Zitto Z. Kabwe,tafuta mshauri!

Zitto Z. Kabwe,tafuta mshauri!

Status
Not open for further replies.
Ngoja niongeze ushauri tena. Zitto, unaweza kudhani chama kinahitaji mabadiliko ya viwango vya juu sana, nyie mnaita total overhaul ya chama. Lakini kwenye andiko lenu mmesisitiza kwamba viongozi wa juu wa Chadema mnaotaka wawapishe wanajivika ndoto za alinacha kudhani wakiingia serikalini watafanya total overhaul ya serikali.

Sasa hiyo si ni contradiction kwa upande wenu? Nyie mnaamini katika total overhaul ya chama, lakini hamuamini overhaul ya serikali. Hiyo ni ishara ya unafiki. Viongozi wako walipokuwa wakisoma hilo andiko, mara moja walinusa harufu ya unafiki, maana hata wewe ni mmjoa wao. Kama uongozi wote wa juu unahitaji total overhaul basi hata na wewe ulipsawa kuwa overhauled.

Somo: Usithubutu kuhamisha lawama kwa mtu mwingine iwapo mambo hayaendi sawa.
 
Ana siku kumi tu zakuendelea kuwa mwanachama wachadema au mpinzani wachadema

Yericko,

Zitto anaweza kuwa mbaya kwa sasa, lakini anaweza kuwa asset kubwa kwa chama pia baada ya haya. Msilenge katika kurudi nyuma, kuna nafasi kubwa sana ya kurekebisha haya na mkasonga mbele. Kama ndani ya mioyo yenu hamna nafasi ya kusameheana na kurekebishana basi hamfai kanisani, hamfai misikitini na hamfai Tanzania pia.
 
Ndio maana wengine tunaamini Zitto ana lake jambo.Hakuna jambo analofanya linaloonesha collective responsibility zaidi ya kujijenga yeye binafsi.Kwa nafasi yake lazima anajua siri na mambo mengi ya chama lakini hizo haziwezi kuwa silaha ya kuogopwa kama mtu unatumwa na dhamira safi.

Na hii mie naisema hapa kila siku Ziito speaks for himself never ever for Chadema, watu wanaomshabikia Zitto sijui hawaoni hizi facts ambazo ziko wazi wazi kabisa, mleta mada umeiweka vizuri sana.
 
Akae atulize akili kwanza siasa za bongo ni kama upepo unavuma kus na kas.walikuwepo akina mrema miaka ile ya 90 cku siku hiz wako kimya
 
Mtei ndio pkee mwenye chama mamlaka ya kuchagua viongozi wa chadema
 
Kaka huyu Zitto ni wa kawaida sana, kinachofanya aonekana ana hoja na kuwa na mvuto kwa wananchi ni kwa sababu ya Magamba. Siku magamba yakimtenga yasimtumie atakosa pa kuegemea, atakosa pesa ya kumfanya awe jeuri na kiburi. Hoja nyingi anazoibua Bungeni ni kwa sababu ya makundi ndani ya magamba kutaka kumalizana kwa hiyo wanamtumia huyu jamaa aziibue hizo hoja.
Bei ya Zitto wanaijua CCM.
Its possible they are blackmailing this Zitto, amekula pesa zao nyingi sana. They can use him in anyway they want.
 
Zitto sasa anataka kuwa kama Kafulila?
 
THIS IS THE BIGGEST OPPORTUNITY FOR CHADEMA

nawashangaa watu wote wanaomsupport zitto. hoja zote zinazojengwa na hao watu ni kwa ku-ignore the fact that mipango yao ya siri ilikua na backup ya CCM. sasa unategemea nini kwa zitto kushika madara ya juu CHADEMA chini ya usaidizi wa CCM. ni mtu mwenye akili fupi tuu ndio hataelewa hili.

1. Idea for suporting zitto was introduced and promoted my CCM. and then zitto knew it and he accepted the deal
2. Strategic plans and set up was done by Kitila Mkumbo and Mwigamba.
3. FINANCIAL BACKUP, INTELLIGENCE SERVICES, AND PLANNED STRATEGIES WERE EXECUTED BY CCM AND SOME OF TISS MEMBERS

hawa wote wanaojitetea... wanajitetea kwa kutokana na hiyo point no 1 and 2. lakini kwa ujanja wao na upotishaji wao wa maukusudi wanafunika hiyo fact no 3

Zitto must be complitely terminated...

ACTION PLAN A = Kumvua madaraka = pre-emptive strike.
1. hao akina zitto na team yake wanachofanya sasa ni kuhakikisha chadema haiwavui uanachama. kuto mvua zito uanachama itakukua ni ushindi kwa zitto.. na ataendelea na mipango yake miovu ya kukiharibu chama....kwa maana atakua ndani ya chama bado...
2. kuto mvua uanachama zitto kutafanya aanze kukusanya wafuasi ndani ya majukwaa ya chadema waziwazi na hatimae kuharibu chama kabisa.
3. akiachwa atajifanya mwaminifu sana na mwenye nia njema... (hii ataifanya pia kwa ajiri ya kudaka wafuasi wake wengi zaidi)

ACTION PLAN B = kumvua uanachama = must be the target action to take
. Lazima mtu huyo asiwe mwanachama wa CHADEMA tena… atahaha kwa muda lakini hatakua na effect.. safi sana CC kwa kumpa 14 days-days ambazo watu wengi tayari tumeshajiridhisha kua huyu jamaa sii mwema kabisa.

