kyalankota
JF-Expert Member
- Jul 27, 2014
- 2,594
- 1,463
Zoezi la uandikishaji wa wapiga kura kwa njia ya teknolojia ya kisasa ya BVR kwa Wilaya ya Ilala limeanza na dosari kwa sintofamu ya majina ya waliochaguliwa kama BVR Kit Operators na waandishi wasaidizi baada ya usaili kuwa na usiri mkubwa wa namna ya kuyaona ili wahusika wajue wamepangwa kata gani kwa ajili ya zoezi litakaloanza tarehe 16 july wiki ijayo!
Wilaya zingine za Kinondoni na Temeke tayari wameshabandika kwenye Kata zao na tarehe za kufanya semina kwa ajili ya maelekezo namna ya uandikishaji imeshapangwa kuwa ni tarehe 13 na 14 wiki ijayo.
Inasemekana kuna namna inafanyika kimyakimya kuwapa taarifa wale wanaohitajika kwa lengo maalum kwa ajili ya maslahi ya watu fulani.
Sasa hii ni hatari.
Wilaya zingine za Kinondoni na Temeke tayari wameshabandika kwenye Kata zao na tarehe za kufanya semina kwa ajili ya maelekezo namna ya uandikishaji imeshapangwa kuwa ni tarehe 13 na 14 wiki ijayo.
Inasemekana kuna namna inafanyika kimyakimya kuwapa taarifa wale wanaohitajika kwa lengo maalum kwa ajili ya maslahi ya watu fulani.
Sasa hii ni hatari.