Zoezi la Uhakiki wa TIN, Katika hili TRA itafeli

Zoezi la Uhakiki wa TIN, Katika hili TRA itafeli

Shark

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2010
Posts
29,936
Reaction score
30,051
Wadau za Wikiend,

Leo Jumapili asubuhi hii nimemsikiliza Afisa wa Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA Bwana Isihaq Shariff akihojiwa na mtangazaji wa TV1 Ndg. Mukhsin Mambo amesema kua lengo la uhakiki wa TIN ni kwa ajili ya Watanzania WOTE wenye hizi TIN bila kujali kua wanazitumia kwa ajili ya gani. Ameelezea kua wanaohitajika kuhakiki ni wale wenye TIN za Biashara na zisizo za Biashara.

Nimefikiria kuhusu hii issue naona kama TRA kama vile wameshindwa kupanga, hivyo wanapanga kushindwa. Maana kuna kundi kubwa la watu wana hizi TIN lakini hawajijui kama wanailiki TIN. Hawa ni MADEREVA. Dereva yoyote mwenye Valid Driving License basi lazima atakua anamiliki TIN atake asitake. Lakini ni Dereva gani mwenye TIN ambae alishawahi kupewa Certificate yake wakati anapewa Driving License yake?? Je pale kwenye Dirisha au Dawati la TRA wanapotoa Driving Licence hua wanaambia madereva kua wao madereva ni wamiliki pia wa TIN ya TRA??

TIN hii kwa madereva hua haiandikwi kwenye Driving License ile kadi, bali pale mwanzo wakati anakata kwa mara ya kwanza na labda akapewa ile Temporary License ya karatasi ndio ataiona hiyo namba, je ni Dereva gani Mzoefu ambae anayo ile Temporary aliyopewa mara ya kwanza na bado anaitunza mpaka leo anaitunza?? Hata kama atakua anaitunza je anaweza kua anajua kama na yeye anahitajika kujihakiki na ile namba ndio inahusika?? Kwa elimu ipi iliyotolewa??

Idadi ya madereva au wamiliki wa Driving License ni kubwa sana, hasa tukiangalia magari yanayopita barabarani na kuweka foleni kuanzia asubuhi mpaka usiku ni ishara kua waendeshaji wa hayo magari wana valid Driving License (assumption) na wako wengi, je ni wote wanajua kwamba Leseni zao zina TIN hivyo wanahitaji kujihakiki??

Na ikitokea Madereva wengi wasijihakiki kutokana na kutokujua na hivyo kupelekea kufutwa kwa TIN zao kwenye system, TRA na serikali hawaoni kwamba wakati wa Ku-Renew hizo leseni itakua mvurugano mkubwa sana??

Mi nadhani TRA na serikali inabidi itoe ufafanuzi kua uhakiki wa hizi TIN unahusisha pia watu wote WENYE LESENI ZOZOTE ZA UDEREVA ili kuweza kupata idadi kamili ni wangapi wenye hizi TIN, otherwise iseme tu kua inahitaji TIN zile za Biashara tu ndio zihakikiwe. Lasivyo basi watakua wameshindwa kupanga, hivyo wanapanga kushindwa...!!!!
 
Kwenye TIN wanahakiki nini? Uhakiki utatekelezwaje, kwa kumtafuta mwenye TIN mahali alipo au vipi? Maana wapo wengi kweli.
 
Wadau za Wikiend,

Leo Jumapili asubuhi hii nimemsikiliza Afisa wa Elimu kwa Mlipa Kodi Bwana Isihaq Shariff akihojiwa na mtangazaji wa TV1 Ndg. Mukhsin Mambo amesema kua lengo la ukakiki wa TIN ni kwa ahili ya Watanzania WOTE wenye hizi TIN bila kujali kua wanazitumia kwa ajili ya gani. Ameelezea kua wanaohitajika kuhakiki ni wale wenye TIN za Biashara na zisizo za Biashara.