FAIDA ZA ACTION B
1. CHADEMA itajidhihirisha kua kweli wako serious na kwa maana hiyo wataingia madarakani kwa kishindo kikuu.. na kwa ouga wa hali ya juu... watu wataacha ufisadi na ujinga wote (irresponsibility) ndani ya serikali.
2. viongozi na wanachama wote wa CDM watakua moyo mmoja with one passion, one vision and one mission kuhakikisha kua chama kinashinda uchaguzi.
mamluki hawatakua na nafasi tena... na kila mamluki ataweza kumulikwa kirahisi sana.
3. hakutakua na lelemama tena.. kila iliye chadema atakua very serious na majukumu ya kichama na kitaifa.
4. CHADEMA wataingia madarakani wakiwa ni wamoja… ready for drastic development of this nation.

Huyo jamaa ana roho wa kiburi, roho wa kujigamba, roho wa misifa, roho wa ubinafsi(u-mimi), roho ya dharua na USALITI

NCHI HII MUNGU HATARUSU KUSHIKWA NA WASHIRIKINA, WANAMITANDAO, WACHEZA RAFU NA WOTE WANAOAMINI KATIKA UCHAWI. WALE WOTE WANAOABUDU SHETANI KWA KUPITIA WAGANGA WA KIENYEJI. NCHI HAITASHIKWA TENA NA WATU WA MAZINGAOMBWE…
...Mzee una akili sana mkuu..heko kwako....Tumaini makene na CDM wote chukueni ushauri huu...hapa mtafunga mwaka CDM ikiwa juu..kama tungekua tunaendesha polls CDM ingekuwa juu sana
 
Kama ndivyo, ndio maana inasemwa huyo jamaa ama hajakomaa kisiasa au sio mwanasiasa mahiri kama anavyotaka jamii imwelewe. Alikuwa na hasira na chama? Bahati mbaya kwake kakutana na visiki; kwa nini Slaa kamwachia Mnyika amjibu? Hizi siasa zina wenyewe Mkuu. Ukiingia kichwa kichwa au kwa mihemuko au kwa kiburi utajiumiza mbaya.

Mkuu nimecheka sana..jamaa kapewa Mnyika amjibu....hahahahah.!
 
Ukiendelea hivi hautafanikiwa kamwe. Hautafika mbali.Utaishia njiani. Hutapata utakacho. Tafadhali tafuta Mshauri wako mbobezi wa mambo ya kisiasa ili awe anakushauri kabla ya kuamua. Bado hujitoshelezi kisiasa. Kweli kabisa. Labda kiuchumi-kwakuwa nawe ni mchumi.

Lakini, Mshauri hakwepeki. Shauriwa kwanza;amua baadaye.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Very well said Vuta Nikuvute. Huyo Zitto alishupaza shingo muda wote aliposhauriwa na sasa shingo imevunjika, atajuta.

Angalia "washauri" na wapambe wake, utamjua Zitto vizuri zaidi. Watazame marafiki zake wa karibu utamfaham kwa undani zaidi.

Frankly, Zitto is never half good of who he thinks, and also he's not half good of what he pretends.
 
Yericko,

Zitto anaweza kuwa mbaya kwa sasa, lakini anaweza kuwa asset kubwa kwa chama pia baada ya haya. Msilenge katika kurudi nyuma, kuna nafasi kubwa sana ya kurekebisha haya na mkasonga mbele. Kama ndani ya mioyo yenu hamna nafasi ya kusameheana na kurekebishana basi hamfai kanisani, hamfai misikitini na hamfai Tanzania pia.

CHADEMA sio kanisa mkuu.Watu wanakwenda hatua tano mbele kwa jasho na damu, halafu watu fulani tu ndani ya chama wanataka wakurudishe hatua kumi nyuma kwa vile wao ni wasomi!Hiyo haikubaliki hata kidogo.Na hii ni kumdhirihishia kuwa Chadema si zitto bali ni taasisi imara na yenye nguvu.Vijana wengi walishamjua kitaambo huyu jamaa kuwa kanunuliwa!ataondoka na wale anaowahonga vihela kutoka kwenye mihela aliyopewa

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Ukiendelea hivi hautafanikiwa kamwe. Hautafika mbali.Utaishia njiani. Hutapata utakacho. Tafadhali tafuta Mshauri wako mbobezi wa mambo ya kisiasa ili awe anakushauri kabla ya kuamua. Bado hujitoshelezi kisiasa. Kweli kabisa. Labda kiuchumi-kwakuwa nawe ni mchumi.

