Ni taarifa kwa TFF na wizara ya michezo kwamba watanzania walishaacha kushabikia timu za ndani ni mashabiki wakubwa wa timu za nje km man u, Barca, zimbabwe, uganda, Rwanda nk. Utaona watakavyofurika uwanja wa taifa siku ya fainali.

Inasikitisha sana! Nilichogundua ni kwamba ignorance level kwa wapenzi wa yanga ipo juu sana! Waelewa ni wachache mno!
 
Inasikitisha sana! Nilichogundua ni kwamba ignorance level kwa wapenzi wa yanga ipo juu sana! Waelewa ni wachache mno!

kwani ni mashabiki wa yanga tu?
 
WADANGANYIKA wamekua WATANGANYIKA wanonyesha Kutoridhishwa na namna mambo yanavyoendeshwa...huu ni mwanzo mziki mnene unakuja.
 
timu haina maadili michezaji mivuta bange milevi...we imagine mchezaji yuko kambini anakamatwa na zigo kalitoa kona bar anapinduana nalo ..sasa ataweza kweli kucheza mpira huyo au ni kutaka kututania tu ...
 
MKuu wale waliokuwa wanazomea ni mashabiki wa yanga. 7bu ya kuzomea ni uchache wa uteuzi wa wachezaji wa yanga kwenye timu iliyoshiliki haya mashindano na kudai kuwa haikuwa kili staz bali ni simba sports club kutokana na kuwa na wingi wa wachezaji.

wachezaji hao ni
1. Juma k juma
2. Juma jabu
3. S.kapombe
4.j.nyoso
5. M.kazimoto
6.h.moshi (baloteli)

kutoka yanga ni

nurdin bakari tu.
 
Back
Top Bottom