Nimefikiria kuhusu hii issue naona kama TRA kama vile wameshindwa kupanga, hivyo wanapanga kushindwa. Maana kuna kundi kubwa la watu wana hizi TIN lakini hawajijui kama wanailiki TIN. Hawa ni MADEREVA. Dereva yoyote mwenye Valid Driving License basi lazima atakua anamiliki TIN atake asitake. Lakini ni Dereva gani mwenye TIN ambae alishawahi kupewa Certificate yake wakati anapewa Driving License yake?? Je pale kwenye Dirisha au Dawati la TRA wanapotoa Driving Licence hua wanaambia madereva kua wao madereva ni wamiliki pia wa TIN ya TRA??

TIN hii kwa madereva hua haiandikwi kwenye Driving License ile kadi, bali pale mwanzo wakati anakata kwa mara ya kwanza na labda akapewa ile Temporary License ya karatasi ndio ataiona hiyo namba, je ni Dereva gani Mzoefu ambae anayo ile Temporary aliyopewa mara ya kwanza na bado anaitunza mpaka leo anaitunza?? Hata kama atakua anaitunza je anaweza kua anajua kama na yeye anahitajika kujihakiki na ile namba ndio inahusika?? Kwa elimu ipi iliyotolewa??

Idadi ya madereva au wamiliki wa Driving License ni kubwa sana, hasa tukiangalia magari yanayopita barabarani na kuweka foleni kuanzia asubuhi mpaka usiku ni ishara kua waendeshaji wa hayo magari wana valid Driving License (assumption) na wako wengi, je ni wote wanajua kwamba Leseni zao zina TIN hivyo wanahitaji kujihakiki??

Na ikitokea Madereva wengi wasijihakiki kutokana na kutokujua na hivyo kupelekea kufutwa kwa TIN zao kwenye system, TRA na serikali hawaoni kwamba wakati wa Ku-Renew hizo leseni itakua mvurugano mkubwa sana??

Mi nadhani TRA na serikali inabidi itoe ufafanuzi kua uhakiki wa hizi TIN unahusisha pia watu wote WENYE LESENI ZOZOTE ZA UDEREVA ili kuweza kupata idadi kamili ni wangapi wenye hizi TIN, otherwise iseme tu kua inahitaji TIN zile za Biashara tu ndio zihakikiwe. Lasivyo basi watakua wameshindwa kupanga, hivyo wanapanga kushindwa...!!!!
Nchi hii kila kitu ni kukurupuka tu.

Walichotakiwa kufanya ni: -

1. Uhakiki ufanyike wakati wowote au pale mteja anapokwenda kupata huduma husika.

2. Kuwe na tin ya aina moja tu, sio udereva wala biashara

3. Uhakiki ufanyike kwa njia ya mtandao.
 
Kwenye TIN wanahakiki nini? Uhakiki utatekelezwaje, kwa kumtafuta mwenye TIN mahali alipo au vipi? Maana wapo wengi kweli.
Ukichukua TIN hua unasema unaenda kuifanyia nini, na pia hua unaweka details zako kua wewe ni mkazi wa wapi.
Sasa inawezekana umehama, matumizi ya TIN yamebadilika au hata umefariki. So wanataka kubaki na valid and updated TINs
 
watanzania ni wataalamu wa kutumia fursa ili kupata. sasa kuna uhakiki, kila mmoja anajipanga kuitumia hiyo fursa, vikao, mikutano na safari haviishi. mpaka itakapoisha hela ndo wakubwa watashtuka. tukumbuke majuto ni mjukuu.
 
Hivi tunakwenda "kuhakiki" TIN zetu au ni kufanya usajili mpya wa TIN ili kila mlipa kodi apate TIN moja tu? Na kama ni kuhakiki kwa maana ya kujua kama unayo, hauna au uhalisia wa TIN yako kama itagundulika kuwa TIN yako ni fake au haionekani kwenye system yao ile leseni (mfano ya udereva) uliyo nayo itahesabiwa kuwa ni fake au? Na nini kinafuata baada hapo?

Na kama TIN ni Taxpayer's Identification Number ni kwa nini miaka yote waajiriwa katika sekta zote za umma na binafsi wamekuwa wakikatwa PAYE lakini bila kupewa TIN wakati ni walipaji wazuri wa kodi kutoka kwenye mishahara yao? Na je si wakati muafaka kwa kipindi hiki huu uhakiki wa TIN unavyoendelea hawa waajiriwa nao wakapewa TIN zao ili kuwapunguzia usumbufu usio wa lazima siku za usoni?
 
Wadau za Wikiend,

Leo Jumapili asubuhi hii nimemsikiliza Afisa wa Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA Bwana Isihaq Shariff akihojiwa na mtangazaji wa TV1 Ndg. Mukhsin Mambo amesema kua lengo la uhakiki wa TIN ni kwa ajili ya Watanzania WOTE wenye hizi TIN bila kujali kua wanazitumia kwa ajili ya gani. Ameelezea kua wanaohitajika kuhakiki ni wale wenye TIN za Biashara na zisizo za Biashara.

Nimefikiria kuhusu hii issue naona kama TRA kama vile wameshindwa kupanga, hivyo wanapanga kushindwa. Maana kuna kundi kubwa la watu wana hizi TIN lakini hawajijui kama wanailiki TIN. Hawa ni MADEREVA. Dereva yoyote mwenye Valid Driving License basi lazima atakua anamiliki TIN atake asitake. Lakini ni Dereva gani mwenye TIN ambae alishawahi kupewa Certificate yake wakati anapewa Driving License yake?? Je pale kwenye Dirisha au Dawati la TRA wanapotoa Driving Licence hua wanaambia madereva kua wao madereva ni wamiliki pia wa TIN ya TRA??

TIN hii kwa madereva hua haiandikwi kwenye Driving License ile kadi, bali pale mwanzo wakati anakata kwa mara ya kwanza na labda akapewa ile Temporary License ya karatasi ndio ataiona hiyo namba, je ni Dereva gani Mzoefu ambae anayo ile Temporary aliyopewa mara ya kwanza na bado anaitunza mpaka leo anaitunza?? Hata kama atakua anaitunza je anaweza kua anajua kama na yeye anahitajika kujihakiki na ile namba ndio inahusika?? Kwa elimu ipi iliyotolewa??

Idadi ya madereva au wamiliki wa Driving License ni kubwa sana, hasa tukiangalia magari yanayopita barabarani na kuweka foleni kuanzia asubuhi mpaka usiku ni ishara kua waendeshaji wa hayo magari wana valid Driving License (assumption) na wako wengi, je ni wote wanajua kwamba Leseni zao zina TIN hivyo wanahitaji kujihakiki??

Na ikitokea Madereva wengi wasijihakiki kutokana na kutokujua na hivyo kupelekea kufutwa kwa TIN zao kwenye system, TRA na serikali hawaoni kwamba wakati wa Ku-Renew hizo leseni itakua mvurugano mkubwa sana??

Mi nadhani TRA na serikali inabidi itoe ufafanuzi kua uhakiki wa hizi TIN unahusisha pia watu wote WENYE LESENI ZOZOTE ZA UDEREVA ili kuweza kupata idadi kamili ni wangapi wenye hizi TIN, otherwise iseme tu kua inahitaji TIN zile za Biashara tu ndio zihakikiwe. Lasivyo basi watakua wameshindwa kupanga, hivyo wanapanga kushindwa...!!!!
Mkuu hili zoezi linaisha lini maana hata Mimi nataka nielekee Huko
 
Mimi inanishangaza kumhitaji mwenye TIN namba afike binafsi ili achukuliwe alama za vidole. Hizi alama tumechukuliwa kwa mbwembwe nyingi kwenye kupiga kura, vitambulisho vya taifa, leseni nk. hivi taarifa hizi siyo za kitaifa na taasisi zinazohitaji zinaweza kuzipata huko? Kweli watanzania tunajua kupotezeana muda. Bora tuletewe hao wataalamu wa Rwanda watufundishe kucentralise data. Tutapotezeana muda kweli kweli kwa jambo ambalo lingeweza kufanyika kimtandao....poor TRA without vision!!!
 
Wadau za Wikiend,

Leo Jumapili asubuhi hii nimemsikiliza Afisa wa Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA Bwana Isihaq Shariff akihojiwa na mtangazaji wa TV1 Ndg. Mukhsin Mambo amesema kua lengo la uhakiki wa TIN ni kwa ajili ya Watanzania WOTE wenye hizi TIN bila kujali kua wanazitumia kwa ajili ya gani. Ameelezea kua wanaohitajika kuhakiki ni wale wenye TIN za Biashara na zisizo za Biashara.

Nimefikiria kuhusu hii issue naona kama TRA kama vile wameshindwa kupanga, hivyo wanapanga kushindwa. Maana kuna kundi kubwa la watu wana hizi TIN lakini hawajijui kama wanailiki TIN. Hawa ni MADEREVA. Dereva yoyote mwenye Valid Driving License basi lazima atakua anamiliki TIN atake asitake. Lakini ni Dereva gani mwenye TIN ambae alishawahi kupewa Certificate yake wakati anapewa Driving License yake?? Je pale kwenye Dirisha au Dawati la TRA wanapotoa Driving Licence hua wanaambia madereva kua wao madereva ni wamiliki pia wa TIN ya TRA??

TIN hii kwa madereva hua haiandikwi kwenye Driving License ile kadi, bali pale mwanzo wakati anakata kwa mara ya kwanza na labda akapewa ile Temporary License ya karatasi ndio ataiona hiyo namba, je ni Dereva gani Mzoefu ambae anayo ile Temporary aliyopewa mara ya kwanza na bado anaitunza mpaka leo anaitunza?? Hata kama atakua anaitunza je anaweza kua anajua kama na yeye anahitajika kujihakiki na ile namba ndio inahusika?? Kwa elimu ipi iliyotolewa??

Idadi ya madereva au wamiliki wa Driving License ni kubwa sana, hasa tukiangalia magari yanayopita barabarani na kuweka foleni kuanzia asubuhi mpaka usiku ni ishara kua waendeshaji wa hayo magari wana valid Driving License (assumption) na wako wengi, je ni wote wanajua kwamba Leseni zao zina TIN hivyo wanahitaji kujihakiki??

Na ikitokea Madereva wengi wasijihakiki kutokana na kutokujua na hivyo kupelekea kufutwa kwa TIN zao kwenye system, TRA na serikali hawaoni kwamba wakati wa Ku-Renew hizo leseni itakua mvurugano mkubwa sana??

Mi nadhani TRA na serikali inabidi itoe ufafanuzi kua uhakiki wa hizi TIN unahusisha pia watu wote WENYE LESENI ZOZOTE ZA UDEREVA ili kuweza kupata idadi kamili ni wangapi wenye hizi TIN, otherwise iseme tu kua inahitaji TIN zile za Biashara tu ndio zihakikiwe. Lasivyo basi watakua wameshindwa kupanga, hivyo wanapanga kushindwa...!!!!
Kwa kifupi labda uwenda nitakuwa nimekusaidia kwa namna moja ama nyinge.
Zile tin za mwanzo zilikuwa na kasoro chache ambazo kwa sasa zimerekebishwa.
moja ya kasoro ,kwenye ujazaji wa form kunakipengere cha barua pepe ambacho kiuhalisi akiwezi kusaidi kumfanya ofisa kukujua ulipo. Kwahiyo badala ya kusema barua pepe tu, inakuhitaji uonyeshe physical address yako pamoja nanamba ya plot.Pia katika inshu ya leseni haina aja ya kutembea na tin number kama unayo leseni yako. system ya tra inatambua driving license number katka upatikaji ama utambuzi wa tin namba yake. Pia ukiwa na majina yako matatu ambayo ulisajiliwa kwenye tin number,yanaweza kukusaidia kupata tin number yako.
Kwa mfano ukiwa unakwenda tra kurenewal leseni yako,kunaform utatakiwa kujaza ambazo kunasehemu inakuonyesha ujaze drving licence number yako pamoja na mwaka na sehemu ilipotolewa.kama umesahau tin number yako itakusaidia kuonekana .
Khasante
 
Wenye TIN wamekuambia wote wana plot no. Na permanent address Na hawatakaa wahame? Jibu swali hizo taarifa unazotaka kama alama za vidole unaweza kuzipata bila kutuhitaji. Kwa utendaji huu wa kusahihisha makosa yenu kwa kuwaita watanzania tuseme kama zaidi ya asilimia 20 ofisini ni uzembe uliotukuka. Baada ya miaka 10 wenzenu wataona mlikosea watataka kubadilisha tena. Na siyo lazima iwe ni kukosea bali kuboresha na watu watakuwa asilimia 40 wana TIN.muwaite tena waje ofisini. Kadhalika Hakuna haja ya deadline. Mmeshauriwa mtu ashughulikiwe pale anapotaka huduma kama kurenew licence au kulipa kodi hamsikii ni longolongo tuu. Kwenye mtandao kuna mawazo mazuri hamtaki kuyachukua. Mtapoteza muda wa wafanyakazi wengi kwa gharama kubwa bila sababu. Ufafanuzi wenu ni upuuzi mtupu ngoja tuone
 
Kwa kifupi labda uwenda nitakuwa nimekusaidia kwa namna moja ama nyinge.
Zile tin za mwanzo zilikuwa na kasoro chache ambazo kwa sasa zimerekebishwa.
moja ya kasoro ,kwenye ujazaji wa form kunakipengere cha barua pepe ambacho kiuhalisi akiwezi kusaidi kumfanya ofisa kukujua ulipo. Kwahiyo badala ya kusema barua pepe tu, inakuhitaji uonyeshe physical address yako pamoja nanamba ya plot.Pia katika inshu ya leseni haina aja ya kutembea na tin number kama unayo leseni yako. system ya tra inatambua driving license number katka upatikaji ama utambuzi wa tin namba yake. Pia ukiwa na majina yako matatu ambayo ulisajiliwa kwenye tin number,yanaweza kukusaidia kupata tin number yako.
Kwa mfano ukiwa unakwenda tra kurenewal leseni yako,kunaform utatakiwa kujaza ambazo kunasehemu inakuonyesha ujaze drving licence number yako pamoja na mwaka na sehemu ilipotolewa.kama umesahau tin number yako itakusaidia kuonekana .
Khasante
Mkuu,
Unaweza kua umesaidia ila swali la msingi bado hujasaidia.
Issue ni kua "Je Madereva wenye Leseni zao za Udereva wanajijua kua wao ni wamiliki pia wa TIN hivyo na wao wanatakiwa kwenda kujihakiki"??
 
kiukweli zoezi linachangamoto zake , katika ushawishi kwa wananchi,binafsi mimi si msemaji wa tra wala afisa habari wa tra. lakini kwa machache ninayoyafahamu najaribu kushare nanyi ili tuendele kuelekezana zaidi na kujitokeza kwenda kwenye ofisi za mamlaka kuweza kubadirisha tin namba yako.
Kiukweli ili zoezi linamuonekano mzuri katika kufanikisha upatikanaji wa taarifa kwa usahihi na kwa haraka. Kwa mfano ofisa anaweza kumtambua mlipa kodi mahali anapoishi kwa kuangalia tin yake kwa kutumia tin za sasa tofauti na zile za manzo ambazo zinakufanya uingie kwenye system ama uwende kutafuta kwenye mafile ndipo uweze kuendelea kumuhudumia mlipa kodi.
pia zoezi lina update tarifa za walipa kodi wote na kuwatambua wapi ni dormant , active nk.
kuhusu madereva kama wanajitambua endepo kama wanajiju wanamiliki tin namba. Binafsi naweza nikajibu YES wanajijua!
hii inatokana na kwamba dereva hawezi kuhudumiwa pasipo tin namba. hii inamaanisha nikwamba,pasipo tin huwezi kupata leseni.
 
TRA imeamua kutafuta TIN hewa ili nao waorodheshwe kwenye idara zilizofanya UHAKIKI maana ndio kipaumbele cha awamu ya tano.. kuhakiki hewa.
 
Ya ni kweli kiongozi... tra kwa kukurupuka ndo wenyewe...
Lakini pia muda wa ku renew hizi TIN wameweka mfupi mno, wakati wanajua kwamba network yao iko polepole sana kuliko kobe. Siku niliyokwenda ku renew TIN yangu pale TRA Shaurimoyo nilitumia almost saa nne. Sasa nani yuko tayari kupoteza muda wake wa saa nne kufanya marekebisho ya TIN?
 
Back
Top Bottom