Katika Mkutano wenu na Waandishi wa Habari juzi,hukupaswa kutaja tuhuma zote zilizojadiliwa ndani ya Kamati Kuu. Kutaja tuhuma zile ni kutoa siri za vikao nje na kujitetea pasipostahili. Sasa ulipojibu pale tuhuma moja baada ya nyingine ulikuwa unamjibu nani? Ili iweje? Kwa ajili ya kumbukumbu gani?

Ndugu Zitto, yawezekana unachokiamini kuwa una uwezo wa kuongoza chochote popote hapa nchini ni kweli. Lakini,imani yako isikuendeshe. Nenda nayo taratibu. Utafika tu! Ukiruhusu machagizo ya vyombo vya habari kukukimbiza mbio kuelekea unapopataka,utajikwaa;utaanguka na kuumia.

Siku ile, ungesema hivi tu: " Nayaheshimu Maamuzi ya chama changu. Nitayamaliza mambo haya kwa mujibu wa Katika na Kanuni za chama changu. Na kwasasa, sina mpango wa kuhama toka CHADEMA.Hatoki mtu hapa." Basi.Ungesubiri maswali na halafu uyajibu. Hapo, ungepata wasaa mzuri wa kuelezea kwa makini na uangalifu mkubwa mambo yako. Watu wangeshangaa.Wangekusifu. Kukosekana kwa Mshauri kumekufanya uongee mengi yenyemshiko haba.

Itoshe kusema kuwa, Zitto Zuberi Kabwe ni mwanasiasa. Bado yuko safarini.Safari ya mafanikio zaidi. Lakini,anapaswa kuwa makini.Aongee kwa kuchagua maneno;kuzingatia hadhira na kuuchuja ujumbe. Achangamane na wenzake chamani. Wawe kitu kimoja. Wasonge mbele. Lakini, Mshauri hakwepeki. Shauriwa kwanza;amua baadaye.

Kila la kheri katika siku zako 14 za utetezi. Yatakwisha tu haya. Wajibu waliokutuhumu. Sisi tunasubiri matokeo tu.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Naona huelewi msingi wa ukweli na uwazi. alichokifanya ZZK na Kitila ndio sahihi wananchi wajue yanayojiri ndani ya chama hicho wakielewe vizuri wakihukumu kwa haki na siyo unafiki. Mambo ya kubebana ,kufichiana siri na zidumu fikra sahihi za mwenyekiti (HATA KAMA SIYO SAHIHI )yako CCM ndio maana kimepoteza umaarufu kimebaki kinanunua wananchi kwa fedha. BIG UP ZZK NA KITILA KWA UKWELI NA UWAZI. Wamelianzisha sasa ni mbele kwa mbele. hatishwi mtu hapa
 
Kiongozi mtimuliwa anadhani anaweza yote kwa hio hahitaji Mshauri!!
cha kushangaza mama yake anasema alifurahi
 
Nakukubali mzee wa lumumba kijana safari bado ndefu, awe makini, watawala na watawaliwa,ndio watanzania na ndio wapigakura.
 
Mtu anaandaa waraka kwamba uongozi wa juu wa CDM haufai...wakati yeye ni mmojwapo wa kiongozi wa juu.....
 
Mtei ndio pkee mwenye chama mamlaka ya kuchagua viongozi wa chadema

Mkuu kwani Leo ndio waanza kufatilia siasa za bongo?,mkapa alichaguliwa na nani kugombea urais 1995?,chama chochote Kina watu ambao wana maamuzi ya mwisho,hii ipo vyama vyote na tena ni zaidi Huko CCM kwani Huko mnafikia hadi hatua ya kumwambia mtu sio Raia Kama hamumtaki,so stop using this cheap card,THINK!
 
Viongozi wanakerwa na kitendo cha mtei kuwachagula viongozi utadhani ile ni kampuni yake binafsi

Mwaka 1995 hayati mwl. Nyerere aliwapiga chini boys II men walioenda Dodoma kwa mbwembwe kwenye mkutano uliokuwa ukiendelea wakati huo kwa ajili ya kuteua mgombea atakayepeperusha bendera ya CCM kwenye kinyag'anyiro cha urais wa JMT mwaka huo. Badala yake aliwashawishi wajumbe wamkubali Mkapa ambaye ndiyo chaguo lake, lakini CCM hakulalamika kwamba Nyerere anawachagulia viongozi? Mlifyata mkia, hakuna siasa ya majitaka mbele ya genius Julius Kambage Nyerere.

Leo CCM inasukuma mapandikizi kushika madaraka ya juu ndani ya CDM kwa kigezo cha demokrasia hata kama watu wenyewe hawana sifa muhimu kama uadilifu na staha. Ni nini kinawapa muwashawasha na masuala ya ndani ya Chadema? Acheni Mtei apendekeze watu anaowaona ni waadilifu na wachapakazi ndani ya CDM kwa kadri ya uzoefu wake wa kisiasa na umri wake pia. Mtei ni mzee, anajua mengi, ameona mengi katika maisha yake na anauzoefu wa kutosha katika kila jambo kulinganisha na hawa mavijana wa aina ya aina Zitto, Kitila na Mwigamba achilia mbali chafuchafu aina ya akina Shonza, Mwapamba, Mwigulu na Nape.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom