Ziwa Mwananyamala Dar es salaam

Ziwa Mwananyamala Dar es salaam

Kijakazi

Platinum Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
9,334
Reaction score
15,038
Nimekuwa nikisoma Historia ya jiji letu la Dar, naona kwamba kuna Ziwa Mwananyamala lililoko Mwananyamala, sasa nashangaa kwa maana katika maisha yangu yote sijawahi kusikia kwamba Mwananyamala kuna Ziwa!
Je kuna mtu anafahamu juu ya hili, au kuna ambaye ameshawahi kuona Ziwa Mwananyamala kwa wanaoishi huko? na liko Mwananyamala sehemu gani?


attachment.php
 
Sio kisiwa hicho? Ambacho kilizaa mwananyamala kisiwani?fanya utafiti wa kina mkuu inawezekana ndio chanzo cha hilo ziwa
 
Ziwa hilo sijawahi kulisikia. Mimi najua ule mto unaotokea ubungo Msewe, Sinza, Tandale hadi Bonde la Mkwajuni mpaka Jangwani then unaenda kumwaga Baharini. Na huu mto unatenganisha Mwananyamala na Tandale, Na shule iliyopo karibu kidogo na huu mto sio Mwananyamala "B",ni Mwananyamala Kisiwani. Kwa upande wa Kinondoni unatenganisha Magomeni na Kinondoni Mkwajuni
 

Maji ya kifuu ni BAHARI ya CHUNGU (sisimizi)

Hata Singida kuna ziwa KINDAI

Morogoro nako kuna ziwa MINDU

Kwahiyo sitashangaa mwananyamala kama nako kuna ziwa Mwananyamala!
 
Yapo maziwa matatu
La kwanza lipo karibu na shule ya sekondari ya Kambagwa,
La pili lipo nyuma ya mahakama ya Kivukoni
La tatu lipo nyuma ya kanisa la KKKT Kinondoni
 
hakuna ziwa mwananyamala.labda useme bonde mwananyamala.
 
Ziwa hilo kwa sasa limeshakuwa nchi kavu. Hata ramani ya sasa haionyeshi. Naomba niweke picha ya MAP View na Earth View
Hapo kwenye alama NYEKUNDU ndipo lilipokuwa
Mwananyamala.GIF
Mwananyamala Earth view.GIF
 
'duh,wee jamaa unabishana na google asee si mchezo ndugu yangu...'

attachment.php

Mimi mwenyewe kukua kwangu kote nimekuja kujua ziwa mwnyamala baada ya kuanza kutumia google map lakini siku zote nilikuwa najua kuna bwawa.Labda wataalamu wa hydrology waje watutofautishie kati ya bwawa na ziwa.Kumbuka hao google nao ni binadamu.
 
Nimekuwa nikisoma Historia ya jiji letu la Dar, naona kwamba kuna Ziwa Mwananyamala lililoko Mwananyamala, sasa nashangaa kwa maana ktk maisha yangu yote sijawahi kusikia kwamba Mwananyamala kuna Ziwa!
Je kuna mtu anafahamu juu ya hili, au kuna ambaye ameshawahi kuona Ziwa Mwananyamala kwa wanaoishi huko? na liko Mwananyamala sehemu gani?


Hilo ni bwawa tu lililokuwa pale karibu na Mahakama ya mwanzo ya Kinondoni na wala halikufikia level ya kuwa Ziwa, bwawa kama hilo pia lilikuwa pale Magomeni mwembechai shule ya Karume, palipojengwa ile fuel station
 
yaah kweli ziwa mwananyamala lipo ila ndo linapotea maana wakazi wanalifukia kwa kila njia wawezayo
 
Mimi mwenyewe kukua kwangu kote nimekuja kujua ziwa mwnyamala baada ya kuanza kutumia google map lakini siku zote nilikuwa najua kuna bwawa.Labda wataalamu wa hydrology waje watutofautishie kati ya bwawa na ziwa.Kumbuka hao google nao ni binadamu.

Kwa hivyo kama ni binadam unamaanisha hoja yako inakataa uwepo wa ziwa hilo mosi,pili wee umesema umejua baada ya kutumia G map una uhakika kila mtu ana G map kama ulivyokuwa nayo wewe...............jibu kwanza mengine yatakuja kutokana na majibu yako usiulize swali juu ya swali,karibu.
 
Back
Top Bottom